Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Said ana upuuzi fulani asee!! Nimeanza kumdharau kabisa.. ukanjanja unataka kuwa mwingi kwenye mambo yanayohitaji taratibu.Na wakati ukisema hayo nakukumbusha, mbinu anayoitumia FEI kutoka UTO ndiyo mbinu hiyo hiyo ilitumiwa na UTO kuwachukua GADIEL MICHAEL na SURE BOY... toka Azam, tofauti ni kwamba wote hao wawili Azam haiutaka kuwadai Fidia huku Sure Boy akipewa Option ya kurudi Chamazi km yatamshinda huku aendako!
KARMA is a Bitch
Mshauri afuate utaratibu, na pia ajitahidi kuwa muungawana. Yanga imemsitiri!Kama feisal hana impact yoyote kwa yanga toka alipoaga kwanini mnaendelea kumng'ang'ania? Si mumuache akatafute maisha sehemu nyingine!
Unachoshangaa hivyo nini?Ndio moyo wa mtu kichaka umeficha mengi sana mabaya na mazuri,meupe na meusi, damu na maji...nk
Hakika msemo huu pasipo na shaka Feisal ametuonyesha maana yake, nani aliamini Feisal yule aliyekua anashangilia kwa kuibusu nembo ya Yanga pamoja na kwenda kwenye Camera na Kuisema I LOVE YANGA.
Pamoja na yote hayo hutoamini leo Feisal anasumbuana na Yanga Pale Tff huku akiwa amejaza mawakili karibia watatu kweli maisha haya yanabadilika binafsi nakiri bado sijaona mengi kwenye hii dunia Ndio RAFIKI YAKO ANAWEZA KUWA ADUI YAKO AND VICE VERSA IS TRUE.
Feisal aliyepita kwenye Nyakati ngumu na Yanga anzia kipindi kile cha bakuli yanga ikipitisha, akitumiwa na Zahera kama namba 6 na kucheza rafu nyingi na kula kadi za njano nyingi tu leo yupo pale Tff akizozana na Yanga.
Nani alitegemea kijana wa Byuti Byuti angeleta Mikwara wakati Yanga ikijiandaa na gemu ngumu na Azam kama ni mawazo ya kijana hakika kijana ana misimamo ila kama kuna watu nyuma yake wana lengo katili sana na timu ya Yanga.
Wapo wanaoamini Yanga imeundwa kupitia Feisal hii nchi kuna mengi kuna wivu, husda, tamaa mbaya, uchawi...nk hapo unaweza kukuta ni kakikundi cha watu wenye pesa zao wameungana kwa lengo la kuikomoa Yanga na kuirudisha nyuma bila kuwaza either wanamwaribia dogo au wanamsadia.
Kiuhalisia Yanga ni Taasisi Kubwa, Yanga ni Serikali kwanini Yanga ni serikali kuna watu wapo tiyari kufa kwa ajili ya Yanga tena mkulima tu wa huko sitimbi ndani ndani,Yanga anamiliki wananchi wake walio tiyari kwa lolote lile ni ngumu Feisal kushindana na Yanga yeye kama yeye labda kama atakua kwenye upande wa haki tu kwa njia haramu labda hao wanaomtumia wana mpunga au Tff waamue kupindisha Sheria.
Yes hatukatai Feisal alikua mchezaji muhimu Yanga lakini jiulize tangu ameondoka Yanga imepoteza michezo mingapi ? Feisal kapandisha kiwango miaka hii miwili ya Nabi baada ya kumtoa namba 6 na kumsogeza mbele na pamoja na kuzungukwa na wachezaji wazuri sisemi vibaya ila bado alikua na mengi ya kujifunza.
Bado hajawahi mchezaji wa kutegemewa ndio maana hata kwenye timu ya Taifa bado hana namba ya kudumu na hata akicheza hamalizi dakika 90 ndio narudia bado alikua na mengi ya kujifunza.
Na huu ndio ulikua wakati sahihi wa kudai DAU KUBWA KWA NJIA STAHIKI NA SIO ALIZOTUMIA YEYE WENYE LUGHA YAO WANASEMA JANJAJANJA MJINI, bado alikua na uwezo wa kukaa na timu ya Yanga na kuzungumza.
All in all yote heri kama kijana anaona njia aliyotumia ni sahihi its ok ila ni vema angeondoka na baraka za wazee nakumbuka kisa cha Maicon wa Brazil huyu jamaa alitakiwa kusajiliwa na timu moja ya italia kutoka timu ya Ufaransa Barcelona wakahijack ndege iliyombeba na kumshusha pale Nou camp kwa kifupi maisha ya jamaa Barca yalikua magumu sana.
Kijiji kisicho na wazee usiishi.
unataka aondoke bure? hujui klabu zinategenea wachezaji kuuzwa?Kama feisal hana impact yoyote kwa yanga toka alipoaga kwanini mnaendelea kumng'ang'ania? Si mumuache akatafute maisha sehemu nyingine!
