Nimeuliza hii kwa manufaa ya watu wote. Wakati mabenki yakiendelea kutangaza kupata faida, bado yamekuwa yakiongeza riba, gharama za ATM withdraw, transfer, deposit, nk. Ni ukweli usiopingika kuwa inapotokea unapokopa kwenye mabenki yetu kama mfanyabiashara au mfanyakazi, hesabu zinaonyesha utarudisha kati ya asilimia 40 - 60 zaidi ya kile ulichokopa. Percentage hii inategemea muda wa kulipa deni husika na kiwango pia. Nataka wenye utaalamu watueleze sheia ya fedha inasemaje juu ya asilimia ya jumla atakayorejesha mkopaji (riba) baada ya kuchukua kiasi fulani cha fedha?
Je sheria inasemaje ama iko kimya hivyo kuyapa mabenki kufanya maamuzi kwa kadri wanavyojisikia? Naomba tuliweke hili wazi ili liweze kuamsha majadiliano na pengine mabadiliko. Na hii inaweza pia kuleta changamoto wakati huu ambao tunafikiria kuwa na morgage act. Kwa nchi za wenzetu (zilizoendelea) riba wakati mwingine haifiki hata 5%.
Je sheria inasemaje ama iko kimya hivyo kuyapa mabenki kufanya maamuzi kwa kadri wanavyojisikia? Naomba tuliweke hili wazi ili liweze kuamsha majadiliano na pengine mabadiliko. Na hii inaweza pia kuleta changamoto wakati huu ambao tunafikiria kuwa na morgage act. Kwa nchi za wenzetu (zilizoendelea) riba wakati mwingine haifiki hata 5%.