Flora Mbasha, amekimbilia mahakama ya hakimu mkazi Kisutu

Flora Mbasha, amekimbilia mahakama ya hakimu mkazi Kisutu

Aliyataka menyewe na akijua tamaa ni dhambi ya MAUTI
 
Mkuu upo sahihi lakini ktk kupata maana kamili ya Wokovu lazima usome maandiko mengi kuhusu wokovu ili kuelewa Mungu anamaanisha nini kuhusu wokovu......kila mstari wa biblia wafaa kwa mafunzo lakini ukisimama na mstari mmoja wowote bila kusoma vizuri na mingine unaweza kufikiri tofauti.
Nakubaliana na wewe Mkuu MTAZAMO. Maandiko yanajaziliana yenyewe kwa yenyewe. Ipo mistari inayojisimamia na ipo inayohitaji mingine kuleta maana kusudiwa. Ipo mingine inayohitaji ukasome mingine ili ufate uchambuzi wa maneno yaliokuwa refered kwenye mstari wa kwanza. n.k
kwa mfano Yesu mwenyewe alisema wote watakaoamini lazima wabatizwe ili wawe "candidate" wa ufalme wa Mungu
Hapo lazima mtu aelewe kuamini ni nini na kubatizwa ni nini, lakini kanisa la leo naona wengi wanachukulia maneno at face value.. lakini kila neno ukilichunguza utakuta kuna mahali limedadavuliwa. Kwa mfano Mtu akiamini (IMANI) maandiko yanayonena khs imani yanasemaje: nakumbuka maandiko machache khs Imani
1. Imani ni kuwa na hakika na mabo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana ......
2. Pasipo Imani, Mtu hawezi kumpendeza Mungu...
3. Mwenye haki ataishi kwa IMANI....
4. Imani pasipo matendo ni kazi bure....
5. Kwa Imani, Ibrahimu alifanywa kuwa rafiki wa Mungu.....
6. Mimi (Yesu) ndiye ufufuo na uzima, Mtu AKINIAMINI mimi hata akifa ataishi....na yeyote anayeishi akiniamini hatakufa kamwe
7. .......Hata akamtoa mwanaye Ili kila AMUAMINIYE asipotee bali awe na uzima wa milele.

TAFAKARI: Yatosha tu mtu kusema namwamini Mungu/Yesu Kristo baasi akaendelea na maisha ya uzinifu, wizi, ulevi, uongo, uasherati, n.k? hapa sasa ndipo mtu anatakiwa kwenda mbele zaidi kujua Maana ya kuamini/Matendo/tabia zinazoambatana na ukiri wake etc.

na kwa maandiko hayo kutoka kwa warumi 10:10-9 basi ungeweza kusema imani yatosha......lakini Yesu alisema imani bila matendo imekufa......je maandiko yamepingana?
Nimejaribu kurefer maandiko hapo juu juu ya imani, Kama nilivyosema Maandiko yanajaziliziana yenyewe kwa yenyewe, kipindi na kipindi, nyakati na nyakati. Ila hayapingani. Kuna maandiko huwezi ukasimamia mstari mmoja bila kuhusianisha na mwingine ili ilete maana timilifu.

Nashukuru sana Mkuu kwa ufafanuzi wako. Tuko pamoja na tunakubaliana kimsingi.
 
Last edited by a moderator:
Mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha, amekimbilia mahakama ya hakimu mkazi kisutu, akiomba kuvunja ndoa kati yake na mumewe, Emmanuel Mbasha. Flora anadai sababu za kuomba kuvunja ndoa hiyo apewe talaka ni kutokana na tabia ya mumewe kumpiga, kumnyanyasa na kushindwa kumpatia matibabu.
Una lipi la kuwaambia wanandoa hawa?
Huyu ana matatizo ya akili coz yeye badala ya kwenda kwa mchungaji aliyewafungishia ndoa yeye anakimbilia Mahakamani. Ameshajiona ni tatizo mbele ya kanisa na ndio sababu hataki kurudi kwa kanisa.
 
Nakubaliana na wewe Mkuu MTAZAMO. Maandiko yanajaziliana yenyewe kwa yenyewe. Ipo mistari inayojisimamia na ipo inayohitaji mingine kuleta maana kusudiwa. Ipo mingine inayohitaji ukasome mingine ili ufate uchambuzi wa maneno yaliokuwa refered kwenye mstari wa kwanza. n.k

Hapo lazima mtu aelewe kuamini ni nini na kubatizwa ni nini, lakini kanisa la leo naona wengi wanachukulia maneno at face value.. lakini kila neno ukilichunguza utakuta kuna mahali limedadavuliwa. Kwa mfano Mtu akiamini (IMANI) maandiko yanayonena khs imani yanasemaje: nakumbuka maandiko machache khs Imani
1. Imani ni kuwa na hakika na mabo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana ......
2. Pasipo Imani, Mtu hawezi kumpendeza Mungu...
3. Mwenye haki ataishi kwa IMANI....
4. Imani pasipo matendo ni kazi bure....
5. Kwa Imani, Ibrahimu alifanywa kuwa rafiki wa Mungu.....
6. Mimi (Yesu) ndiye ufufuo na uzima, Mtu AKINIAMINI mimi hata akifa ataishi....na yeyote anayeishi akiniamini hatakufa kamwe
7. .......Hata akamtoa mwanaye Ili kila AMUAMINIYE asipotee bali awe na uzima wa milele.

