Fatma Karume aondolewa kwenye orodha ya mawakili (Permanent removal), akutwa na hatia ya kukiuka maadili

Fatma Karume aondolewa kwenye orodha ya mawakili (Permanent removal), akutwa na hatia ya kukiuka maadili

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
1600858044277.png
Kikao cha kamati ya maadili ya Mawakili kilichokaa leo tarehe 23/9/2020 kimemkuta na hatia ya kukiuka maadili kwa kiwango cha juu, wakili Fatma Karume mwenye roll namba 848 na hivyo kuamuru jina lake liondolewe (permanent removal) katika orodha ya mawakili Tanganyika.

Septemba mwaka 2019, wakili Karume alisimamishwa kufanya kazi ya uwakili Tanzania Bara, maamuzi yaliyotolewa na Jaji Feleshi kwenye kesi iliyofunguliwa na Ado Shaibu akipinga uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali kuteuliwa kimakosa na Rais Magufuli na kesi iliondolewa.

Mahakama kuu iliamuru Fatma apelekwe kamati ya maadili ya mawakili kwa kosa la kushambulia ofisi ya mwanasheria mkuu ambae ndiye alikuwa wakili wa Ado Shaibu katika kesi hiyo.

Pia, soma=> Fatma Karume asimamishwa kufanya kazi za Uwakili

===
Akijibu hoja ya mdau kwenye mtandao wa twitter aliyemuomba akate rufaa dhidi ya uamuzi huo, Fatma amesema hatafanya hivyo kwa maelezo kwamba muamuzi wa rufaa yake sio huru.

"Ukiingia kwenye mapambano unahitaji kujua nani unapambana nae, kanuni za mpambano na uhuru wa muamuzi. Iwapo kanuni haziko wazi na muamuzi hayuko huru, huo sio mpambano bali upotevu wa muda. Hifadhi nguvu zako kwa mpambano unaoweza kushinda". Yalinukuliwa majibu ya Fatma Karume.

Pia, soma=> TLS: Kamati ya Maadili Haijahusika Kumuondoa Fatma Karume kwenye orodha ya Mawakili
 
Makosa yake ni yepi? Huyu mama mwaka huu analo, kule Imma advocates wamemtimua na huku nako pia
 
KIKAO CHA KAMATI YA MAADILI YA MAWAKILI KILICHOKAA LEO TAREHE 23/9/2020. KIMEMKUTA NA HATIA YA KUKIUKA MAADILI KWA KIWANGO CHA JUU, WAKILI @fatma_karume (ROLL 848) NA HIVYO KUAMURU JINA LAKE LIONDOLEWA (PARMANENT. REMOVAL) KATIKA ORODHA YA MAWAKILI TANGANYIKA



1600857218264.png

1600857205429.png
 
Yule mama ni msomi mzuri,ni mtanzania Sasa mnataka awe mkimbizi ndani ya nchi yake? CCM jitafakarini ,mtakuwa KANU October 28.
Kila anae ongea ukweli CCM lazima wamfanyie figisu ili aharibikiwe. Huyu mama kosa lake lilikua ni kutetea na kuongea maovu yanayofanywa na serikali.

Lissu asiposhinda uchaguzi huu, basi na yeye atafanyiwa figisu ili aondolewe kwenye Advocate Roll. Ila Tundu Lissu akiwa Rais basi Fatma Karume atakuwa Waziri Wa Sheria au Mwanasheria Mkuu Wa Serikali (Hapa ndio mahakama na wanasheria wanaotumikia na kuwaabudu CCM watakapo juta).
 
duh! season one or two?
nafikiri wangeweka wazi kila kitu sababu za kumuengua inapendeza zaidi nchi ya uchumi wa kati kuweka data mezani wenye akili wachambue if what was done is logical or emotional! umaskini ni janga!
Sababu ni kwamba alikosoa uteuzi usiofata sheria wa kuteuliwa mwanasheria wa serikali kinyume na sheria
 
Hivi hawafaham kwamba huyu ni Mtoto wa Rais.!!
 
Back
Top Bottom