Fanya yafuatayo kulinda afya ya uke

Fanya yafuatayo kulinda afya ya uke

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
0001-17960324776_20210308_125550_0000.png


Usafi wa uke ni jambo muhimu sana kwa afya ya wanawake. Mambo usiyostahili na unayostahili kufanya ili kutunza afya ya uke

Usiingize kidole ndani ya uke kwa lengo la kujisafisha hiyo huondoa asidi ya asili ya uke ambayo ni muhimu kwa sababu huzuia bakteria kukua. Aidha usitumie sabuni kuosha uke

Onana na daktari wa wanawake mara kwa mara kwa uchunguzi au unapojihisi tofauti. Hii husaidia kubaini ikiwa una saratani ya kizazi kabla haijaanza kukuathiri .

Fanya machaguo sahihi ya nguo zako za ndani. Wanawake wanapaswa kuvaa nguo za ndani za pamba. Pamba haishiki unyevu na huweka uke ukiwa baridi. Wakati wa hedhi, wanawake wanapaswa kubadilisha pedi mara kwa mara .

Kausha uke baada ya kutumia choo. Tumia kitambaa laini au tishu laini kukausha uke baada ya kutumia choo. Epuka kutumia tishu zenye harufu kali

Kutumia kinga wakati wa kujamiiana, kula lishe bora, kupunguza pombe na sigara pia ni muhimu kwa kulinda afya ya uke.
 
Kwema Wakuu!

Nimeona vijana wengi wakilalamikia mabinti kunuka Uke/nyuke Zao. Uke kunuka sio tuu ni aibu kwa Mwanamke bali inamshushia thamani na heshima yake.

Uke kunuka utakufanya ukose Mume.
Uke kunuka utakufanya usiwe comfortable ukikaa mbele za Watu au ukienda kusuka.
Au hata kwenye Daladala, unakuta binti mrembo na kajipamba vyema kabisa. Lakini mara unashangaa unasikia harufu fulani hivi yenye ukaribu na usaha au Kibudu(mnyama aliyeoza), inakuja na kupotea. Ni aibu.

Sasa warembo, sipo hapa kumlaumu yeyote. Najua tonatofautiana uelewa, akili, elimu na malezi.

Unapoambiwa uoshe Uchi/Uke wako haimaanishi uchukue masabuni usugue kama unasugua kikwapa. Nop.
Usitumie maji ya moto au yenye sabuni kuoshea Uke wako.
Wala usiingize kitu chochote ambacho sio kwa maelekezo ya wataalamu hasa wa mambo ya uzazi.

Uke wako utanuka usaha nakuhakikishia.

Kwenye Uke kuna wadudu maalum kwaajili ya kiungo hicho. Unapotumia madawa(sabuni) au maji ya moto au kemikali zozote kusafisha Uke wako unapelekea hao wadudu kupoteana, kuangamia, kufa na hiyo itafanya ujio wa wadudu ambao sio mahususi kwa eneo hilo kama Fangasi na jamii zingine za bacteria.

Usiingize vidole vyako Ukeni wakati wa kujisafisha. Osha eneo la nje la Uke na maji baridi. Kisha tumia kitambaa kikavu kilichokisafi kujikaushia. Hakikisha pawe pakavu. Kisha vaa chupi ambayo umeipiga Pasi vizuri. Na kama hauna pasi. Basi hakikisha unaitunza mahali safi na salama.

Usijioulizie marashi Ukeni.
Ukitoka kujisaidia haja ndogo hakikisha unajisafisha (maji ya baridi) vizuri na kujifuta ujikaushe vizuri.

Epuka kuvaa pedi muda mrefu. Wastani wa pedi angalau masaa matano mpaka nane. Hivyo kwa siku ni vizuri ubadilishe Pedi sio pungufu ya Tatu.

Kunywa maji Mengi ili kuufanya mwili uwe sawa. Kuepuka kunuka nuka hovyohovyo. Kunywa maji mengi hufanya mifumo wa mwili kuwa safi na kufanya kazi vizuri. Ikiwemo mifumo ya utoaji takamwili.
Wastani wa maji itategemea na umri na uzito. Lakini kikawaida usipungue lita mbili na nusu na isizidi tano.

Ni aibu kunuka Uchi. Na kutibu uchi unaonuka ni mchakato mrefu.

Hakuna kitu kitamkera mwanaume kama kukutana na Mwanamke mwenye uchi unaonuka. Ni vizuri kujisafisha kwa njia sahihi.

Huwezi ukajiamini kama Uke wako unanuka. Utaishi kwa stress, utaachwa kila mara, hakuna mwanaume atakuvumilia.

Mimi nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Ila watoto wa siku hizi! Nyapu tu! Mawazo yote ni mapajani mwa wanawake. Huyo Mungu wenu)kama kweli yupo) bado ana kazi si mchezo.
 
Ila watoto wa siku hizi! Nyapu tu! Mawazo yote ni mapajani mwa wanawake. Huyo Mungu wenu)kama kweli yupo) bado ana kazi si mchezo.
Hii imeenda kushoto au mm ndio nimezingua. Jamaa akongea mambo mazuri kwa afya ya ndugu zetu wa kike sasa ulicho reply sasa 😆😆😆
 
Hii imeenda kushoto au mm ndio nimezingua. Jamaa akongea mambo mazuri kwa afya ya ndugu zetu wa kike sasa ulicho reply sasa 😆😆😆
Sema tu wengine wanachukuliaga kama ubaya,lakini hapa utapana kila aina ya jibu. Ya ovyo lazima na yenyewe yaje,ya kuchekesha yapo,ya maana yapo.
Ila angewaomba wao waeleze kwa nini. Ingekaa poa. Tunakutanaga nao. Sema sasa ukute umekaa nae kashika bomba. Unatamani ushukie hapo hapo.

unakuta binti mrembo na kajipamba vyema kabisa. Lakini mara unashangaa unasikia harufu fulani hivi yenye ukaribu na usaha au Kibudu(mnyama aliyeoza), inakuja na kupotea. Ni aibu. Kwa hili kaua. Yeye hapa hapa,angewaachia wajitetee wenyewe.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom