Fedha zilizo expire kurudishwa kwenye mzunguko, kuna harufu ya ufisadi.

Fedha zilizo expire kurudishwa kwenye mzunguko, kuna harufu ya ufisadi.

gstar

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2011
Posts
790
Reaction score
1,373
Tunapo karibia uchaguzi mkuu pesa itatafutwa kwa njia yoyote ile ikiwemo ya halali na ya haramu. Hatuwezi kupuuzia jambo dogo kama hili la kubadilisha fedha ambazo kimsingi zilisha pita muda wake wa matumizi, ni fedha zilizo kwisha ku-expire.

Nadhani ni fedha ambazo hazipaswi kurudishwa tena kwenye mzunguko. Ninavyo fahamu mimi kabla ya ku introduce note mpya tangazo lilipita na watu wakazibadilisha note hizo, inakuwaje tena sasa ionekane kuwa note hizo bado zina thamani ile ile ya tangu miaka ya 95 ama 2003?

Kutokana na kufikiria kwa kina nimehisi hapa kuna harufu ya utakatishaji fedha, na kutokana na maoni ya wadau mbalimbali nimegundua vitu kadhaa.

(i) Ni fedha ambazo watu walizificha kwenye masandarusi na mahandaki na sasa wanatumia mwanya wa kuzirudisha ili wapewe fedha halali na wazirudishe kwenye mzunguko.

(ii) Ni fedha zilizoibwa kwenye mambenki ambazo zilisha pita na muda wake na wahusika wakitumia njia ya kuzihalalisha ili zirudi kwenye mzunguko.

(iii) Ni fedha halali na inafaa zirudi benki ili zifutwe kabisa na kupatikana fedha mpya. (Hii ni kwa maono ya BOT wenyewe)

Kwa maoni yangu mimi hapa kuna harufu ya ufisadi mwingine unao enda kutokea. Tusijifunze kupuuzia kila jambo, jambo hili laweza kuonekana kuwa dogo lakini likawa na impact kubwa hasa kwenye uchumi wa nchi yetu kwani kitaalamu hatuelewi ni idadi kiasi gani ya fedha hizo ambazo hazikubadilishwa kwa sababu kadhaa ikiwemo hofu ya kukamatwa ama kutaifishwa.

Iwapo zikiwa ni chache haziwezi kuwa na athari kubwa lakini iwapo zikiwa ni ma billions ya shilingi inaweza kuleta changamoto hasa kwenye uchumi wa nchi yetu. Isije ikawa nia hii njema ya BOT ikaingiliwa na watu wasio kuwa na nia njema na hasa wenye nia ya kutakatisha fedha.

Tujadili bila kutumia personal attacks, twende hoja kwa hoja lengo ni kueleweshana.
 
Hata kama mimi siyo mchumi! Ila naona kama kuna kitu serikali inakificha juu ya jambo hili! Maana lilishapita kitambo. Na hatukuwahi kusikia watu wakilalamika labda muda ulikuwa mfupi wa kurejesha hizo hela zilizo ondolewa kwenye mzunguko.

Au serikali inataka kuchapisha fedha mpya na kuziingiza kwenye mzunguko kutumia hiki kisingizio! Au kweli kuna watu walificha hela za wizi/ufisadi miaka hiyo kwa kutumia njia ambazo siyo rasmi! Na sasa wametumia ushawishi wao ili wazirejeshe benki, na hivyo kupatiwa pesa nyingine!
 
Kwa kuwa kuchapisha noti mpya ni gharama tena ya pesa za kigeni ambayo hatuna ya kutosha kama Nchi, ni vyema ufafanuzi wa kina juu ya umuhimu wa hatua hii kiuchumi na kisiasa utolewe kwa uwazi kwa wa-Tanzania kabla ya zoezi hilo kuanza. Isipofanyika hivyo, wa-Tanzania ambao jasho lao ndilo litakalolipia kwa pesa za kigeni, gharama ya kuchapisha noti mpya, watalazimika kuamini kuwepo kwa mbinu, mikakati na mengine yanayotajwa.
 
Nyei watu gani hampendi pesa? Kama ime expure lakini inakybalika na inabeba thamani ile ile who cares? Tanzania hii ni kubutua kwenda mbelw, ukizipata tumia. Kama huna zitafute hata kwa kukaba, ukizipata zitumie kuhonga ukae sawa.
Pesa ngumu, tumieni any means necessary. Kama zipo wazimwage, nchi haina mwenyewe hii.
Mkiwasikiliza ccm mtaumuia nyie, nanyi kuleni kwa urefu wa kamba zenu, iba, kaba vyovyote vile tafuteni pesa. Mta deal na sheria muda utakapofika wa kudeal na sheria, kwa sasa ni lawless country.
 
Una hoja nzuri.
(IV) Ni fedha hewa ambazo itadaiwa labda zimerejeshwa kiasi cha Tsh 50Bln hivyo waliorejesha wamelipwa kwa noti mpya. Hapo watu wametengeneza 50B from thin air.
 
Back
Top Bottom