TEAM 666
JF-Expert Member
- Dec 7, 2017
- 4,399
- 8,594
KHERI NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI . Haikua bahati tu , bali ni neema ya siku ya jumapili ya tarehe 5 ya September 1993 kwenye uzao wako mtukufu , haikua baraka ya jiji la Bujumbura tu , bali nchi nzima ya burundi ilinufaika na ujio wako duniani.
Nyota ilianza kung'aa mapema sana , tangu ulipopata mafunzo ya soka pale Lydia Ludic Burundi Academy , tangu hapo kila mrundi alijipiga kifua kwa kujua utalisaidia taifa hapo baadae.
Haikua ajizi kwako , kiwango chako kilikusafirisha nchi nyingi , Halitasahaulika goli lako moja kunako Mamelodi soundows ya Afrika kusini.
Ni nani asiye enzi mchango wako pale Luanda Angola knako Desportivo de agosto . Ipo haja ya kuvikwa kilemba cha uhodari kwa kazi uliyoifanya kule Al Zawraa nchini Iraq , kote ulitembeza soka safi.
Waarabu wa Misri na Algeria watabaki na jina lako tu , uliwafundisha jinsi ya kucheza kama striker wa kisasa . Naomba nikueleze tu , Wananchi wana imani kubwa na wewe , Hakuna anayetia doa rekodi zako ulizoweka barani Afrika , haikua rahisi kwako kufunga magoli 16 kwenye mechi 20 za timu ya taifa , ni nani aliyewaza kuwa utamzidi Mo salah kwa magoli kule Afcon .
Ni nani asiyejua ulikua sawa na ODIO IGHALO wa man U ?. Inatosha kuelezea ubora wako , karibu timu ya wananchi , wawekezaji pia ni wananchi , hawa ni watu wenye hamasa kubwa sana , wakitaka jambo lao liwe na linakua
. Karibu kwenye jangwa lenye neema na baraka , jangwa lisilo na njaa , jangwa safi.
Wananchi wanataka uwape ladha ya Amisi Tambwe kwenye mchuzi wa Donald Ngoma, wape Tamu za Sunday Manara kwenye icecream yako.
Na ukifanya hivyo , jina lako litakua na utukufu mara mbili ya sasa.
Busara za ndugu yako Ntibazonkiza zikufikishe kwenye ukuu wa jina lako kwakua mnafahamiana na mtacheza soka safi .
Fiston naomba nikung'ate sikio tu , wananchi wanahitaji magoli , kama hutojaaliwa kuwapa vyote ulivyonavyo , basi wape kwa uchache na usiwanyime vyote.
Rekodi zako zimeingia kwenye vichwa vya wananchi , nenda kaziongeze kwa kugongelea misumari ya magoli Ni kheri uwape nusu ya furaha kuliko kuwanyima kabisa .
Chonde usije zifuta . Kila la kheri striker.
Nyota ilianza kung'aa mapema sana , tangu ulipopata mafunzo ya soka pale Lydia Ludic Burundi Academy , tangu hapo kila mrundi alijipiga kifua kwa kujua utalisaidia taifa hapo baadae.
Haikua ajizi kwako , kiwango chako kilikusafirisha nchi nyingi , Halitasahaulika goli lako moja kunako Mamelodi soundows ya Afrika kusini.
Ni nani asiye enzi mchango wako pale Luanda Angola knako Desportivo de agosto . Ipo haja ya kuvikwa kilemba cha uhodari kwa kazi uliyoifanya kule Al Zawraa nchini Iraq , kote ulitembeza soka safi.
Waarabu wa Misri na Algeria watabaki na jina lako tu , uliwafundisha jinsi ya kucheza kama striker wa kisasa . Naomba nikueleze tu , Wananchi wana imani kubwa na wewe , Hakuna anayetia doa rekodi zako ulizoweka barani Afrika , haikua rahisi kwako kufunga magoli 16 kwenye mechi 20 za timu ya taifa , ni nani aliyewaza kuwa utamzidi Mo salah kwa magoli kule Afcon .
Ni nani asiyejua ulikua sawa na ODIO IGHALO wa man U ?. Inatosha kuelezea ubora wako , karibu timu ya wananchi , wawekezaji pia ni wananchi , hawa ni watu wenye hamasa kubwa sana , wakitaka jambo lao liwe na linakua
. Karibu kwenye jangwa lenye neema na baraka , jangwa lisilo na njaa , jangwa safi.
Wananchi wanataka uwape ladha ya Amisi Tambwe kwenye mchuzi wa Donald Ngoma, wape Tamu za Sunday Manara kwenye icecream yako.
Na ukifanya hivyo , jina lako litakua na utukufu mara mbili ya sasa.
Busara za ndugu yako Ntibazonkiza zikufikishe kwenye ukuu wa jina lako kwakua mnafahamiana na mtacheza soka safi .
Fiston naomba nikung'ate sikio tu , wananchi wanahitaji magoli , kama hutojaaliwa kuwapa vyote ulivyonavyo , basi wape kwa uchache na usiwanyime vyote.
Rekodi zako zimeingia kwenye vichwa vya wananchi , nenda kaziongeze kwa kugongelea misumari ya magoli Ni kheri uwape nusu ya furaha kuliko kuwanyima kabisa .
Chonde usije zifuta . Kila la kheri striker.