Fatma Karume: Yaani leo nimethibitisha Adelardus (AG) hajui Katiba, anadai Serikali ina mihimili mitatu na yeye ndie anasimamia yote

Fatma Karume: Yaani leo nimethibitisha Adelardus (AG) hajui Katiba, anadai Serikali ina mihimili mitatu na yeye ndie anasimamia yote

Bado


Kwa sasa kutokana na sheria ya juzi pia na mwanya wa kikatiba yeye ni mshauri wa mihimili yote

AG ni mshauri wa serikali
AG ni mbunge na mshauri wa bunge kwenye masuala ya utungaji na kufuata sheria husika bungeni

AG ni mshauri wa mahakama kutokana na tume ya utumishi wa Umma ambaye yeye ni mjumbe

Ni mshauri wa mihimili mitatu katika mashauri ya wakuu wa vyombo hivyo


Fatuma anasema moja katika 3 yaani nguvu hizo haziko sawa kwa kuwa 1 ndiye anazaa tatu as if hakuna watu! Rais licha ya kuwa kiongozi wa nchi hapaswi kuingilia mifumo mingine kiutendaji isipokuwa kwenye checks and balance

Msingi wa mhimili na watu hivyo ndiyo maana uchaguliwa kwa kuwa mahakama ni ya kudumu na uhitaji wa watendaji inaundwa na principle za utendaji na si mawazo ya watu isipokuwa mkuu ambaye anachaguliwa na rais aliyechaguliwa na watu kisha anapaswa kuidhinishwa na bunge ambao ndiyo watu kwa mifumo ya marekani na kenya lkn ilipaswa CJ achaguliwe na bunge ambao ni wawakilishi wa watu tena kwa kura ya siri baada ya kuomba nafasi hiyo kwa utaratibu uliowekwa au watendaji wote wa mahakama ndiyo wapige kura kumchagua kiongozi wao mkuu kama lilivyo bunge hata kama si mwajiriwa isipokuwa awe na cheti cha sheria au leseni ya uanasheria

Tunaendelea
Ramark

Ukisoma Kanuni za Bunge, utakuta mtu anaitwa Chief Parliamentary Legal Counsel, huyu ndo mshauri wa bunge kwenye maswala ya kisheria na sio Attorney General.

Kuhusu Tume ya Utumishi wa mahakama, ile sio chombo cha ushauri but ni disciplinary body ya mahakama.
 
Government?

The group of people with the authority to govern a country or state; a particular ministry in office.

Na ukisikia nchi mmepinduliwa, kinachopinduliwa ni government , ni watu walio shika madaraka tu, na pale tu tunapo sema serikali inavunja sheria au inawaonea wananchi au wanasiasa, maana yake ni viongozi wenye mamlaka.

Wengi wanavyo fahamu police ni government, au bunge au mahakama, hivi ni vitu tofauti, lazima tuelewane bwana. Nyie wanasheria muwaelimishe watanzania
Ni shida watu wengi humu wanachanganya on what is an ‘executive government’.

Executive maana yake ni raisi, baraza la mawaziri, makatibu wakuu na viongozi wa idara za serikali. In short executive government ni senior decision makers only ambao maamuzi yao yanawagusa wengi.

Local government is not part of the executive kama ilivyo mahakama na bunge.
 
Powa sana.... umenielimisha anyway
Nadhani bado itategemea uwakilishi huo ni kwa ajili ya nini. Nadhani kwa vile mwakilishi wa dola nje ya nchi ni serikali (k.m. mahakama na Bunge hawana uwakilishi nje tofauti na balozi zetu ambazo ni sehemu ya serikali) basi AG atapewa jukumu la kuwakilisha mihimili mingine ingawa nitategemea kuwa washauri wao wa ndani watahusika sana. Kwa mfano, kampuni ya kigeni ikimshitaki katibu wa Bunge au Mtendaji Mkuu wa Mahakama kwa kukiuka mkataba, AG ndie atakaewatetea. Ila usiniamini sana kwa vile mimi sio mwanasheria, mimi ni technician tu.

Amandla....
 
Hivi unataka kuniambia legislature maanake bunge!? Na parliament nini? au walikosea kusema legislature badala yake wangeandika parliament?
Watanzania tujifunze hiko ni kiingereza
😅😅😅😅😆😆😆😆
 
Aibu kubwa sana kwa wanachama wa Chadema kuwa mbumbumbu huki wakijifanya wanataka chama chao kikamate dola,wakati hawajui dola ni nini na serikali nini.
Dola inajumuisha mipaka,watu,uhuru wa kujitawala n.k
Serikali ni watu wachache waliochaguliwa ambao ni wawakilishi,hawa ndio huwa wanaunda serikali na serikali huwa na branches tatu(mihimili).
Ndio maan Rais anamteua CJ majaji n.k,Spik nae anatoka kwenye chama kinachounda serikali
Aibu kwa Cdm Bishweko
Mkuu Soma post zako za nyuma Kisha linganisha na hii,I hope akili zinaanza kukurudia ndo maana unaanza kuingiza siasa zako uchwara kwenye huu uzi
 
Acha uhuni ,umeandika wewe kule juu....alafu kumbuka Spika anatokana na chama ambacho Rais ndiye mwenyekiti ata kama apigiwi kura za kua Mwenyekiti.
Usikute wewe ni mkuu wa wilaya eti
 
Mkuu acha ukilaza,state ndiyo dola kwa lungha nyingine na ndo nchi au jamhuri.State/dola/nchi/jamhuri ya Tanzania ndo yenye mihimili mitatu kwa mujibu wa katiba ya nchi hii ya mwaka 1977 ambayo ni serikali,mahakama na Bunge.Kama hadi hapa hujaelewa naomba umtafute Oni sigara akufundishe kiswahili
Ndio Mzumbe mlifundishwa hivyo?
 
Mkuu Soma post zako za nyuma Kisha linganisha na hii,I hope akili zinaanza kukurudia ndo maana unaanza kuingiza siasa zako uchwara kwenye huu uzi
State vs government. Hicho ndio hujui ndio maana bado ni mbumbumbu.
Kuna kitu kinaitwa State's government hiki ndio huwa kina mihimili mitatu. Nafikiri ulipoteza muda wako bure pale Mzumbe.
 
Kasome doctrine of separtion of powers uondoe ujinga. Usidhani kupost Jf ndio kujua mambo. Unaweza ukawa unapost ila unafikiri kwa kutumia makalio kama wenzako.
Sisiemu mmejaa wajinga na ndio mtaji wa watu kama nyinyi msiojua A wala B ,Yaani kabisa unasema serikali ina mihimili mitatu? UTOPOLO MTUPU NYIE.
 
Serikali ni mhimili mmoja kati ya 3,ana maanisha nini?
Serikali ina mihimili 3,Executive judiciary and Legislature, kosa liko wapi? Maana ni serikali moja iliyojigawa katika mihimili mitatu.
Chadema imejaa wavuta bangi na wanywa konyagi. Upuuzi kama huu sio wa kushabikia.
Nadhani unatakiwa kutofautisha kati ya dola na serikali ndio urudi kwenye mjadala
 
K
Kwahiyo Serikali ni moja ya Tawi la Serikali au Serikali ni moja ya mihimili? Unajua tofauti ya Dola na Serikali? Unajua kwamba Serikali inachange kila baada ya Uchaguzi?
Kwani bunge halibadiliki baada ya uchaguzi? Kwani jaji mkuu hawezi kubadilishwa baada ya uchaguzi? Au jaji mkuu hawezi kubadilishwa na Rais?
 
Aibu kubwa sana kwa wanachama wa Chadema kuwa mbumbumbu huki wakijifanya wanataka chama chao kikamate dola,wakati hawajui dola ni nini na serikali nini.
Dola inajumuisha mipaka,watu,uhuru wa kujitawala n.k
Serikali ni watu wachache waliochaguliwa ambao ni wawakilishi,hawa ndio huwa wanaunda serikali na serikali huwa na branches tatu(mihimili).
Ndio maan Rais anamteua CJ majaji n.k,Spik nae anatoka kwenye chama kinachounda serikali
Aibu kwa Cdm Bishweko
Unawaita watu mbumbumbu wakati maelezo yako yanaonesha moja kwa moja hujui hata unachoongea!!

Eti Spika anatoka chama kinachounda serikali!! Kwa mujibu wa katiba ipi, na ya mwaka upi?! Kila anayeijua katiba yetu pia anafahamu Spika anaweza kuwa mtu yeyote hata asiye mwanachama wa chama cha siasa!

Na unaposema dola inajumuisha mipaka, watu, uhuru wa kujitawala n.k, na kisha unasema serikali ni watu wachache, hapo unasahau hao watu wachache is just a subset ya watu ambao ni sehemu ya dola!

Kwa maana nyingine, serikali nayo ni subset ya dola na sio dola!
 
Back
Top Bottom