Fisadi Asababisha kigugumizi kwa Kikwete.

Fisadi Asababisha kigugumizi kwa Kikwete.

Indume Yene

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
2,962
Reaction score
721
Katika hali isiyotegemewa, Rais Jakaya Kikwete amekumbwa na kigugumizi cha utoaji vyeti kwa wale waliosaidia kuchangia ununuzi wa pikipiki kwa makada wa SISIEMU. Fisadi huyo ni Japhet Lema anayejulikana zaidi kwa jina la NJAKE.

Pikipiki hizo zenye thamani ya millioni 24.5 zilikuwa zigaiwe kwa Makatibu wa Chama wilayani Arusha. Mgeni wa heshima katika utoaji huo Rais Kikwete alichezwa na machale ya kuzigawa hizo pikipiki pamoja na vyeti baada ya kugundua kuwa Fisadi Njake ni mmoja wa wadhamini waliochangia ununuzi huo. Hivyo aliutupa huo mpira kwa viongozi wa chama hicho wilayani ili waweze kujigawia.

Hata hivyo danadana ilianza baada ya viongozi wa wilaya nao kuanza kurushiana mpira.

Hii inatia aibu sana, kwa nini Mwenyekiti wa SISIEMU(T) ambaye ni Rais wa JMT asiamuru kurudishwa kwa fedha alizotoa fisadi kununua hizo pikipiki badala ya kurushiana mpira? Bado hizo pikipiki zitatumiwa na SISIEMU, kwa hiyo JK kuruka viunzi na kuchomoa kugawa pikipiki kwa makada wake bado hakuleti unafuu wowote. Hizo ni baadhi ya pesa za wizi zilizonunua hizo pikipiki kwa ajili ya usafiri wa makada wa SISIEMU.
 
Jakya kukataa kugawa hizo pikipiki hakuwaondolei sifa hawa CCM kuwa ni mafisadi; mbona walipokea shilingi milioni 400 kufadhili mkutano wa vijana mchana kweupe zilizotolewa ma fasadi Somaia ambaye tunajua fika kuwa alihusika na kutuibia kwenye dili ya radar!! Huu wote ni usanii wa muungwana.
 
Jakya kukataa kugawa hizo pikipiki hakuwaondolei sifa hawa CCM kuwa ni mafisadi; mbona walipokea shilingi milioni 400 kufadhili mkutano wa vijana mchana kweupe zilizotolewa ma fasadi Somaia ambaye tunajua fika kuwa alihusika na kutuibia kwenye dili ya radar!! Huu wote ni usanii wa muungwana.

Labda JK hakujua kipindi hicho kuwa Somaia ni fisadi vilevile kwa njia moja au nyingine. Zitawatokea matakoni tu muda ukifika. Wananchi bado wanaendelea na ANALYSIS zao.
 
Jakya kukataa kugawa hizo pikipiki hakuwaondolei sifa hawa CCM kuwa ni mafisadi; mbona walipokea shilingi milioni 400 kufadhili mkutano wa vijana mchana kweupe zilizotolewa ma fasadi Somaia ambaye tunajua fika kuwa alihusika na kutuibia kwenye dili ya radar!! Huu wote ni usanii wa muungwana.

Ndiyo maana nasema tuzidi kuwapigia kelele hawa mafisadi. Kelele zetu baada ya JK kupokea shs. 400,000,000/-, zimemfanya aogope kupokea hizo piki piki - si picha zingepigwa ? Kidogo kidogo tutafika na aibu zao zitawafanya angalau wawe waoga lakini kamwe hauwasafishi kwenye ufisadi - huo ni mfumo wa maisha ndani ya CCM.
 
wandugu,

..hizo pikipiki zimetolewa na mafisadi ambao hawako kundi moja na Raisi Kikwete.

..zingetolewa na wale mafisadi wanaomuunga mkono basi angetoa baraka zake na kuzikabidhi kwa wanachama.

..Sophia Simba amechaguliwa kwa kutumia rushwa ya fedha za mafisadi walioko ktk kundi la Raisi Kikwete. hiyo ndiyo sababu iliyomfanya Raisi aivumilie rushwa ktk uchaguzi wa mwenyekiti wa UWT.

NB:

..ukitaka ufanikiwe ktk masuala ya ufisadi inabidi uwe ktk kundi linamuunga mkono Raisi Kikwete ndani ya CCM.

..kujifanyia ufisadi kivyako-vyako kama Mramba,Yona,na Mgonja, is too risky these days.
 
Back
Top Bottom