Fatma Karume atamani Watanzania Wangekuwa na Ufahamu kama Gen Z wa Kenya

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mjukuu wa baba wa taifa la Zanzibar Fatma Karume anesema anatamani Watanzania Wote wangekuwa na ufahamu kama Watoto Wadogo wa Gen Z

Karume amefurahishwa na Kauli ya Gen Z Kwa Ruto kwamba " Sisi ndio tumekuweka hapo na Sisi Tunaweza kukuondoa"

Karume ameongea ukurasani X

Baadae Mlale Unono πŸ˜ƒ
 
Tanzania hatuhitaji ufahamu wa Gen-Z badala, yake jamii zetu zinatakiwa ziamushe ubongo kubuni mbinu za kukabiliana na tabia ya unyumbu ambayo wanayo viongozi tuliowapa dhamana, unyumbu ni tabia ya waliopewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama uoga kwa viongozi wao na kutumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi
 
Biblia inasema, Kila Jambo chini ya Mbingu, lina-, "WAKATI WAKE"
 
Haitatokea kwa Tanzania hiyo kitu, asijisumbue kuwaza
 
Gen Z wapo duniani kote, ila wakwetu wamerithi utamaduni wetu ambao unahitaji marekebisho chanya (kuondoa nira za utumwa wa fikra na utii wa kikondoo, uliozaa uchawa).

Tujitahidi kabla gen alpha hawajaja kufanya yanayotokea Kenya.

Hii ni assignment ya TISS (kama kansa ya uchawa haijaingia ndani ya taasisi).
 
Gen Z wapo duniani kote, ila wakwetu wamerithi utamaduni wetu ambao unahitaji marekebisho chanya (kuondoa nira za utumwa wa fikra na utii wa kikondoo, uliozaa uchawa)...
Uchawa ni tabia ya unyumbu ambayo a.k.a chawa ana ahirisha kufikiri Kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza na kulituumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi, (human herding is an occurrence of entrusted people suspending their individual reasoning because of flattering or working towards group objectives and fear of their leaders), neno rahisi ni unafiki
 
Watanzania sio wapumbavu kama yeye,mda huu angetangulia au yeye sio Mtanzania?

Kwamba haya mambo ndio Haki zenu mnazohitaji au? πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ‘‡πŸ‘‡

View: https://www.instagram.com/reel/C8uifH2K-Qn/?igsh=cWo4a25xdXh3NTk4
 
Hii ni hatari kwa mustakabali wa taifa.
Ukiwa baba, mama, kaka, dada au kiongozi mwenye mamlaka yoyote, fikiria maisha ya baadaye ya taifa lililojengwa kwenye fikra za uchawa na unyumbu. Siyo Uzalendo kupalilia uchawa na unyumbu.
Tunaweza kabisa kutumia akili, hekima na busara kutafuta na kupata uongozi huku tukijenga jamii na taifa bora badala ya kulijeruhi kwa uchawa na unyumbu.
 
Haitakuwa rahisi kwa sababu wabongo wamejikita sana kwenye imani za kidini.
 
Ili
Yasiyoyatarajiwa, (uncertainty) husababishwa na majanga ama binadamu, binadamu ana sababisha yasiyoyatarajiwa Kwa wengine Kwakutokujua ama kwa makusudi kwa tabia ya unyumbu na uchawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…