FBI yadai kupata ushahidi mpya mauaji ya Rais John Kennedy

FBI yadai kupata ushahidi mpya mauaji ya Rais John Kennedy

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
458
Reaction score
1,280
Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) limesema limepata ushahidi mpya kuhusu mauaji ya aliyekuwa Rais wa Marekani, John F. Kennedy, ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Donald Trump.

FBI imesema imepata nyaraka mpya 2,400 zinazohusiana na ushahidi wa mauaji hayo, na tayari imeanza kuzifanyia kazi nyaraka zote.

Tamko la FBI linakuja siku chache baada ya Trump kuagiza kuwa upelelezi wa tukio la mauaji ya Rais Kennedy uanze upya, pamoja na mauaji ya mdogo wake, Robert Kennedy, na uchunguzi wa haki za kiraia za Martin Luther King Jr.

Mauaji ya Rais Kennedy yaliyotokea Novemba 22, 1963, huko Dallas, Texas kwa kupigwa risasi na Lee Harvey Oswald, yamekuwa yakihusishwa na nadharia nyingi kwa miaka mingi, huku mamilioni ya Wamarekani wakiwa na mashaka juu ya wahusika halisi wa mauaji hayo.

Mwaka 2023, katika kura za Gallup, asilimia 65 ya Wamarekani walionyesha kutoamini ripoti ya Tume ya Warren, ambayo ilihitimisha kwamba Lee Harvey Oswald alimua Rais Kennedy bila kushirikiana na mtu yeyote.
Pia Soma:

 
12 February 2025

Mkuu wa jopokazi jipya la uchunguzi asema kwa miaka mingi walitufanya kama watoto, wabaini mapya ya JFK


View: https://m.youtube.com/watch?v=FkjuYEHiqgk
Mkuu wa jopokazi jipya la bunge linalolenga kufichua "siri za shirikisho" amefichua kuwa anaamini "wapiga risasi wawili" walihusika katika mauaji ya Rais wa zamani wa Marekani John F. Kennedy (JFK). Kikosi kazi kitachunguza mauaji ya JFK, Robert F. Kennedy (RFK) na Martin Luther King (MLK). Pia itachunguza orodha ya wateja wa Epstein, asili ya COVID-19, Wafanyakazi...
 
Mauaji ya mwaka 1963 yanachunguzwa Leo 2025 inakuaje Sisi TANZANIA tunashindwa kuchunguza waliojaribu kumuuwa tundu lissu
Usihadaike sana mengine huwa ni propaganda!, halafu usijipe tumaini sana taarifa watakazotoa kwamba nizakweli zinaweza kutolewa taarifa zinazoendana na ukweli tu ili kutuliza wanaopiga kelele kuhusu hilo sakata!.
Michezo ya siasa na dini unatakiwa kwenda na akili ya ziada!.
 
12 February 2025

Mkuu wa jopokazi jipya la uchunguzi asema kwa miaka mingi walitufanya kama watoto, wabaini mapya ya JFK


View: https://m.youtube.com/watch?v=FkjuYEHiqgk
Mkuu wa jopokazi jipya la bunge linalolenga kufichua "siri za shirikisho" amefichua kuwa anaamini "wapiga risasi wawili" walihusika katika mauaji ya Rais wa zamani wa Marekani John F. Kennedy (JFK). Kikosi kazi kitachunguza mauaji ya JFK, Robert F. Kennedy (RFK) na Martin Luther King (MLK). Pia itachunguza orodha ya wateja wa Epstein, asili ya COVID-19, Wafanyakazi...

Duh!...noma sana...
 
Hakuna ukweli na nia ya wazi ya kuwajua waliopanga na kumuua JFK. Hata Trump anajua Lee Harvey Oswald si yeye peke yake aliyeamua kumuua JFK.
Na anajua si kweli kwamba ana nia ya kugundua Kwa uwazi kwamba JFK aliuawa na mfumo kwasababu alitaka normalization ya uhusiano na Soviet Russia.
Na anajua hata akiforce sanaa nae anaweza kwenda kama mwenzake Jfk.
Anachofanya ni mchezo wa kujitekenya na kujicheka.
 
Karata tatu, chekundu, cheusi. Ukiangalia huku, unapigwa kule.
 
Back
Top Bottom