FIFA, UEFA washirikiana kuifungia Urusi michuano yote, klabu na timu za taifa

FIFA, UEFA washirikiana kuifungia Urusi michuano yote, klabu na timu za taifa

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA) kwa pamoja wametangaza kuzifungia timu zote za Urusi katika michuano ya kimataifa kuanzia ngazi ya klabu hadi timu za taifa hadi hapo itakapotolewa taarifa nyingine.

Mamlaka hizo za soka zote zimetoa tamko la pamoja, hiyo inamaanisha kuwa Urusi imeondolewa katika mbizo za kushiriki Kombe la Dunia Qatar 2022.

Maamuzi hayo yanafikiwa kutoka na Rais wa Urusi, Vladimir Putin kuagiza majeshi yake kushambulia Ukraine, hivi karibuni.

Hivyo, Urusi haitashiriki katika mchezo dhidi ya Poland uliopangwa kuchezwa Machi 24, 2022 na timu ya soka ya wanawake itakosa michuano ya Euro 2022.

FIFA na UEFA wamesisitiza kuwa soka ni mchezo wa umoja na amani ambapo pia UEFA imevunja mkataba wa udhamini wa paundi milioni 33.5 wa Kampuni ya Gazprom ya Urusi.

Source: The Sun

Fifa.jpg
 
Warusi ni wajinga Sana ...dunia yote inatakiwa tumtenge huyu mjinga
 
Mbona hawakufanya hivyo kwa Marekani ilipoovania Afghanistan au Syria? Mbona hawakuifungia Ufaransa walipoivamia Libya?

Mesut Ozil aliwahi kuondolewa kwenye kikosi cha timu yake na akaonywa na vyama vya mpira vya Ulaya alipokua akishangilia kwa kuonyesha fulana yenye maneno ya kuiunga mkono Palestine dhidi ya mauaji, ukatili na uvamizi wa Israel kule Ghaza na Ukingo wa Magharibi wa mto Jordan. Lakini sasa hivi ni ruksa kufanya hivyo kuonyesha mshikamano na watu wa Ukrain!!!!!!@!
 
Hao yuefa na fifwa ni wapuuzi kama wapuuzi wengine wakianza kuingiza siasa kwenye mpira itakuwa ndo mwanzo wa mgawanyiko. Bora yaundwe mashirikisho mengine kama ilivyo kwenye ngumi
 
Back
Top Bottom