Mkuu hapa wasipokuelewa, ni basi tu kwa kuwa kauli ya Haji Manara inaakisi ukweli kule Utopoloninyo.Na wakati ukisema hayo nakukumbusha, mbinu anayoitumia FEI kutoka UTO ndiyo mbinu hiyo hiyo ilitumiwa na UTO kuwachukua GADIEL MICHAEL na SURE BOY... toka Azam, tofauti ni kwamba wote hao wawili Azam haiutaka kuwadai Fidia huku Sure Boy akipewa Option ya kurudi Chamazi km yatamshinda huku aendako!
KARMA is a Bitch
Wacha bwanaa. Nyie si ndiyo mulimficha Ngasa na kumshauri azime simu wakati watu walikuja na mapesa yao ili wamsajili (nadhani viongozi wa timu mojawapo toka Sudan kama sikosei). Hamuwatakii mema au mafanikio wachezaji wenu. Mmemwachia Ngasa akiwa amekomaa kama bamia, kaenda South mpira umeisha, hakuchukuwa round huyu akarudi kucheza mpaka Ndanda. Kudadadek.Mshauri afuate utaratibu, na pia ajitahidi kuwa muungawana. Yanga imemsitiri!
Simba ilimpotezea kumsaini. Azam ndiyo kwanza hawakuwahi hata kumuona kama ni mchezaji wa kumshajili! Ilimsajili, na baadaue akaboreshewa mkataba wake mpaka 2024!
Katika mazingira ya kawaida kabisa, Dogo alitakiwa kukaa mezani na Yanga kabla ya kufanya hicho alichokifanya. Yanga haina nongwa na mchezaji yeyote yule! Na ndiyo maana hata wakina Msuva walichezq kwa mafanikio, na baadaye wakaondoka.
Mtu kama Mrisho Ngasa, amecheza Yanga, akaondoka! Akarudi! Akaondoka tena!! Yaani mpaka dakika za mwisho anaachwa, tayari alishakuwa mwanajumuiya wa klabu ya Yanga.
Matured comment from sportsladyPoleni sana nawatakia kila la heri
Yanii WIN WIN SICHUESHENI
Ishu ya Ngasa ina utofauti kidogo na hii ya Feisal. Ngasa alikuwa ni mtoto wa mjini. Ilikuwa ni ngumu kumpeleka Sudan, halafu aache kula bata katika Jiji la MakambaWacha bwanaa. Nyie si ndiyo mulimficha Ngasa na kumshauri azime simu wakati watu walikuja na mapesa yao ili wamsajili (nadhani viongozi wa timu mojawapo toka Sudan kama sikosei). Hamuwatakii mema au mafanikio wachezaji wenu. Mmemwachia Ngasa akiwa amekomaa kama bamia, kaenda South mpira umeisha, hakuchukuwa round huyu akarudi kucheza mpaka Ndanda. Kudadadek.
Pamoja mkuu...Matured comment from sportslady
sawa mtamuYote machafu tu na ni kielelezo tosha tu.
Ha ha hasawa mtamu
Ila Ngasa Ni bonge la kenge aisee yaani aliitema milioni 300 za wasudani ili achezee utopolo leo hii hata hela ya kulipia kuingia uwanjani hana na utopolo hawamkumbuki.Wacha bwanaa. Nyie si ndiyo mulimficha Ngasa na kumshauri azime simu wakati watu walikuja na mapesa yao ili wamsajili (nadhani viongozi wa timu mojawapo toka Sudan kama sikosei). Hamuwatakii mema au mafanikio wachezaji wenu. Mmemwachia Ngasa akiwa amekomaa kama bamia, kaenda South mpira umeisha, hakuchukuwa round huyu akarudi kucheza mpaka Ndanda. Kudadadek.
Ila nyinyi utopolo ni wachawi yaani mnamtemesha kijana wa watu milion 300 alafu leo hata hela ya kiingilio uwanjani anakosa ?Ishu ya Ngasa ina utofauti kidogo na hii ya Feisal. Ngasa alikuwa ni mtoto wa mjini. Ilikuwa ni ngumu kumpeleka Sudan, halafu aache kula bata katika Jiji la Makamba
Alikuwa na uwezo wa kwenda kucheza Sudan. Ila hata yeye mwenyewe hakuwa na mzuka wa kwenda. Kwa Fei Toto, ni tofauti. Yeye ameamua kutukimbia, katika kipindi ambacho angeweza kutumia njia ya kiungwana ya kukaa na waajiri wake.
Umeandika ukweli mtupu hata luc eyamel aliyasema haya mkaja mkalia lia kawatusi wakati aliwaeleza ukweliYanga ya Said wa Gsm Ina mazuri lakin ina mapungufu mengi sana kiutawala, na kimsimgi wapo kiujanaujana na usela mwingi Sana ktika Mambo ya msingi...!!. Ndio Fei anaweza akawa asiwe sahihi au sahihi lakini mbona kuna muendelezo wa matukio yanayofanana??, Morrison Sasa Fei na kwa mtazamo wakishabiki utaona yanga ndio ina haki lakini kumbe n propaganda na utoto!!.
Ni aibu kwa timu kubwa Kama yanga kuhangaika na mchezaji ambaye replacement yake kwenye kikosi ipo na anaweza sahaulika ndani muda mfupi Sana, viongozi wetu wajifunze kilibali na kuachana na Mambo ambayo wamekosea.