Msanii Ferooz
Ferooz amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio na kudai kuwa mtaani kulikuwa na maneno kuwa amenunuliwa gari aina ya Jeep na Rais jambo ambalo si kweli.
"Mimi nashukuru Mungu Rais Mkapa alizungumzia kwenye hotuba yake kuwa nimefanya jambo zuri kupitia wimbo wangu 'Starehe' na akasema nina stahili zawadi kwa kazi ile, hivyo katika kipindi hicho hicho mimi nilikuwa ndiyo nilikwenda kununua ile gari Jeep, kwa hiyo ile gari nilinunua kwa pesa zangu za muziki nilikwenda kununua Dubai na kuiingiza nchini mwenyewe, hata hiyo zawadi ambayo Rais alisema nastahili kupata sikuwahi pata" alisema Ferooz.
Mbali na hilo Ferooz anasema gari hilo baadaye alikuja kuliuza kwa kuwa aliona tayari limepitwa na wakati
"Ile Jeep kwa kifupi baadaye nilikuja kuiza maana ingekuwepo mpaka leo huenda ingekuwa banda la kuku, kwa hiyo niliiuza kama miaka kumi iliyopita huko" alisisitiza Ferooz
Mbali na hilo msanii huyo ameahidi kuwa sasa anajipanga kuja kivingine katika muziki na kuwataka mashabiki kutotilia manani maneno ambayo yapo mtaani na kusema watu wanakuwa wazushi kwa mambo ambayo hawayajui
Chanzo: EATV