Fedha ya Serikali inavyopigwa na Halmashauri kupitia Waalimu

Fedha ya Serikali inavyopigwa na Halmashauri kupitia Waalimu

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2019
Posts
1,213
Reaction score
1,918
Pamoja na fedha ya Serikali kuwekewa Ulinzi mzito kwenye awamu hii ya tano lakini bado wapo wajanja wanaendelea na upigaji tena kiulaini.

Ipo hivi, huu mchezo unapigwa Halmashauri za Wilaya/Manispaa. Wakitaka kupiga hela wataanza kutoa Taarifa kwa wafanyakazi katika Wilaya husika kwamba kutafanyika Uhamisho wafanyakazi wa ndani ya wilaya yao, haswa haswa waalimu kutokana na uwingi na uoga wao huwa ndo wanaotumika. Baadae wataingiza fedha kwenye akaunti za wale waalimu wanaoonekana watafaa kwa huu mchezo wao. Au muda mwingine hawatoi taarifa za Uhamisho ila wataingiza hela kwenye akaunti tu.

Sasa baada ya siku mbili au tatu huyu mfanyakazi aliyeingiziwa fedha ya Uhamisho anapigiwa simu na mtu wa Halmashauri akimweleza kuwa amehamishiwa kwenda shule ya mbali halafu atamwambia kama anataka asipelekwe basi amrushie zile fedha zote za Uhamisho alizoingiziwa na atapangiwa shule ya karibu.

Kama kawaida mtu mfano tayari yupo anaishi na familia yake ukimletea habari za Uhamisho kwenda sehemu za porini basi atakuwa tayari kufanya lolote, kwahiyo atarusha zile pesa kwa yule aliyempigia naye atahamishiwa shule ya karibu ili kuhalalisha matumizi ya fungu la fedha.

Kwahiyo hawa akina CAG wakipita kila kitu kinakuwa sawa na wao maisha yanaendelea..

Nafikiri wazo la Kishimba lifanyiwe kazi hiko Chuo cha Wizi kianzishwe mapema.
 
Lisemwalo lipo, nadhani wahusika kama siyo sehemu ya huo mchezo mchafu watalifuatilia.
 
Bado kuna mianya mingi ya ufujaji wa hela za umma katika Halmashauri zetu, vyombo husika viangazie macho huko
 
Sasa si useme tu Wilaya/Halmashauri uliyopo badala ya ku generalize kana kwamba hilo tatizo ni la Tanzania nzima!
 
Mkuu umeishia mbali sana taja halmashauri tu tutashughulika nalo kwa haraka
 
Usizani CAG anahakili za kondoo hivyo! CAG anafuatilia kila kitu! Km nimwl. Kuhama lazima ajiridhishe km kweli alihama , nakituo chake kipya cha kazi km yupo
Hamna lolote, wakaguzi Mara nyingi huishia wilayani lakini laiti wangekuja chini kabisa kwa watumishi naamini wapo wakurugenzi na wakuu wa idara wengi wasingekuwepo kwenye hizo nyazifa
 
Usizani CAG anahakili za kondoo hivyo! CAG anafuatilia kila kitu! Km nimwl. Kuhama lazima ajiridhishe km kweli alihama , nakituo chake kipya cha kazi km yupo
Kama unafanya au umeshawahi fanya kazi serikalini huwezi kushangaa hili jambo..

Hivi unajua kwenye kipindi kama hichi ambacho mwaka wa fedha uaelekea ukingoni, KUNA mchezo mchafu kwenye HALMASHAURI zetu ambapo YANAFOJIWA MADOKEZO yasiyo na idadi na wanapiga chenji zinazobakia. Yaani kipindi hiki huko maofisini unakuta watu wanafosiwa wasaini vitu ambavyo havikuwahi kufanyika..
Na hapo CAG anapita na kila kitu ni OK..
 
Ningeamini CAG anafanya kazi kama angekuwa anafatilia kwa umakini pesa ya elimu bure. Yaan kuna mkuu mmoja wa shule na wenzake halmashauri niliopo kila mwezi pesa inaonekana imetumika lakini hadi chaki tunaenda azima shule ya jirani. Boksi la chaki linaandikiwa hadi laki 1. Boksi la kalamu hadi elfu 20 linaandikiwa. Pedi za wasichana zinaandikiwa ila sijawahi ona hata moja imenunuliwa. Achia mbali vifaa vya maabara vinaandikwa vimekuja ila havionekani. Ukikomaa unajikuta upo peke yako. Maticha wenzako woote ni waoga hata hawaulizi chochote. Bank statement inasoma kuna elfu 7 wakati kwenye vikao vya SMT balance mmnajua ipo karibu milioni. Mzabuni ndo mkuu wa shule sijui sheria ya manunuzi inazingatiwaje hapo. Waalim ukiwambia hii sio sawa wanaogopa.
Yaan kazi ya CAG binafsi sijaiona huku mashuleni. Shule nyingi ni miradi ya wakuu wa shule na maafisa elimu kupitia elimu bur . Elimu imeoza tuseme ukweli.
 
Ningeamini CAG anafanya kazi kama angekuwa anafatilia kwa umakini pesa ya elimu bure. Yaan kuna mkuu mmoja wa shule na wenzake halmashauri niliopo kila mwezi pesa inaonekana imetumika lakini hadi chaki tunaenda azima shule ya jirani. Boksi la chaki linaandikiwa hadi laki 1. Boksi la kalamu hadi elfu 20 linaandikiwa. Pedi za wasichana zinaandikiwa ila sijawahi ona hata moja imenunuliwa. Achia mbali vifaa vya maabara vinaandikwa vimekuja ila havionekani. Ukikomaa unajikuta upo peke yako. Maticha wenzako woote ni waoga hata hawaulizi chochote. Bank statement inasoma kuna elfu 7 wakati kwenye vikao vya SMT balance mmnajua ipo karibu milioni. Mzabuni ndo mkuu wa shule sijui sheria ya manunuzi inazingatiwaje hapo. Waalim ukiwambia hii sio sawa wanaogopa.
Yaan kazi ya CAG binafsi sijaiona huku mashuleni. Shule nyingi ni miradi ya wakuu wa shule na maafisa elimu kupitia elimu bur . Elimu imeoza tuseme ukweli.
 
Back
Top Bottom