Figo zimefeli ghafa umri miaka 37

mtindo wa maisha kwa sasa ni hatari
unatumia chakula chenye sukari au mafuta mengi asubuhi
unatumia chakula chenye chumvi nyingi mchana na kinywaji cha sukari nyingi
unatumia chakula cha chumvi nyingi na kinywaji cha sukari ya kutosha jioni

wakati huo huo wenzako wahadzabe na ndugu yao dr janabi wanawinda siku nzima jasho kila kona kula mara moja tu jioni, habari za presha na kufeli viungo hawazijui, wote tutakufa lakini kuna watu watakufa kifo cha mende.
 
Poleni sana
Mgonjwa anaendeleaje?

Mungu awape uponyaji.
 
Sababu zinaweza kuwa ni POISONING. bila yeye mwenyewe binafsi kujua kama amekuwa Poisoned.

Kuna kila sababu hapa nimuite mtaalamu ili aje atoe somo kuhusiana na suala hili.

"Unconventional Methods of Inflicting Harm Upon Another Person."
 
Kwa maisha ya sasa ni vizuri kuwa na blood pressure machines majumbani watu wengi wana tatizo la pressure ila hawajui , ni vizuri kucheki atleast once a week inaokoa mambo mengi sana ukijua mapema na kuanza kutumia dawa, stroke na figo husababishwa na highblood pressure mara nyingi
 
Ukijua mapema anza dozi upo sahihi mkuu
 
Ndiyo; high blood pressure husababisha uharibifu wa figo na viungo vingine nyeti vya mwili.

Kusema kuwa hajawahi kuugua pressure siyo kweli, kwani high blood pressure siyo ugonjwa, na mara nyingi pressure inaweza kuwa iko juu sana wakati mtu mwenyewe hajui. Ndiyo maana umekuwa unasikia watu wanaanguka ghafla na kufariki kwa sababu ya stroke. Labda kama alikuwa anapima pressure kila siku na kujiaminisha kuwa kweli hana high blood pressure; bila vipimo huwezi kusema hajawahi kuwa na pressure. Kama amefikia figo kuharibika, maana yake ni kuwa amekuwa nayo kwa muda mrefu sana.

Kutibu figo zilizoharibika ni ama transplant ya kuwekewa figo kutoka kwa mtu mwingine au dialysis. Tiba zote ni ngumu sana

Pole sana kwa dhahama hii iliyoingia kwenye familia yako
 
On point
 
Serikali kupitia taasisi za afya, wafanye utafiti wa kina kuhusu suala hili la ugonjwa wa figo.
Wasione aibu wala kusita, kama kuna vyakula, mfumo wa maisha au baadhi ya vinywaji vinasababisha huo ugonjwa vipigwe marufuku na elimu iendelee kutolewa kwa wananchi juu ya tabia hatarishi kwa afya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…