Abby Newton
JF-Expert Member
- Nov 12, 2017
- 1,252
- 2,253
Niseme tu kwa mara ya kwanza nimemuona Carlinhos akichezeshwa nafasi sahihi anayoimudu na aliitendea haki haswaa! Nadhani makocha waliopita hawakuliona hilo na hii ndio faida na hasara ya kubadilisha makocha. Kuna wa kunufaika na wa kuumia. Kufa kufaana.
Yanga ina mapungufu mengi lakini kukosa kiungo laini,mwenye akili, kasi, na uharaka wa maamuzi ndio vimekuwa vikiigharimu sana timu. Feitoto pamoja na uwezo wake wa kumiliki mpira na kukaba anatatizo la kupiga " Square pass" nyingi, anakosa sifa tajwa hapo juu.
Carlinhos aliimudu vilivyo nafasi ya kiungo namba 8, alimfundisha Feitoto nini maana ya kiungo mshambuliaji. Carlinhos anamacho, anaongozwa na akili,"He has an amazing passing accuracy" Ni nadra mno kumuona akipiga pasi mkaa, lakini pia ni"attacking minded"Mbele kwa mbele!
Endapo Yanga ingekuwa na "quality players" wa kiwango cha Carlinhos basi si ajabu Yanga angeshinda zaidi ya goli 3. Tatizo Mipira inapotea sana eneo la mbele, nidhamu ya kuutunza mpira si ya kutosha.
Kwa mechi ya Yanga vs Biashara kwangu Carlinhos ni "Man of the Match". What a player!
Natamani kumuona Carlinhos uwanjani mara nyingi zaidi kuanzia sasa.
Yanga ina mapungufu mengi lakini kukosa kiungo laini,mwenye akili, kasi, na uharaka wa maamuzi ndio vimekuwa vikiigharimu sana timu. Feitoto pamoja na uwezo wake wa kumiliki mpira na kukaba anatatizo la kupiga " Square pass" nyingi, anakosa sifa tajwa hapo juu.
Carlinhos aliimudu vilivyo nafasi ya kiungo namba 8, alimfundisha Feitoto nini maana ya kiungo mshambuliaji. Carlinhos anamacho, anaongozwa na akili,"He has an amazing passing accuracy" Ni nadra mno kumuona akipiga pasi mkaa, lakini pia ni"attacking minded"Mbele kwa mbele!
Endapo Yanga ingekuwa na "quality players" wa kiwango cha Carlinhos basi si ajabu Yanga angeshinda zaidi ya goli 3. Tatizo Mipira inapotea sana eneo la mbele, nidhamu ya kuutunza mpira si ya kutosha.
Kwa mechi ya Yanga vs Biashara kwangu Carlinhos ni "Man of the Match". What a player!
Natamani kumuona Carlinhos uwanjani mara nyingi zaidi kuanzia sasa.