Mkuu Sandeni, ingawa kuna waliokunanga kwa ushauri wako. Mi nitatofautiana naomba nikupongeze umeeleza jambo la msingi sana, mfano Rwanda wana program mahususi kwa wanafunzi wanaomaliza chuo, kwamba ni lazima afanye na kufaulu driving test. Hii ipo pia USA ambapo baadhi ya majimbo karibu yote mtoto wa umri wa kuanzia 14-21 lazima ajifunze na kufaulu driving.
Ingawa kuna uangalizi kwa wenye age ya 14-16,21 in some states all newly licensed adult drivers may be or obation for a set amount of time (usually between six months and two years). Kwetu nimeona mfumo mpya wa upatikanaji licence ukizigawa katika madaraja kutikana na umri, chombo au mitambo.
Ni nini faida za kuwa na ujuzi huu, kwanza ni kuattend dharura yoyote itakayo jitokeza katika mazingira yatakayo kulazimu kuendesha chombo. Hii itakupunguzia gharama za undeshaji wako maisha badala ya kuajiri mtu utakae mlipa ingawa hili hutegemea pia title ya mtu na taratibu zilizopo katika maeneo yake.
Mfano jaji wa mahakama kuu hawaruhusiwi wawapo kazini kujiendesha, na kuna title nyingi ambazo utahitaji msaidizi wa kazi hiyo. Tatu unaweza kupata neema ya kuwa gari yako maana sisi wengi kuwa na gari ni hatua kubwa ambayo wengi wetu tunaitamani., au tuikwepa mfano kuna ambao ununuzi wa gari kabla ya ujenzi kwao ni upuuzi. Na misemo juu .."ooh hakuna baba mwenye gari ni baba mwenye nyumba" na mingine kama hiyo.
Nne kuwa na ujuzi wa udereva kunapanua wigo wako wa ajira (kwa wanaofukuzia ajira) hata kama huna gari wewe binafsi lakini utaweza kujiendesha kwa gari ya mahali ulipoajiriwa.