Uchaguzi 2020 Fao la Kujitoa ni Turufu nyingine kwa Wagombea Urais

Uchaguzi 2020 Fao la Kujitoa ni Turufu nyingine kwa Wagombea Urais

Wabunge wote walaaniwe, ndo waliopitisha hii Sheria enzi za kikwete. Magufuli, Mbowe, Membe, Zitto, wote walihusika.
Mkuu Tafadhari waondoe wabunge waupinzani hapo, walikataa katakata, kwasababu ccm niwengi wakalipitisha.Na haikua enzi za Kikwete nienzi za Magufuli .
 
Baada ya sheria mpya kupitishwa iliyofuta FAO LA KUJITOA na kuja na mbadala wake wafanyakazi wengi hususani katika sekta binafsi walionja na wanaendelea kuonja joto la jiwe kutokana na kutoruhusiwa kuchukua MAFAO yao kwa mkupuo pale ajira zao zinapokoma ama kwa kumaliza mkataba au kwa kuachishwa kazi. Kile kilichohifadhiwa kama akiba ya mtu anapokwenda kukidai hakipati chote badala yake kuwa analipwa asilimia 33.3 kama sikosei ya mshahara wake wa awali.

Naamini kundi hili ni kubwa sana na kwa sababu sheria hii bado ipo na inaendelea kufanya kazi hata wale ambao bado ni watumishi wakati wa kumaliza mikataba yao au kuachishwa kazi utakapofika changamoto hiyo watakumbana nayo.

Hivyo kwa jinsi hali ilivyo akitokea mgombea urais yeyote akaishikia kibendera hoja hii ya FAO LA KUJITOA kwamba atalirudisha kama ilivyokuwa zamani atazoa kura nyingi sana na atapata kuungwa mkono na wananchi wengi.

Ewe mgombea urais kupitia chama chako wakati unatafuta kuungwa mkono na wananchi usisahau kutafuta kura zingine kwenye FAO LA KUJITOA na linadi kwa nguvu zote lipate kusikika masikioni na kunenwa vinywani mwa wananchi. Usidharau maana kura moja tu ina "impact" kubwa sana katika uchaguzi mkuu ujao.

CHAUMA, CUF, ACT- WAZALENDO, CCM na CHADEMA kazi kwenu. Sera zenu ziguse kila kundi fulani katika jamii. Kila mmoja ana hamu ya kusikia mgombea urais atakayekuja na majibu ya FAO LA KUJITOA

Niwatakie mpambano mwema katika kutafuta kuungwa mkono na wananchi katika harakati hizi za kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.
Kasome ilani ya chadema,


Pale kwenye siku 100 za mwanzo wanadai wataruhusu mpoteza ajira kupewa pesa zake mara 1 kutoka kwenye mifuko hiyo.
 
mkuu naona hii hoja imekugusa sana, kuongelea fao la kujitoa ni mawazo ya kienyeji sana,

Kwanza, kwanini mtu anadai fao lake? nikwa sababu kapoteza ajira "labor turnover" kinachopaswa kuangaliwa kwanini watu wapoteze ajira zao? Jambo la kwanza alilofanya mwalimu baada tu ya uhuru ni kufanya mtu kupoteza ajira kuwa jambo gumu. Na ndivyo inavyopaswa kuwa, kuwa mtu kupoteza ajira yake liwe jambo gumu sana.

Hawa wagombea wetu hakuna anayezungumzia job security, maelfu ya watu wamefutwa kazi kwa sababu mbalimbali, serikali ilipaswa iwajibike na hayo mambo ya hovyo kabisa. Lakini si Lissu wala jpm anaongelea hilo, tunatengeneza ajira na kupoteza ajira wakati huohuo work done equal to zero.
Kuna mtu anafanya kazi kwa mkataba labda miaka 5

Shughuli zinaisha kabisaa

Wakati huo una miaka 30 sasa usubiri mpaka ufikishe 60 wakati huo pesa ni kama m10 tu

Kwq nini usipewe pesa yqko ukafungua hata genge ukasongesha maisha?
 
Kuna mtu anafanya kazi kwa mkataba labda miaka 5

Shughuli zinaisha kabisaa

Wakati huo una miaka 30 sasa usubiri mpaka ufikishe 60 wakati huo pesa ni kama m10 tu

Kwq nini usipewe pesa yqko ukafungua hata genge ukasongesha maisha?
Kiukweli hii Serikali nikitafakari hilo, naona niwezi sana, kwa nini wabunge nao wasingekua wanasubir miaka 60 ndio wapewe mafao yao,lakini wao wakimaliza tu miaka miatano wanapewa fedha zao, lkn ww mlala hoi umeingia mkataba wamiaka mitano imeisha au umeachishwa kazi ,eti usubir mafao mpaka sijui ufikishe miaka 53.
 
