Fatma Nyoro muimbaji mwenye sauti tamu kama Malaika

Fatma Nyoro muimbaji mwenye sauti tamu kama Malaika

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Ukizungumzia waimba taarabu wa kike wenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni basi Fatma Mahmoud Nyoro maarufu kama Fatma Mcharuko ni namba one.

Waimba taarabu wengi wanapata shida kugandamizia/ kuimba nyimbo alizoimba Fatma kutokana na upekee wa sauti yake.

Wasanii wa jahazi modern taarabu walikuwa wanapata tabu sana kuimba nyimbo za Fatma kipindi kile Fatma mjamzito ,walikuwa wanaziharibu haswa tofauti na nyimbo za wengine hata wasipokuwepo lazima mbadala atakuwepo kuweza kuziba pengo hilo.

Bendi nyingi sana za taarabu zinatamani sana kuwa na Fatma katika bendi yao kutokana na upekee wa sauti.

Fatma alishawahi kutamba na vibao kama vile Mfamaji, Maruperupe,Aso kasoro, kwa sasa anasumbua na ngoma ya Siwaguni wala siwakohoi.

Fatma kwa sasa anaitumikia bendi ya Yah TMK na ndiye msanii aliyefanikiwa kuwajazia mashabiki bendi hiyo kutokana na umahiri wa uimbaji wake.
images.jpeg
 
Nachekaga na ule mstari wa "naringia shape yangu Nina mvuto nyuma na mbele"[emoji23][emoji23][emoji23] sijui alifikiria Nini kuimba vile
 
Nachekaga na ule mstari wa "naringia shape yangu Nina mvuto nyuma na mbele"[emoji23][emoji23][emoji23] sijui alifikiria Nini kuimba vile
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]labda anamaanisha amekamilika kila kitu
 
Ukizungumzia waimba taarabu wa kike wenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni basi Fatma Mahmoud Nyoro maarufu kama Fatma Mcharuko ni namba one.

Waimba taarabu wengi wanapata shida kugandamizia/ kuimba nyimbo alizoimba Fatma kutokana na upekee wa sauti yake.

Wasanii wa jahazi modern taarabu walikuwa wanapata tabu sana kuimba nyimbo za Fatma kipindi kile Fatma mjamzito ,walikuwa wanaziharibu haswa tofauti na nyimbo za wengine hata wasipokuwepo lazima mbadala atakuwepo kuweza kuziba pengo hilo.

Bendi nyingi sana za taarabu zinatamani sana kuwa na Fatma katika bendi yao kutokana na upekee wa sauti.

Fatma alishawahi kutamba na vibao kama vile Mfamaji, Maruperupe,Aso kasoro, kwa sasa anasumbua na ngoma ya Siwaguni wala siwakohoi.

Fatma kwa sasa anaitumikia bendi ya Yah TMK na ndiye msanii aliyefanikiwa kuwajazia mashabiki bendi hiyo kutokana na umahiri wa uimbaji wake.View attachment 1195219
Nyoro si ni MNDUKU... Kwa hiyo anaitwa Fatuma MNDUKU eti....
 
Back
Top Bottom