foreign investors VS local investors

mama dunia

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2011
Posts
420
Reaction score
84
Yaani jana nilikuwa natizama citizen tv ya kenya, Raila Odinga akifungua kiwanda kipya cha bia huko mombasa, sasa nilijisikia kutahayari pale aliposema 'namkoti' kwa kiswahili, "Nchi yoyote haiwezi kuendelea kwa kutegemea wawekezaji wa nje" akimaanisha kuwa wawekezaji wa ndani ndo mambo yote.... kweli nilitahayari kwakuwa mie hapa bongo nimezoea kusikia kila kukicha kuwa wawekezaji hao wa nje ndo wanaoleta maendeleo nchini, na wamekuwa wakija na kualikwa na kutembelewa kila sikuuuu... sasa sielewi lipi ni lipi
 
Ukweli ndohuo muwekezaji wa nje haleti maendeleo makubwa nchini na pesa zote azipato haziachi hapa anatoa lakini muwekezaji wa ndani ataziacha hapapohapo na ataongeza miradi ingine ndani ya nchi
 

Si kila anayekuja kwa jina la mwekezaji wa nje anamaanisha,wengine ni wezi tu wa kawaida. Tabia ya 10% inawabeba sana. Kusema ukweli wawekezaji wa ndani ni bora mara mia kuliko hao wa kigeni,japokuwa kuna asilimia fulani kwa upande wa tekinolojia ktk maeneo fulani tunawahitaji.
 
Kenya ndio nchi ya kwanza kwa afrika kwa mwananchi wake kuanzisha kiwanda cha beer kinachoitwa keroche breweries,,,ni mwanamke,na alipewa loan ya zaidi ya millioni 500 ya kenya kufungua branch nyingine
 
ni kweli we fikiria sababu tu za hawa wageni kuja kuwekeza tanzania , unafikiri hawapendi kutoa ajira kwawatu wao , kama ilivyotokea kwamba viwanda vya nguo vinaenda asia kwa ajili ya cheap labour, wanakuja kwetu kwa ajili ya rasilimali na si kutusaidia inasikitisha sana kwamba ukisema neno MUWEKEZAJI kwa tanzania mara nyingi inaonekana ni mgeni
 
Anaitwa tabitha karanja,na raila odinga aliweka foundation kwa ajili ya ujenzi wa 2.5bill plant ambapo kiwanda kikiisha kitakuwa na uwezo wa kuzalisha chupa 600,000 kwa siku hiki cha sa hv kinazalisha chupa 60,000 kwa siku.nilishasoma historia ya huyo mama,mume wake alikuwa agent wa kampuni ya bia,biashara ikawachosha wakataka waende beyond ndo wakaanzia kutengeneza spirits(pombe kali),mume wake sa hv ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi,ilhaali wyf wake ndo managing director
 
ohh ok nimeelewa wajameni, basi inabidi kuwe na mifumo ya kuwawezesha wawekezaji wa ndani zaidi ili kuleta haya maendeleo, maana katika nchii hii kila mahala ni ma-foreign investors tu ukimtoa wa kwetu bakhresa hahahahaha
 
Na upuuzi wenyewe unaanzia pale airport. Wageni hawasumbuliwi wala kuulizwa maswali ya kijinga, lakini ukiwa na passport y kibongo basi miswali ya kijinga kibao. eti mara "ooh unafanya nini huko nje?" Mbona umebeba miswaki miwili? Mbona una viatu vingi?
Wawekezaji wengi wamekuja ku-loot. wapo wawekezaji wageni ambao wako poa, lakini ni wachache
 
Wakuu Tatizo liko kwa Wabongo wenyewe na si kwa hao wawekezaji, pamoja na Rushwa tukubali hawa wazungu wan mitaji mukubwa sana ukilinganisha na wazawa,

Wazawa kama wangeacha ubinafisi na kuunganisha Nguvu tungeweza kupambana na wazungu na kuwashinda, chukulia mfano wa Supermarket za Shoprite, watanzania walikuwa na uwezo wa kushindana na hawa makubulu lakini tatizo kila mmoja anataka awe na ki minsupermarket chake sasa hii wapi na wapi?

Njoo kwa kampuni za Ujenzi, Makandarasi wakibongo kama wangeweza kuungana na hata makandarasi 20 na kuwa na kampuni moja nina uhakika wangeweza kushindana na wachina na watu wengine, tatizo kila mmoja anataka aonekane anaweza na ana kampuni

Kama watanzania hawataunganisha nguvu tutabakia kulalamika tu, leo MZUZU nataka watu wakufanya nae kazi, najua watu wengi wataona ni bora wange kuwa pekee yao, so ni lazima tunao lalamika tuonyeshe mfano

So mnao lalamika pls anazeni kwa kuonyesha mfano wa kuunganisha nguvu na kuja na kampuni moja ya kueleweka na si kuwa na utitili wa kampuni
 
wawekezaji wapo wengi tu hapa e.g ipp, metl, azam, au ni bia ndo ishu?
 

Tatizo lenu mnapenda sana kulalamika watanzania linapokuja suala la maendeleo yenu, wewe unasema watu waungane kwenye kufanya biashara sababu ni zipi za kuungana ujaelezea, zaidi ya kuseama hili kupambana na wageni?

Na assume ni kwenye kutaka kuunganisha capital that is the most logic reason i can think of, hili waweze wekeza vizuri na kuwa na vifaa vya kupambana na hao wageni. Either way (including if my assumption is wrong), wewe huwezi sema watu waungane bila ya kujua implication za parterships na pengine ndio sababu wengine wanaona heri ya kuwa pekeyao.

Na huwezi kumlaumu mgeni kuwekeza kwenye soko lako (kwa sababu anaongeza ajira ambazo otherwise zisingekuwepo), ingawa it is not an ideal scenario in terms of benefiting with those profits and also it opens the doors for tax evasions (kutokana na miuondo ya hizi kampuni, kama watu wanaweza wasilipe ushuru nchi ambazo zipo alerted kama za europe sidhani kama watashindwa TZ).

Lakini tatizo ni financial institutions zilizopo ndani na government policies zilizopo kwenye kui-encourage uwekezaji wa ndani. At the end of the day people need money to turn their bright ideas into reality, where is that money going to come from within Tanzania au labda utuambie risk investors waliopo ambao wanaweza toa mikopo on ideas.

Vinginevyo amna jinsi kwa sasa zaidi ya kutegemea wawekezaji wa nje unless serikali itenge hizo fedha na isaidie watu wenye mawazo ya kuwekeza kwa faida ya taifa or else watakuja tu watu wenye hela zao toka nje kuwekeza, muwalaumu tu bila ya sababu sahihi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…