Mkuu Tafadhari waondoe wabunge waupinzani hapo, walikataa katakata, kwasababu ccm niwengi wakalipitisha.Na haikua enzi za Kikwete nienzi za Magufuli .
Kuna Mbunge alibatizwa kwa jina la Kikokotoo kama sikosei na alikuwa wanatoka upinzani...heshima kwao
 
Kuna Mbunge alibatizwa kwa jina la Kikokotoo kama sikosei na alikuwa wanatoka upinzani...heshima kwao
Hicho kikokotoo wanakileta 2023. Ngoja Magufuli apite hakika maisha yatakua magum mara 4 yasasa, hasa kwa watu wanaofanya kazi za mikataba private sector.
 
Hii ni moja ya hoja ambayo LISSU anatakiwa kuitangaza mara kwa mara na kuiwekea mkazo wa dhati,hii sheria inamfanya mfanyakazi wa serikali/wa sekta binafsi kuwa mtumwa kwa kuhofia kuwa endapo atapoteza kibarua atakuwa hana cha kufanya endapo atakuwa nje ya ajira ukizingatia pesa hana za kujiajiri.

Wabunge mnapopitisha sheria kama hizi angalieni mazingira ya kazi kwa wafanyakazi..watu hufanya kazi katika mazingira magumu yaliyojaa manyanyaso na ukandamizaji,mwishowe mtu anapoamua kuacha/kuachishwa kazi anakuja kukumbana na ugumu wa maisha kutokana na ukata wa pesa...hali hii upelekea watu kuishi na msongo wa mawazo.

Rai yangu, hii sheria ifutwe maana ina mkandamiza mfanyakazi na kumfanya awe mtumwa...sijaona haja ya kutunga sheria kandamizi kwa wafanyakazi ukizingatia tupo kwenye karne ya 21 hatupo dark age jamani,wakati mnapokuwa bungeni jaribuni kuwa na huruma,lakini hata huyo mtetezi wa wanyonge alikuwa hajui kuwa sheria hii ni kandamizi juu ya kupigiwa kelele kutoka kwa wapinzani mpaka anaisaini.
 
Baada ya sheria mpya kupitishwa iliyofuta FAO LA KUJITOA na kuja na mbadala wake wafanyakazi wengi hususani katika sekta binafsi walionja na wanaendelea kuonja joto la jiwe kutokana na kutoruhusiwa kuchukua MAFAO yao kwa mkupuo pale ajira zao zinapokoma ama kwa kumaliza mkataba au kwa kuachishwa kazi. Kile kilichohifadhiwa kama akiba ya mtu anapokwenda kukidai hakipati chote badala yake kuwa analipwa asilimia 33.3 kama sikosei ya mshahara wake wa awali.

Naamini kundi hili ni kubwa sana na kwa sababu sheria hii bado ipo na inaendelea kufanya kazi hata wale ambao bado ni watumishi wakati wa kumaliza mikataba yao au kuachishwa kazi utakapofika changamoto hiyo watakumbana nayo.

Hivyo kwa jinsi hali ilivyo akitokea mgombea urais yeyote akaishikia kibendera hoja hii ya FAO LA KUJITOA kwamba atalirudisha kama ilivyokuwa zamani atazoa kura nyingi sana na atapata kuungwa mkono na wananchi wengi.

Ewe mgombea urais kupitia chama chako wakati unatafuta kuungwa mkono na wananchi usisahau kutafuta kura zingine kwenye FAO LA KUJITOA na linadi kwa nguvu zote lipate kusikika masikioni na kunenwa vinywani mwa wananchi. Usidharau maana kura moja tu ina "impact" kubwa sana katika uchaguzi mkuu ujao.

CHAUMA, CUF, ACT- WAZALENDO, CCM na CHADEMA kazi kwenu. Sera zenu ziguse kila kundi fulani katika jamii. Kila mmoja ana hamu ya kusikia mgombea urais atakayekuja na majibu ya FAO LA KUJITOA

Niwatakie mpambano mwema katika kutafuta kuungwa mkono na wananchi katika harakati hizi za kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.
Wananchi wa hili taifa baadhi walivyo mambumbumbu , mtu akiwa anapigania maslahi yao wao ndiwo wanamuona mbaya, sijui nini huwa kinawekwa kwenye akili zao.

Anayewakandamiza kama Joniijo ndiwo wanamuona kama mkombozi wao
 
Esther Bulaya alitetea mno sana sana
Ester alilipigania hili ila alikatishwa tamaa na wenzie, yule mangi aliyatoa ma zombie yake bungeni hoja ikapita kiulaini alipaswa awaache watie vurugu hadi hoja ife
 
Ndiyo, katika hali hiyo ya job insecurity, CCM wakaona haitoshi wakashusha rungu kwa kuondoa fao la kujitoa. Yahani hawataki uchukiwe hata kale kadogo uliko accumulate ukiwa kazini. Mtoa mada kawataja ccm wakati kwenye hili ndo wenye kutengeneza tatizo,obvosly siamiamini kama ccm wanaweza kuwa sehemu ya utatuzi wake kwani ndo wanufaika wakuu wa hilo tatizo (ndo walolitengeneza).
chakushangaza hata wapinzani wakauchuna, Ester alibaki pekeyake naye akaishiwa nguvu, ukweli hakuna mwenye uchungu na watumishi wa nchi hii, na kama hawatajisimamia wenyewe mtetezi hakuna.
 
