KERO Foleni ya magari Mizani Mikumi ni kero kubwa, mbona haipati ‘solution’ au kuna watu wananufaika?

KERO Foleni ya magari Mizani Mikumi ni kero kubwa, mbona haipati ‘solution’ au kuna watu wananufaika?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Bado Hujasema

Member
Joined
Dec 1, 2024
Posts
12
Reaction score
14
Sisi Wakazi wa Mikumi Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro tuna kero ya muda mrefu ya foleni ya magari makubwa ya mizigo katika Mizani ya Mikumi, hali ambayo inatufanya kuhofia kutokea kwa ajali katika eneo hilo.

Foleni hiyo inatokana utaratibu wa askari wakati wa ukaguzi wa magari hayo mpaka tunahofia kuwepo kwa viashiria vya rushwa, kwanini eneo hilo magari yakae muda mrefu maana inaleta kero kwa watumiaji wengine wa barabara kama magari madogo, bajaji, pikipiki mpaka kwa watembea kwa miguu.

Kibaya zaidi kuna sehemu ya kupaki hayo malori ambayo ni jirani kabisa na mizani hiyo, kwanini magari yasiwe yanatoka kwa utaratibu na mpangilio ili foleni isiwepo au kuna kitu nyuma ya pazia ambacho sisi hatukijui.

Unakuta mtu mwenye gari dogo anakaa saa kadhaa au alazimishe kupita, la sivyo mtu kama si mzoefu au mgeni wa eneo hilo hawezi kupita pale.

Tunaomba mamlaka husika zitupie jicho eneo hilo ili foleni ma mkusanyiko wa magari upungue kama si kuisha kabisa iwe pawe salama kwa watumiaji wa barabara hiyo.

Siku kutakuja kutokea ajali kubwa sana halafu Serikali ije itupiwe lawama wakati uwezekano wa watu kufanyakazi yao wapo au watu kulifanyia kazi wanaweza askari wanaokagua eneo hilo wafanye kazi yao kuondoa foleni na mkusanyika wa magari katika eneo hilo.

IMG-20250107-WA0003.jpg
IMG-20250107-WA0009.jpg
IMG-20250107-WA0013.jpg
IMG-20250107-WA0013.jpg
 

Attachments

  • IMG-20250107-WA0005.jpg
    IMG-20250107-WA0005.jpg
    444.9 KB · Views: 3
  • IMG-20250107-WA0011.jpg
    IMG-20250107-WA0011.jpg
    386.7 KB · Views: 4
  • IMG-20250107-WA0007.jpg
    IMG-20250107-WA0007.jpg
    386.2 KB · Views: 2
  • IMG-20250107-WA0015.jpg
    IMG-20250107-WA0015.jpg
    390 KB · Views: 3
Ni mizani inayoongoza kuwa namsululu mkubwa w magari hasa malori something ipo au siyo.
 
Sisi Wakazi wa Mikumi Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro tuna kero ya muda mrefu ya foleni ya magari makubwa ya mizigo katika mizani ya Mikumi, hali ambayo inatufanya kuhofia kutokea kwa ajali katika eneo hilo.

Foleni hiyo inatokana utaratibu wa askari wakati wa ukaguzi wa magari hayo mpaka tunahofia kuwepo kwa viashiria vya rushwa, kwanini eneo hilo magari yakae muda mrefu maana inaleta kero kwa watumiaji wengine wa barabara kama magari madogo, bajaji, pikipiki mpaka kwa watembea kwa miguu.

Kibaya zaidi kuna sehemu ya kupaki hayo malori ambayo ni jirani kabisa na mizani hiyo, kwanini magari yasiwe yanatoka kwa utaratibu na mpangilio ili foleni isiwepo au kuna kitu nyuma ya pazia ambacho sisi hatukijui.

Unakuta mtu mwenye gari dogo anakaa saa kadhaa au alazimishe kupita, la sivyo mtu kama si mzoefu au mgeni wa eneo hilo hawezi kupita pale.

Tunaomba mamlaka husika zitupie jicho eneo hilo ili foleni ma mkusanyiko wa magari upungue kama si kuisha kabisa iwe pawe salama kwa watumiaji wa barabara hiyo.

Siku kutakuja kutokea ajali kubwa sana halafu Serikali ije itupiwe lawama wakati uwezekano wa watu kufanyakazi yao wapo au watu kulifanyia kazi wanaweza askari wanaokagua eneo hilo wafanye kazi yao kuondoa foleni na mkusanyika wa magari katika eneo hilo.

View attachment 3194685View attachment 3194688View attachment 3194690View attachment 3194690
Iyo foleni igeuzeni kuwa fursa mnaoishi jirani na barabara au maeneo hayo, Mungu awape nini sasa!! Aisee,


Wauzieni maji,kuku wa kukaanga,matunda,hao abiria na madereva qb,m
 
Back
Top Bottom