FIFA yaiagiza Etoile Sahel kuilipa Simba fedha za usajili wa Okwi

FIFA yaiagiza Etoile Sahel kuilipa Simba fedha za usajili wa Okwi

sembo

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
4,350
Reaction score
3,451
Hii ni baada ya CAS kuiamuru Etoile Du Sahel kuilipa Simba Sc USD 300,000. Kiasi hicho kilikuwa ni kwa ajili ya uhamisho wa Okwi. Simba Sc iliamua kwenda CAS baada ya Etoile du Sahel kugoma kulipa ada ya uhamisho ikidai kua ina hali mbaya kiuchumi.

NB: "zaidi ya usd 300,000 + mkwanja wa mtani jembe + vyanzo vyetu vya mapato = Simba Sc Complex mitaa ya Bunju"

===============
===============

Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limeiagiza Etoile du Sahel kulipa kitita cha dola 300,000 (Sh milioni 480) pamoja na faini.

Fifa imeitaka klabu hiyo ya Sousse nchini Tunisia kuhakikisha inalipa fedha hizo ndani ya mwezi mmoja pamoja na faini ya dola 28.


[TD="align: center"] [/TD]

[TD="align: center"]OKWI (KUSHOTO) WAKATI AKIICHEZEA ETOILE KATIKA LIGI YA TUNISIA[/TD]

Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limeiagiza Etoile du Sahel kulipa kitita cha dola 300,000 (Sh milioni 480) pamoja na faini.

Fifa imeitaka klabu hiyo ya Sousse nchini Tunisia kuhakikisha inalipa fedha hizo ndani ya mwezi mmoja pamoja na faini ya dola 28,000.

Hatua hiyo imefikia baada ya Simba kushinda kesi iliyotokana na Simba kushitaki kwa Fifa baada ya Etoile kushindwa kulipa fedha za malipo ya kumnunua Emmanuel Okwi.

Okwi aliuzwa wakati wa uongozi wa Ismail Aden Rage na Etoile ikautumia mwanya huo kuanza kuizungusha Simba.

Rage aliahidi Etoile wangelipa wakati akiwa madarakani, kabla hajaondoka, lakini haikuwa hivyo.

Zigo likamuangukia yeye kwa kuwa ndiye aliidhinisha Okwi kwenda Etoile hata kabla ya Waarabu hao kulipa, kabla ya kumgeuka.

Etoile walizidi kusumbua baada ya Okwi kurejea Uganda na baadaye Yanga, hali iliyofanya Simba kukata tama.

Taarifa zinaeleza barua ya agizo hilo, tayari imetua TFF ambayo imewasilisha kwa Rais wa Simba, Evans Aveva kwamba anatakiwa kupokea mzigo pamoja na faini hiyo ndani ya mwezi mmoja.

Tayari Okwi ameisharejea Simba akitokea Yanga, hivyo Simba itafaidika kuwa na mchezaji halafu na mkwanja juu.

SalehJembe BLOG
 
Hii ni baada ya CAS kuiamuru Etoile Du Sahel kuilipa Simba Sc USD 300,000. Kiasi hicho kilikuwa ni kwa ajili ya uhamisho wa Okwi. Simba Sc iliamua kwenda CAS baada ya Etoile du Sahel kugoma kulipa ada ya uhamisho ikidai kua ina hali mbaya kiuchumi.

NB: "zaidi ya usd 300,000 + mkwanja wa mtani jembe + vyanzo vyetu vya mapato = Simba Sc Complex mitaa ya Bunju"

Hapo kwenye red ni hadithi za kusadikika
 
Hata 1m US$ haifiki eti Simba kapakatwa sijui complex my foot

Mkuu mbona una wivu hivyo?? Kipindi tunaenda kufyeka nyasi Bunju, si kwamba tulikua tunapoteza mda. Kuna fungu maalumu kwa ajili ya uwanja. Hilo fungu, ukichanganya na hayo hapo juu kwanini tusimalize ujenzi wa Simba Sc Complex?? It's a matter of time.
 
stroke hawa kandambili wanatakiwa wakae kimya tu.. kandambili mnatakiwa kujua kua ukiacha hizo usd 300,000 pia tunatakiwa tulipwe gharama za usumbufu, ambapo mkwanja unaweza ukapaa hata zaidi ya usd 350,000.
 