Mkuu Tafadhari waondoe wabunge waupinzani hapo, walikataa katakata, kwasababu ccm niwengi wakalipitisha.Na haikua enzi za Kikwete nienzi za Magufuli .
Umesahau wewe, ni enzi za kikwete,labda Kama wewe bado uko shule. Sheria ilipitishwa wakati ule hata Mimi Kuna wakati nadai mafao wakati ule tuliambiwa tusubiri maelekezo toka makao makuu. Wafanyakazi wa migodini walianza kuacha kazi kabla ya Sheria haijakaziwa ndo ikaahirishwa ila haikufutwa na tukapewa mafao yetu.
 
Kasome ilani ya chadema,


Pale kwenye siku 100 za mwanzo wanadai wataruhusu mpoteza ajira kupewa pesa zake mara 1 kutoka kwenye mifuko hiyo.
Tatizo la chadema ni kwamba hawatashinda urais. Kwa hiyo utekelezaji wa hii Sheria haiwezekani. Labda tumbane huyu Magufuli vinginevyo mafao HAKUNA atakaye pata.
 
Umesahau wewe, ni enzi za kikwete,labda Kama wewe bado uko shule. Sheria ilipitishwa wakati ule hata Mimi Kuna wakati nadai mafao wakati ule tuliambiwa tusubiri maelekezo toka makao makuu. Wafanyakazi wa migodini walianza kuacha kazi kabla ya Sheria haijakaziwa ndo ikaahirishwa ila haikufutwa na tukapewa mafao yetu.
Acha kudanganya uma, kipindi Cha kikwete lilikuja likaahirishwa, hio sheria umeanza 2018. Kama huamini nenda hata kwenye website za taasisi husika uangalie. Au gugo ujiridhishe sheria imeanza kutumika lini.
 
Kuna mtu anafanya kazi kwa mkataba labda miaka 5

Shughuli zinaisha kabisaa

Wakati huo una miaka 30 sasa usubiri mpaka ufikishe 60 wakati huo pesa ni kama m10 tu

Kwq nini usipewe pesa yqko ukafungua hata genge ukasongesha maisha?
Hii Sheria ni kandamizi Sana labda wanufaika waamue kuandamana vinginevyo serikali haitawalipa maana hela serikali walizifisadi zote.
 
Baada ya sheria mpya kupitishwa iliyofuta FAO LA KUJITOA na kuja na mbadala wake wafanyakazi wengi hususani katika sekta binafsi walionja na wanaendelea kuonja joto la jiwe kutokana na kutoruhusiwa kuchukua MAFAO yao kwa mkupuo pale ajira zao zinapokoma ama kwa kumaliza mkataba au kwa kuachishwa kazi. Kile kilichohifadhiwa kama akiba ya mtu anapokwenda kukidai hakipati chote badala yake kuwa analipwa asilimia 33.3 kama sikosei ya mshahara wake wa awali.

Naamini kundi hili ni kubwa sana na kwa sababu sheria hii bado ipo na inaendelea kufanya kazi hata wale ambao bado ni watumishi wakati wa kumaliza mikataba yao au kuachishwa kazi utakapofika changamoto hiyo watakumbana nayo.

Hivyo kwa jinsi hali ilivyo akitokea mgombea urais yeyote akaishikia kibendera hoja hii ya FAO LA KUJITOA kwamba atalirudisha kama ilivyokuwa zamani atazoa kura nyingi sana na atapata kuungwa mkono na wananchi wengi.

Ewe mgombea urais kupitia chama chako wakati unatafuta kuungwa mkono na wananchi usisahau kutafuta kura zingine kwenye FAO LA KUJITOA na linadi kwa nguvu zote lipate kusikika masikioni na kunenwa vinywani mwa wananchi. Usidharau maana kura moja tu ina "impact" kubwa sana katika uchaguzi mkuu ujao.

CHAUMA, CUF, ACT- WAZALENDO, CCM na CHADEMA kazi kwenu. Sera zenu ziguse kila kundi fulani katika jamii. Kila mmoja ana hamu ya kusikia mgombea urais atakayekuja na majibu ya FAO LA KUJITOA

Niwatakie mpambano mwema katika kutafuta kuungwa mkono na wananchi katika harakati hizi za kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.
Kauli ni moja na nia ni moja sasaaaa basi lisu atosha hayo mengine mbwembwe tu
 
Ester alilipigania hili ila alikatishwa tamaa na wenzie, yule mangi aliyatoa ma zombie yake bungeni hoja ikapita kiulaini alipaswa awaache watie vurugu hadi hoja ife
Mbowe mnafiki Sana aliona wabunge wake wanaibana serikali akavuta mshiko akawatoa ili mswada upite. Biashara za Chadema za hovyo Sana.
 
Mbowe mnafiki Sana aliona wabunge wake wanaibana serikali akavuta mshiko akawatoa ili mswada upite. Biashara za Chadema za hovyo Sana.
Hivi CHADEMA wanaweza zuia mswada usiende kuwa sheria, yaan bunge lenye wabunge zaidi ya 314 wazuiliwe na CHADEMA yenye wabunge 70 bunge lililopita??
 
Back
Top Bottom