Farmaajo, Rais wa Somalia ambaye aliichukia Kenya sana, abanduliwa katika uchaguzi wa Urais

Farmaajo, Rais wa Somalia ambaye aliichukia Kenya sana, abanduliwa katika uchaguzi wa Urais

Tony254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2017
Posts
16,017
Reaction score
16,431
Huyu mtu mwenye roho mbaya, kisirani number moja kwa jina la Farmaajo, rais wa Somalia amebanduliwa katika uchaguzi uliofanyika jana.

Amefanyia Kenya madhambi mengi sana. Yeye ndio aliban Kenya kuexport miraa to Somalia. Yeye ndio alikataa kuondoa kesi mahakamani na kukataa kunegotiate na Kenya kwenye kesi ya ICJ. Alidhani ataongoza milele.

 
Now come to the point What next.
Kumbuka Kila mtu anaongoza kwa utashi wake
Kila mtu anaangalia Faida na madhara ya kitu
Si ulete hiyo miraa Tanzania basi ama?
Tusilaumu kila kitu
Kenya mnahalalisha dhambi ...Sasa mwingine akikataa kushiriki dhambi yako anakuwa mbaya?
 
Hahahaha, Kenya mpo na matatizo mengi Sana, kwahiyo mkikwaruzana na majirani wenu, "automatically" wao ndio wenye kuichukia Kenya na sio konyume chake?

Kwahiyo baada ya uchaguzi wa Kenya Uhuru Kenyatta akimaliza muda Wake, wasomali nao wasndike kwamba "rais wa Kenya aliyekua akiichukia Somalia hayupo tena madarakani?",

Wewe unahisi rais mpya wa Somalia hatodai tena eneo la Somalia walilokabidhiwa na ICJ?. By the way, ni jirani gani wa Kenya ambaye haichukii Kenya?[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Rais aliyeingia ni rafiki wa Kenya na hii ni mara yake ya pili kuwa rais wa Somalia. Yeye ndio alikuwa rais kabla ya Farmaajo. Wakati alikuwa rais uhusiano kati ya Kenya na Somalia ulikuwa mzuri.
 
Hahahaha, Kenya mpo na matatizo mengi Sana, kwahiyo mkikwaruzana na majirani wenu, "automatically" wao ndio wenye kuichukia Kenya na sio konyume chake
Eneo gani hilo ambalo ICJ wamewakabidhi Somalia?
 
Sio kwamba aliichukia Kenya, maanake Kenya ndio ilifanikisha azimio lake na mipango yote hadi akawa rais. Hapo awali, enzi za rais Mwai Kibaki, Farmajoo alikuwa anaishi Kenya na kutawala nchi yake kutoka jijini Nairobi.

Bifu zake na Kenya zilianza alipostukia mipango ya Kenya kule Jubaland. Eneo ambalo limepakana na Kenya na ambalo linataka kujitenga rasmi na nchi ya Somalia. Rais Uhuru alilazimisha kuwe na uchaguzi Jubaland, kabla ya muda. Kisa Kenya ilitaka Rais Sheikh Ahmed Madoobe aendelee kuitawala Jubaland. Uchaguzi ulifanywa Kismayu, licha ya pingamizi za Farmajoo na serikali kuu ya Mogadishu.

Sheikh Madobe akashinda kwa kishindo, jambo ambalo Farmajoo hakulitarajia. Ikawa wazi kwamba Nairobi ina ushawishi mkubwa Kismayo, zaidi ya serikali kuu kule Mogadishu. Rais Sheikh Madobe akisaidiwa na Kenya, kihali na kimali, amekuwa tishio kubwa sana kwa Mogadishu. Kikosi chake cha Ras Kamboni Brigade kimeimarika sana. Baada ya kufanyiwa mafunzo na kufanya kazi na KDF kwa muda mrefu, wakipagana kwa pamoja dhidi ya magaidi wa alshabaab.

Zaidi ya hayo, silaha na vifaa vya kivita vinafika Kismayu, Jubaland moja moja kwa moja kutoka Nairobi, chini ya ufadhili wa serikali ya Kenya. Baada ya rais Uhuru kuwakubalia wapinzani wote wa Farmajoo kufanya vikao vyao vya kampeni kutoka Nairobi. Jamaa akaanza kupanick na kujaribu kuleta chuki kati ya Kenya na Somalia, ili apate kura za huruma. Ila hamna namna sasa, itabidi afunganye virago vyake roho safi na arudi kwao US.
 
Sio kwamba aliichukia Kenya, maanake Kenya ndio ilifanikisha azimio lake na mipango yote hadi akawa rais. Hapo awali, enzi za rais Mwai Kibaki, Farmajoo alikuwa anaishi Kenya na kutawala nchi yake kutoka jijini Nairobi...
Umeelezea vizuri.
 
Back
Top Bottom