jimmyfoxxgongo
JF-Expert Member
- Jan 23, 2013
- 5,352
- 9,329
kwani nisipo oa kabisa kuna nini kitatokeaAcha uoga wa maisha wewe,dawa sio kuahirsha,unatakiwa uyaingie maisha mapema,unataka kuoa ukiwa na miaka 45?
Biblia inasisitiza sana kusameheana na inasema asiye samehe wengine bila kujali aina ya kosa, basi hata yeye Mungu hatamsamehe mtu huyo.
Kuhusu kisa cha hawa wawili, Flora ndiye aliye mwacha Emma, wakati ule Emma alimbembeleza sana Flora wasahau tofauti zao warudi waishi kwenye ndoa yao lakini Flora alikataaa kata kata hata kumtia aibu mumewe. Wakati huo Flora alikuwa anahatia mbele za Mungu kwa kuvunja ndoa na kukataa msamaha wa mumewe.
maana biblia inasema mtu akikosa hata saba
mara sabini kwa siku akija na kuomba msamaha, msamehe.
Baada ya kesi kwisha, Flora alimtaka mume wake amsamehe warudiane, kakini Emma alikataa katakata. Hivyo hatia ikageuka kwa Emma.
Kwa sababu hiyo Flora amehesabiwa haki kwa sababu aliomba msamaha kabla Emma hajaoa lakini Emma alikataa, kibiblia hata Mungu hajamsamehe Emma dhambi zake kwa kukataa kumsamehe Flora. hivyo Emma anahesabiwa kama mdhambi tu aliye amua kumwacha mkewe.
Hivyo Flora aliye tubu anapata uhalali wa kuolewa kwa neno linalosema:- yeye asiye amini akitaka kuondoka na aondoke, ndipo huyo ndugu mume au mke yu huru.
Kwa sasa Flora yuko huru
kuolewa kwa sababu Emma kamwacha kwa kukataa kumsamehe pale Flora alipoomba Emma amsamehe warudiane.
Emma atabaki na hatia.
Biblia inasema heri kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa. Flora bado kijana sana. Hana hatia kabisa mwacheni aolewe amtumikie Mungu vizuri.
HAPPY WEDDING FLORA.
Mathayo 5:32, Mathayo 19:9 1Wakorintho 7:15.Nafahamu kwenye Biblia inaeleza ndoa inaweza kuvunjika kama
Mmoja wapo alifanya uzinzi nje ya ndoa. Pili endapo mtu anataka kukutoa kwenye Imani hebu tafuteni hio mistari.
Hilo la uzinzi nimelisikia kwao.Hebu someni maandiko vizuri najua alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe isipokua kifo au uzinzi so ukithibitisha mwezako anachepuka talaka tu ingawa Mungu haipendi kwakua hapendi kuachana.
Mtumishi wa Mungu si binadamu?Mi nadhani anahukumiwa kutokana na yeye kuaminika kama mtumishi wa Mungu kumbe la! Sidhani kama angekuwa mwanamke wa kawaida ingekuwa issue..
Utaonekana bazazi au sio mwanamke mkamilifu tuKw
kwani nisipo oa kabisa kuna nini kitatokea
Utaonekana bazazi au sio mwanamke mkamilifu tuKw
kwani nisipo oa kabisa kuna nini kitatokea
mbona siwaelewi hapa:Mwache aolewe, hana mume, maana kifo kilishawatenga, kwa hiyo yuko huru.
Kibiblia huyo Daudi, haitajiwi kumwoa flora, mpaka mbasha Mungu amchukue!!
Ahya bhana!!
Kama wewe Ni Mwanaume Jitahidi kutomuamini Mwanamke maana mwanamke Hachelewi kukusaliti ni Matumaini Yangu Flora alimwambiaga Mume wake Kwamba Kifo Ndio Kingewatenganisha lakini sasa Hicho hakikuwatenganisha...nA Leo anaolewa tena....Wanaume Jifunzeni kitu Hapo i know wanaume tuna tamaa hata ikitokea tukasaliti wapenz au wake zetu ni kwa tamaa za wakati huo tyu bali yale mapenzi ya dhati yanakuwa Bado yapo kwa wenzi wetu tofautu na mwanamke akichepuka ndo keshapenda mrengo wa kushoto na wewe huna chako tena hapo Na huwa nachekaga sana Pale nikikumbuka yule binti Nilimpendaga akaniambiaga Kwamba mimi na wewe hatutoachana Milele lakini leo hata salamu Hakuna......Anyway Nmamtakia Flora Bahati Njema!Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Madame Flora (Flora Mbasha zamani), Jumapili ya wiki ijayo anatarajia kufunga ndoa na mume wake mtarajiwa Daudi Kusekwa katika bustani za hoteli ya Rock Beach jijini Mwanza.
Madame Flora ameliambia Swaggaz kuwa ndoa hiyo itaambatana na uzinduzi wa albamu yake mpya inayoitwa Wakati Wake pamoja na kitabu alichokipachika jina la Siri za Flora Mbasha.
“Ndoa itafungwa asubuhi na jioni kutakuwa na sherehe ya harusi, utambulisho wa albamu yangu mpya pamoja na kitabu, watu wote wanakaribishwa kadi zimebaki chache tu kutokana na idadi ya ambayo imepangwa na kamati,” alisema Flora.
Chanzo. Mtanzania
Kweli aisee...Flora MUNGU anakuona
Mbona wana fanana hawa jamaa
Mkuu hebu tupe sheria za ndoa zinasemajeKweli machangudoa wapo kila sehemu, Kumbe hata waimba nyimbo za enjili nao ni wahuni kiasi hili? Hivi hao wanaokwenda kumsikiliza Frola wanaupako sawa sawa? Tangu lini NDOA iliyofungwa kanisani ikavunjwa na mahakama na bado ukenda olewa tena?
Tafsiri ya haraka, ikiwa mume atamtaliki mke kwa sababu nyingine yoyote, asioe tena kwa kuwa atakuwa anadhini. Mke aliye achika naye akiolewa, basi huyo aliyemuoa anadhini. Hapa haijamzungumzia mwanamke. Lakini, ikiwa amemtariki kwa sababu za uzinifu, mume anaweza kuoa tena.Kwenye Biblia ya Kiingereza imendikwa hivi; " And I say to you, whoever divorces his wife, except for sexual immorality, and marries another, commits adultery; and whoever marries her who is divorced commits adultery "