TAFAKARI: Yatosha tu mtu kusema namwamini Mungu/Yesu Kristo baasi akaendelea na maisha ya uzinifu, wizi, ulevi, uongo, uasherati, n.k? hapa sasa ndipo mtu anatakiwa kwenda mbele zaidi kujua Maana ya kuamini/Matendo/tabia zinazoambatana na ukiri wake etc.


Nimejaribu kurefer maandiko hapo juu juu ya imani, Kama nilivyosema Maandiko yanajaziliziana yenyewe kwa yenyewe, kipindi na kipindi, nyakati na nyakati. Ila hayapingani. Kuna maandiko huwezi ukasimamia mstari mmoja bila kuhusianisha na mwingine ili ilete maana timilifu.

Nashukuru sana Mkuu kwa ufafanuzi wako. Tuko pamoja na tunakubaliana kimsingi.

Umefafanua kwa uzuri sana............sina hata nukta ya kuongeza .......
 
Umesahau kuwa ndoa ni mktaba wa kisheria? Kwa kuwa kisheria ni mkataba basi usishangae yeye kuomba kibali cha Mahakama ili kutengua huo Mkataba.

Pili, inaonekana kuna mchanganyiko wa hoja hapa,lkn kama ni kwelu Flora anadai talaka, Kibiblia siamini kama amefanya dhambi ili mradi aishi kama mtu ambaye hajaolewa [ asishiriki mambo ya kindoa].

Vv

Samahani kiongozi, unaweza nisaidia reference ya hayo maandiko yanayozungumzia ulikokisema hapo? Asante

Navyofahamu (I stand to be corrected and assisted):
Mtu akimwacha mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati, Akienda kuoa au huyo mke akiolewa, atakuwa anafanya uzinzi. (Mathayo 19: 3-11). Kwa nini iwe tu uasheraji, Tendo la ndoa lina implications gani kati ya mtu mke na mume?. kwa nini Yesu aliruhusu hilo? n.k n.k... haya ni mambo ambayo wakristo wengi wanayaogopa kuyasemea kwa maana kama Yesu alivyosema Asiye na dhambi awe wa kwanza kumpiga yule mwanamke mzinzi Jiwe... Vivyo hivyo asiye muasherati awe wa kwanza kumshitaki mwenzake mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.. maana anayo hio haki... Vinginevyo watubu, waache ujinga wao na wakae kimya milele.

Mungu wetu ni Mungu wa maagano, na anaheshimu sana mapatato/maagano. Agano mojawapo ni ndoa inayounganishwa na tendo la ndoa. Na kwa kuwa hakuna agano lisilokuwa na damu, Mungu aliweka ubikira kulithibitisha agano kati ya mtu mke na mume. n.k (hii ni mada ndefu tuiache kwa sasa)
 
Pamoja sana Kaka Mkubwa MTAZAMO . Nimejifunza kitu kutoka kwako. Asante sana kwa uchambuzi na hekima zako. Uwe na sikukuu njema sana pamoja na familia yako na woote uwapendao.
Umefafanua kwa uzuri sana............sina hata nukta ya kuongeza .......
 
Last edited by a moderator:
Wanapeana BP tuu, ataki mwenzie basi, ampe talaka Yake maisha ya songe...

Kwenye ukristo hakuna talaka,na kama mkiachana kwa sababu ya uzinzi yule atayekutana na yule mwanamke aaliyeachwa atakuwa amezini nae..ndio maandiko yanavyosema ambayo hao walikula kiapo kuyalinda katika ndoa yao...
 
Nashukuru sana Mkuu Otorong'ong'o kwa ufafanuzi wako yakinifu. Tuko pamoja sana.

Nakubaliana na wewe, Yesu alikuja kuwaokoa watu na Dhambi na madhara ya dhambi kwa mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele.

