Fei Toto huwezi kuwakwepa Yanga, ukivuliwa nguo chutama

Fei Toto huwezi kuwakwepa Yanga, ukivuliwa nguo chutama

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Kwa mara nyingine naona Bwana Fei Toto kawasilisha barua TFF ya kutaka kuvunja mkataba na Yanga. Mpaka sasa nafikiri yeye na watu wake washashtuka na kuona kuna mahala waliteleza ndio maana wanakwepa kupeleka mashtaka CAS.

Kwa akili ya kawaida baada ya review yake kugonga mwamba, alitakiwa anyooke CAS moja kwa moja kama alikuwa anaona hajatendewa haki, na anaona alichokifanya alikuwa sahihi kwanini tena awasilishe barua nyingine wakati anadai ameshavunja mkataba na waajiri wake?

Hiki ni kichekesho kingine anapeleka barua TFF, kwani TFF ndio waajili wake? TFF inawezaje kuvunja mkataba wake wakati washamwambia ni mchezaji halali wa Yanga? Anajaribu kuwakwepa Yanga lakini hatoweza, ni mpaka atarudi kwao tu.

Hata akiruka akaenda wapi, TFF watamwambia aende akaongee na waajiri wake na si vinginevyo, kiburi chake hakiwezi kumsaidia hata alete Wanasheria kutoka Sayari ya Mars hawezi toboa kwa staili anayotaka yeye.

Kuongea na Yanga hakuepukiki, aende wamtajie dau lao la kuvunja mkataba endapo watakubaliana na sababu anazozitoa na si vinginevyo, na ziwe sababu zilizoshiba zinazoendana na muongozo wa mikataba ya FIFA otherwise haitokuwa rahisi pia.

Dawa ya kiburi ni jeuri, asisahau hilo.
 
Kwa namna Tafsiri za wakili msomi Shangazi Fatma akinukuu Sheria za FIFA kama Yupo sahihi kuwa, Mchezaji sio mtumwa anaweza kuingia mkataba na ku uvunja bila Sababu yoyote Ili mradi mchezaji hafurahii mazingira ya kazi.

Tafsiri hii Ina maanisha upo uwezekano mchezaji katika Kila dirisha la usajili liwe dirisha dogo au kubwa anaweza Kuvunja mkataba na kuondoka kwakua yeye si mtumwa atakama klabu imekutimizia matakwa yote ya ki mkataba.

Mwenye kufahamu anisaidie ni mchezaji gani aliwahi Kuvunja mkataba uko Duniani kwakua yeye si mtumwa akaondoka klabuni bila klabu inayo mmiliki kuhusishwa, Sababu ikiwa kula ugali na sukari au yoyote Ile ikiwa makubaliano ya kimkataba hayajawahi Kuvunjwa na klabu na FIFA ika toa baraka zote.
 
wanaomba TFF ndio wavunje mkataba ,naona kaenda na mamaa Jasmine yule mdada anasaida wachezaji Ulaya huko
 
Karume anapotosha, kutumikia mkataba si utumwa na huwezi kusema hufurahii mazingira ya kazi wakati kila hitaji la mkataba unatimiziwa.
 
Feisal amekataa ushoga ndiyo mateso yote haya. Komaa hivyo hivyo dogo kama wanaona mazuri wafanyane wenyewe.
Awa vipi?
Screenshot_20220404-175820.jpg
 
Naskia mnamtishia kuwa nyie ndo wananchi,mmejazana uhamiaji,mahakamani na kila mahali so mtampoteza..ACHENI USHAMBA
 
Back
Top Bottom