Last edited by a moderator:
Kwenu ni za kusadikika, maana maamuzi ya kandambili yanategemea na Mhindi kaamkaje.

Ni Kweli Kabisa, Uwanja Wa Bunju Umekamilika Ndio Maana Unatumika Kwa Mazoezi!
 
Kama tumempa Mkude 80m kwa ajili ya usajili, tambwe na kwizera zaidi ya 40m ili kuvunja mikataba yao kipindi hicho tuliwapa zaidi ya 60m kina sserunkuma ili kuziba gap la kina tambwe, tutashindwaje kuongezea above 400m ili kukamilisha Simba Sc Complex????
 
Mkuu mbona una wivu hivyo?? Kipindi tunaenda kufyeka nyasi Bunju, si kwamba tulikua tunapoteza mda. Kuna fungu maalumu kwa ajili ya uwanja. Hilo fungu, ukichanganya na hayo hapo juu kwanini tusimalize ujenzi wa Simba Sc Complex?? It's a matter of time.
mkuu hiyo km inakuja kweli


tegemea kuingia kwenye mifuko ya watu,kurwa na doto bado hawajapata viongozi wenye nia ya kweli ya kimaendeleo,wengi wako pale kwa maslahi yao tu,juzi kati kuna viongozi wa simba wameingiza kontena 3 za jezi za simba,jaribu kuuliza km ni za mradi wa smba au wa viongozi
 
Hii ni baada ya CAS kuiamuru Etoile Du Sahel kuilipa Simba Sc USD 300,000. Kiasi hicho kilikuwa ni kwa ajili ya uhamisho wa Okwi. Simba Sc iliamua kwenda CAS baada ya Etoile du Sahel kugoma kulipa ada ya uhamisho ikidai kua ina hali mbaya kiuchumi.

NB: "zaidi ya usd 300,000 + mkwanja wa mtani jembe + vyanzo vyetu vya mapato = Simba Sc Complex mitaa ya Bunju"

Subiri utakachoambiwa na kina Aveva na Kasim Dewji. Watakuambia hizo pesa wala hazitoshi kulipa madeni ya klabu. Watakuambia kuwa hata hao wachezaji wanaosajiliwa ni kwa fedha za mkopo kutoka kwa hao wanaojiita wafadhili au friends of simba na sio kutoka klabuni.
 
mkuu hiyo km inakuja kweli


tegemea kuingia kwenye mifuko ya watu,kurwa na doto bado hawajapata viongozi wenye nia ya kweli ya kimaendeleo,wengi wako pale kwa maslahi yao tu,juzi kati kuna viongozi wa simba wameingiza kontena 3 za jezi za simba,jaribu kuuliza km ni za mradi wa smba au wa viongozi

Mkuu upigaji upo kila kona na si katka Simba Sc tu, na kuzuia ni ngumu sana maana system nzima ya nchi imeganzishwa.
 
Kama tumempa Mkude 80m kwa ajili ya usajili, tambwe na kwizera zaidi ya 40m ili kuvunja mikataba yao kipindi hicho tuliwapa zaidi ya 60m kina sserunkuma ili kuziba gap la kina tambwe, tutashindwaje kuongezea above 400m ili kukamilisha Simba Sc Complex????

sembo acha masikhara!! mmefyeka uwanja halafu hadi Leo hamna kitu!!

yesu atawahi kurudi kabla ya simba au Yanga kumiliki complex kama chamazi

huo ndo ukweli na moyoni mwako unalijua hilo.
 
Hii ni baada ya CAS kuiamuru Etoile Du Sahel kuilipa Simba Sc USD 300,000. Kiasi hicho kilikuwa ni kwa ajili ya uhamisho wa Okwi. Simba Sc iliamua kwenda CAS baada ya Etoile du Sahel kugoma kulipa ada ya uhamisho ikidai kua ina hali mbaya kiuchumi.

NB: "zaidi ya usd 300,000 + mkwanja wa mtani jembe + vyanzo vyetu vya mapato = Simba Sc Complex mitaa ya Bunju"

Hiyo pesa haifiki hata TZS 1bn/= wewe unazungumzia kujenga uwanja! Heri kuwa kipofu wa macho kuliko kuwa kipofu wa akili (ujinga).
 
Back
Top Bottom