Kwa hiyo cha kwanza tunaokolewa kutoka kwenye dambi na madhara yake yanayoambatana na mtu akiwa hai na baadha ya maisha ya hapa. Kwamba kuna uzima wa milele na jehanamu/Ziwa la moto/ moto wa na mateso ya milele aliyoandaliwa yule malaika muasi anayeshawishi wanadamu ili wakateseke pamoja. Kwa hio kuokoka kwa kwanza ni dhidi ya dhambi na concequences zake hapa duniani na pili ni kuokoka na hukumu ya milele. Yohana 5:24 ''Ninawaambia hakika, ye yote anayesikiliza maneno yangu na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Amevuka kutoka kwenye mauti, na kuingia katika uzima''

Na anaposema atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokoka ni kwamba zawadi ya mshindi haitolewi mwanzoni wala katikati, inatolewa mwishoni wa mbio. . Ili kuokoka na hukumu ya milele yampasa mwanadamu amalize vyema mbio zake ili akaipate ile taji ya uzima. Ndio maana Paulo akasema sijihesabii kama nimekwisha kufika au kuwa mkamilifu, bali nakaza mwendo ili niifikie mede ya Thawabu ya mwito mkuu wa Mungu...

Nakushukuru sana mkuu kwa hekima na busara zako. Tuko pamoja sana. Kazi imeanza ilioko mbele ni ngumu zaidi.. tuzidi kukua kiroho na kimatendo.
Shem Khantwe huku huwa huji eeh!!

Mkuu MTAZAMO na Tized naomba kuchangia hapa kidogo maana naona mimi na wewe tized tunataka kwenda mabali..

Tuangali maana ya kuokoka katika Agano la Kale..
Kuokoka ni kutokana na maovu mbalimabali: Vita njaa, magonjwa, kifo, hukumu na mambo kama ayo..

HAPO NI aGANO LA kALE...
jE! aGANO JIPYA LINASEMAJE

Agano jipya linaendeleza maana ileile ya kuokoka kama ilivyo Agano la kale (Luka 1:74; 2Timoth 4:18) Lakini Agano Jipya linatilia mkazo juu ya Kuokoka kuwa tendo la kuondolewa dhambi....Na hivyo inasemwa Yesu alikuja kuwaokoka watu na dhambi zao...(Mt. 2:21) Mungu ndiye aliyechukua hatua ya kuwaokoa watu
Hivyo unatakiwa kutubu zambi na Kumwamini Yesu kuwa ni Mwokozi...(Rum 10:9)
Ila kubatizwa na kukiri bado hakutoshi...Kazi bado jaijaisha..Ndo kwanza safari imeanza
 
Last edited by a moderator:
Samahani kiongozi, unaweza nisaidia reference ya hayo maandiko yanayozungumzia ulikokisema hapo? Asante

Navyofahamu (I stand to be corrected and assisted):
Mtu akimwacha mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati, Akienda kuoa au huyo mke akiolewa, atakuwa anafanya uzinzi. (Mathayo 19: 3-11). Kwa nini iwe tu uasheraji, Tendo la ndoa lina implications gani kati ya mtu mke na mume?. kwa nini Yesu aliruhusu hilo? n.k n.k... haya ni mambo ambayo wakristo wengi wanayaogopa kuyasemea kwa maana kama Yesu alivyosema Asiye na dhambi awe wa kwanza kumpiga yule mwanamke mzinzi Jiwe... Vivyo hivyo asiye muasherati awe wa kwanza kumshitaki mwenzake mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.. maana anayo hio haki... Vinginevyo watubu, waache ujinga wao na wakae kimya milele.

Mungu wetu ni Mungu wa maagano, na anaheshimu sana mapatato/maagano. Agano mojawapo ni ndoa inayounganishwa na tendo la ndoa. Na kwa kuwa hakuna agano lisilokuwa na damu, Mungu aliweka ubikira kulithibitisha agano kati ya mtu mke na mume. n.k (hii ni mada ndefu tuiache kwa sasa)

Mkuu hapo kwenye Mathayo 19:9 debate yake kwa Scripture scholar ni ya muda mrefu sana ........hata mimi binafsi naamini hapo Yesu hakuweka loop hole ya talaka maana maandiko mengine yote yanaonesha jinsi Mungu anavyochukizwa na talaka ........nadhani huu mstari ukibebwa kama ulivyo kwa lugha iliyotumika inaleta utata ........kule kwenye Catholics answers kuna haka kakipande mdau mmoja amejibu hivi...........

What may appear as a loophole is a consequence of misinterpretation or mistranslation. The King James Version and others translate the passage into English words that appear to say fornication, unchastity, or adultery are exceptions that allow a divorce.
The constant teaching of the Church has been that a valid sacramental marriage can not be broken, even if one party sins. As Matthew 19:6 says, "Therefore, what God has joined together, no human being must separate." Biblical scholars, such as J. Bonsirven, have pointed out that the Greek word that is pivotal here is "porneia," which means unlawful sexual intercourse.

