Fid Q nani kakuloga? Umeanza kurithi ujinga na Chuki za Ali Kiba dhidi ya wasanii wenzake! Walichokifanya msibani ni kitendo cha kijinga na kishamba!

Haha wewe jamaa bhana sema ukweli unajua nn kitatokea ila ukweli umeamua kuukalia kisa chuki....
Siyo chuki mkuu, mtu anapopuyanga lazima umchane, isiwe kwa sababu unampenda mtu basi hata akifanya mambo ya hovyo unapiga makofi, huo sasa umaandazi. Na haimaanishi ukimkosoa mtu unamchukia!
 
Samahani mkuu, kwani alikufa?
 
Sioni tatizo lolote kwa msanii yoyote hapo wala simlaumu harmonize ulinzi ni muhimu kwa msanii kama harmonize pia inasaidia kulinda brand yako nashauri tu wasanii hao wa wcb wangekuwa wanatuma wawakilishi tu hasa hiyo misiba ya mtaani huko
 
Harmonize alichemka kwenda msiban kwa style ile. Sie bado watanzania misiba tunaiheshimu kuanzia kimavazi. Mtu umeenda msibani umevaa hereni kweli

Ulitaka aendeje? Kwani kwenda na walinzi ni kosa?
 
Nimeangalia hiyo clip sijaona baya alilofanya huyo Dogo, unless kama alianza kupiga Watu au kutukana.

Hivi angekuja raisi au Waziri Mkuu hapo asingekuwa na Walinzi na camera?, au tunaona ni Wanasiasa tu wenye haki hiyo na si kada nyingine yoyote? kwani wao Wanasiasa ni binaadamu maalumu sana kuliko wengine? kama Mwanasiasa anaweza kuishi hivyo kwa nini na Mtu mwingine yeyote akifanya iwe nongwa?

Kila Mtu aishi maisha yake to the fullest maana hicho kifo kipo tu hata kama ukiamua kuishi maisha yako yote kwa kukaa tu chini ya mti asubuhi mpaka jioni, maana Waswahili kwa kutishiana kupitia msiba hatujambo.

Hata hivyo naona kama hili swala la Walinzi kwa Msanii ni la kisanii zaidi kuliko kumaanisha, ni sehemu tu ya sanaa yake hivyo ni vyema tukaacha kila mmoja akaishi maisha aliyochagua ili mradi asivunje sheria.

Wenzetu Wazungu hawako huko ndio maana wana muda wa kutosha kufanya ya msingi na sisi kazi yetu imebaki kuwaiga.
 
Sioni tatizo lolote kwa msanii yoyote hapo wala simlaumu harmonize ulinzi ni muhimu kwa msanii kama harmonize pia inasaidia kulinda brand yako nashauri tu wasanii hao wa wcb wangekuwa wanatuma wawakilishi tu hasa hiyo misiba ya mtaani huko

Watume wawakilishi kila siku si ndio mtasema oooh hawaendagi msibani?
 
kwn harmonize ni wa wcb? unachelewea wapi
 
Kwa hiyo walinzi ndiyo wanazuia usiuawe? Na wale marais wote wa Marekani wakati wanauawa nao hawakuwa na walinzi? Na wote wasio na walinzi wanauawa?
Man, tukiachana na suala la msibani, kwa celebrity ulinzi isn't all about kulindwa ili usiuawe bali kulindwa hata dhidi ya mashabiki wanaoweza kukuvamia kwa shangwe any time na kuvuruga kila kitu kama vile kama vile ratiba n.k!! Kwahiyo ma-bodyguard kwa celebrities ni kama watengeneza njia kwa msanii husika! Mchukulie mtu kama Diamond kwa mfano, akifika mahali lazima ataja shazi! Hawa wanaojaza shazi sio kwamba wanataka kumdhuru bali kumuona tu, na ikiwezekana hata wampe mkono! Kwahiyo ni lazima wawepo wa ku-maintain order!

Kitu ambacho sijakiunga mkono kwa Konde Boy ni hao bodyguards kuingia kwa mbwembwe! Wangeingia tu kwa kawaida ili kuhakikisha Konde Boy hazongwi zongwi lakini umuhimu wa kuwa nao, upo!!
 
Sasa hamooo Si ungekuja na I'd yako tuu tungekuelewa
 
kibongo bongo ukifanikiwa utachukiwa na ulowazd bila sabab xa mi hua najiulz je wahusika wanahc chuk itapunguz rizk ya unaemchukia...?, tujifunz kuwapenda w2 ili 2barikiw nasi
Kwani ukiandika maneno vizuri bando huwa linawahi kuisha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…