Fatma Karume: Yaani leo nimethibitisha Adelardus (AG) hajui Katiba, anadai Serikali ina mihimili mitatu na yeye ndie anasimamia yote

Fatma Karume: Yaani leo nimethibitisha Adelardus (AG) hajui Katiba, anadai Serikali ina mihimili mitatu na yeye ndie anasimamia yote

K
Kwani bunge halibadiliki baada ya uchaguzi? Kwani jaji mkuu hawezi kubadilishwa baada ya uchaguzi? Au jaji mkuu hawezi kubadilishwa na Rais?
Jaji Mkuu kama Majaji wengine hawezi kubadilishwa na Rais kirahisi. Ndio maana huwezi kusikia rais anamtumbua Jaji. Ili Jaji aondolewe, linatakiwa kukaa jopo la Majaji wenzake kutoka nchi za jumuia ya Madola na hao wakiridhia ndio anaondoka. Tenure yao inalindwa kikatiba kamailivyoya CAG. Hii ni kulinda uhuru wao wa kuhakikisha haki inatendeka bila kuogopa Mamlaka iliyomteua.

Tofauti na Mahakama, Bunge na Serikali zinapaswa kupata ridhaa ya wananchi kila baada ya miaka mitano kupitia uchaguzi. Kwa sababu hiyo Serikali na Bunge zinaweza kubadilika kila baada ya uchaguzi. Aidha, ingawa Mkuu wa Serikali ana mamlaka kamili ya kubadilisha mawaziri wanaounda serikali yake lakini analazimishwa kuwachagua kutoka ndani ya Bunge.

Amandla...
 
Endeleeni ku support Ujinga huko ndani ya Chama Chenu!!
Sasa kama unajua kabisa nchi inakuwa na eneo,watu,na mamlaka ya nchi n.k
Sasa unashindwa kutofautisha vipi mamlaka ya nchi na nchi?
Mamlaka ya nchi yanakuwa na organs tatu,kama una akili timamu unashindwa vipi kujua?
 
Sasa kama unajua kabisa nchi inakuwa na eneo,watu,na mamlaka ya nchi n.k
Sasa unashindwa kutofautisha vipi mamlaka ya nchi na nchi?
Mamlaka ya nchi yanakuwa na organs tatu,kama una akili timamu unashindwa vipi kujua?
Kasome Civics tena maana haujui kutofautisha Country,State,Nation ,Sovereignty and Government ukielewa hayo hauwezi kuendelea na UTOPOLO.
 
Huyu mama mkorofi na muongeaji aisee Jana nimekutana naye jengo la Alfa house mkabala na jengo la makao makuu ya vodacom.hapana huyu mama mtata sana.mpaka nikawauliza wenzangu huyu mama kaolewa maana anaongea kama Kasuku aisee
nikiri tu kuwa Shangazi ni Genius na ukiwa na akili chini yake huwezi kumuelewa! watu wenye akili nyingi hupambana kuongea wawafikishe wasioelewa katika uelewa na huwa hawafanikiwi sababu wale wanaowapigania hawana uwezo wa kuelewa!!

wakati Chadema wakivunjwa miguu na mikono na mabuti na virungu na mabomu na maji ya kuwasha wanasambazwa barabarani kwa miaka yote hii Shangazi akawaambia mtakufa bure solution ni kubadili vipengele vibovu vya sheria ya uchaguzi sio barabarani! yaani tume iwe huru wakurugenzi wa kijani ambao ni magwiji wa mabao ya mkono waondolewe na mengine kibao!! hakika Fatma ana akili nyingi tukubali kushindwa tu! mimi nimesoma ulaya najua tofauti ya elimu yetu na ya nje! bongo ni thinking inside the box one question one answer , developed world one question many answers and opinions defend your answers, expand the boundary of what you know or what is known and think outside the box!

yaani kila mtu kwa akili za bongo zenye athari ya elimu ya kikoloni ataona AG ni gwiji wa sheria kuliko sote , kwa akili za kizungu AG ni cheo na kuna watu wamemzidi akili ya sheria hawana hicho cheo! ujinga ni mzigo!
 
Back
Top Bottom