The Gospel does not use the Greek word "moicheia," which is the ordinary Greek word for adultery.
The intent appears to be to distinguish a true marriage from concubinage. What is being said is that if a man and a woman are in fact married, the bond is inseparable. But if they are not married, just "living together," then there is no lawful marriage and there can be a separation or annulment. The wording of the New American Bible for Matthew 19:9 is a translation that gives us this sense.
 
Hapo hajatafuta suluhisho kaahirisha matatizo.
 
Hahahaha shem Tized huwa nakuja ila sema kuna binadamu wana midomo michafu sana siwezagi mimi kujadiliana nao nachagua kupita kimyakimya
 
Last edited by a moderator:
Asante sana kwa hilo andiko Mkuu MTAZAMO. Kati ya maswala yenye mkanganyiko mkubwa ni swala hili.

Tukianza na uchambuzi wa huyu ndugu hapo niliko bold inabidi tena tukayachunguze maandiko kwamba ndoa inaanzia wapi? kuishi pamoja au inaanzia kanisani au inaanzia mtu yeyote mke na mtu mume wanapokutana? au watu wawili wanapokubaliana, na je tunaposema wanakuwa mwili mmoja, ni kimwili au kiroho? Na je? Mmoja wapo anapoenda kulala na mwanaume au mwanamke mwingine, kimwili na kiroho kunatokea nini? na hayo yanayotokea yaweza kutengenezwa au kurekebishwa na nini? n.k n.k.....
Tukishafahamu muunganiko uliko wa mtu mume na mtu mke, ndio twaweza anza kujua kuvunjika kwa huo muunganiko kunatokea wapi na kwa weza sababishwa na nini.

Mfano katika kiapo cha ndoa makanisani kuna sehemu wanasema ... nitakua WAKO na Nitakuwa mwaminifu kwako hadi kifo kitakapo tutenganisha.....(Je kutokuwa mwamininifu madhara yake ni nini? Ni kifo au kupoteza nafasi au uhalali wake kama mke au mume?...

Kwa maana tunamuona Adamu akiambiwa na Mungu akila tunda alilokatazwa HAKIKA ATAKUFA... lakini hatuoni akifa kimwili bali tunaona akifa kiroho (positionally) kwanza kutoka chini ya Mungu hadi kuwa chini ya shetani.. then vingine vikafuatia kufukuzwa na kadhalika) sijui kama nitaelewka vizuri hapa.. mniwie radhi (Adam ndio alikua anatawala dunia lakini baada ya dhambi tunaona maandiko yakimsema Shetani kama Mtawala(controller) wa dunia, Mungu wa dunia hii, Mkuu wa ulimwengu
n.k nafasi ambayo ilikua kwa Adamu .... uzuri ni kwamba baada ya Yesu kuja, Adamu wa pili hawi tena chini ya Mungu bali anatawala pamoja na Mungu.

Kwa hio mtu mume anavyotoka nje ya agano/patano kufanya uasherati, anapoteza uhalali au nafasi yake kiroho kama mume au mke. hatukioni japo tunawaona wakiishi ila spiritually they are disjoined/dis connected.

Unasemaje hapo mkuu? nini maoni yako!! Naona mjadala unazidi kuwa mgumu aisee!!! ukisoma hilo andiko Yesu alilokua akiwajibu wale majamaa kuhusu talaka unaona nini?

Many thanks

Mkuu hapo kwenye Mathayo 19:9 debate yake kwa Scripture scholar ni ya muda mrefu sana ........hata mimi binafsi naamini hapo Yesu hakuweka loop hole ya talaka maana maandiko mengine yote yanaonesha jinsi Mungu anavyochukizwa na talaka ........nadhani huu mstari ukibebwa kama ulivyo kwa lugha iliyotumika inaleta utata ........kule kwenye Catholics answers kuna haka kakipande mdau mmoja amejibu hivi...........

What may appear as a loophole is a consequence of misinterpretation or mistranslation. The King James Version and others translate the passage into English words that appear to say fornication, unchastity, or adultery are exceptions that allow a divorce.
The constant teaching of the Church has been that a valid sacramental marriage can not be broken, even if one party sins. As Matthew 19:6 says, "Therefore, what God has joined together, no human being must separate." Biblical scholars, such as J. Bonsirven, have pointed out that the Greek word that is pivotal here is "porneia," which means unlawful sexual intercourse.

The Gospel does not use the Greek word "moicheia," which is the ordinary Greek word for adultery.
The intent appears to be to distinguish a true marriage from concubinage. What is being said is that if a man and a woman are in fact married, the bond is inseparable. But if they are not married, just "living together," then there is no lawful marriage and there can be a separation or annulment. The wording of the New American Bible for Matthew 19:9 is a translation that gives us this sense.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom