Feitoto agoma kurudi Uto, ataka review ya hukumu ya TFF

Maslahi mazuri kwa Fei inawezekana.
Umshauri sasa arudi kambini ili akaendelee kuipambania timu, na mwisho wa siku apate hayo maslahi yake mazuri.

Na kama hana mahaba na timu kama inavyo semekana, basi akafuate utaratibu sahihi wa kwenda kwenye timu aliyo na mahaba nayo. Na siyo kutumia njia ya mkato.
 
Unadhani haya mambo wakiya endekeza kitatokea nini? Kesho atakuja Job, next time Kibwana and so on itakuaje?
 
Katika nchi hii, ni Fei Toto pekee ndiyo mchezaji mzawa anayelipwa mshahara mdogo wa milioni 4 kwa mwezi?

Wachezaji wote wazawa wenye viwango vya uchezaji kama Fei Toto kutoka simba, Azam, Singida Big Stars, nk wanalipwa mshahara wa milioni 23 kwa mwezi?
 
Alikuwa kambini bila maslahi mazuri boss na hakuna aliyemshawishi asiondoke mpaka wakaja wengine kutoka nje.
 
Unadhani haya mambo wakiya endekeza kitatokea nini? Kesho atakuja Job, next time Kibwana and so on itakuaje?
Wote wana kiwango kikubwa? Kama ndio sawa wapewe maslahi, kama sio na wakataka maslahi si unamwacha aondoke?
 
Ķama fei ni sawa na hawa wengine kwann anatakiwa abaki ili hizo zinazoitwa taratibu zifuatwe? Si ili auzwe kwa bei kubwa club ipate fedha?

Fei sio mchezaji kama hao wengine, ingekuwa hivyo sio tu kwamba viongozi wa Yanga wangemruhusu, bali wangefurahia kumruhusu huku yeye akiwa kadeposi fedha za mishahara yake mitatu na signing fee sijui. Tena wangesema wazi HAYUPO KWENYE MIPANGO YA TIMU, TUNAMTAKIA KILA LA HERI HUKO AENDAKO.
 
Mkuu hata wewe jifikirie tu, Feisal katika ubora ule aliokuonesha uwanjani ambao ni zaidi ya hao wanaochukua 20+M, hivi kwa mtu mwenye busara unaweza ukasubiria uombwe kuongeza mshahara wakati unaona?
Mchezaji anatakiwa kujua thamani sio kusubiri mpaka ufanywe fadhira, as long as alisaini mkataba wake wa sasa basi anatakiwa kuutumikia
Kuhusu suala la mkataba kwanza imevujishwa page moja tu na mkataba una page zaidi ya tatu sio sawa kutolea hitimisho wakati hujasoma mkataba mzima. Pili hivi vipengere vya kuvunja mkataba vinawekwa ili mkichokana basi kuwe na namna rahisi ya kuachana pasipo kukomoana mfano kutajiana pesa kubwa kama wanavyofanyiwa wasanii wa wasafi wakitaka kuondoka wanaambiwa watoe bilioni na utata unaanziaga hapo wangeshakubaliana dau la kuvunja mkataba tangu mwanzo iyo isingeleta utata release clause inawekwa tu ili mkikubaliana kuachana usiibuke utata au mambo ya kukomoana ila haimaanishi kwamba mtu unaweza kudeposit tu iyo pesa ukawa huru kimkataba, mkataba mmesaini pande mbili kwaiyo kuuvunja lazima mkae mezani pande mbili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…