0.25% shule' 99.75% juhud zang.... Na hapo ndipo nilipo angukia. Sijachoka nimeinuka na safari yangu nataka iendelee hadi nifike nitakapo. Ushauri wenu ndio dira yangu! Namimi ndio nitachagua wapi pakuelekea.
Nashukur kaka
Kama juhudi zako zilikua 99.75% basi naweza kusema hii asilimia ujaitendea haki, maana kwa alama ulizozipata, inadhihilisha kuna makosa ulikua unayafanya. Fanya ujifanyie tathmini halafu uyajue makosa yako kwanza, bila ya hivyo sidhani kama utabadili hali. Hizi ni baadhi ya sababu ambazo nadhani baadhi yake ungetakiwa kujibu swali uliloulizwa na mmoja wa wachangiaji.
1)Kwa uzoefu wangu, watu wa namna kama yako wenda mnasoma sana lakini hamuelewi, na hili hamligundui mpaka mnapofeli.
2)Sababu nyingine mnakua mnasoma matango pori, yani mambo ambayo kimsingi hayapo kwenye mtaala, na mnakua heti na mtazamo wa kujiweka tayari zaidi kwa mitihani, kumbe huwa aina ulazima hiyo mitango pori.
3)Pia watu wa namna kama yako huwa hamna mazoea ya kufanya mitihani kwenye vituo mbalimbali kwa lengo la kujifanyia tathmini, huwa mnajiamini kupita kiasi kuwa mko vizuri, mwisho wa siku NECTA inawapakata.
4)Huwa mnasubiri walimu wawaletee kila kitu, wawahamasishe msome na mengine mengi kupitia walimu, hayo ndio matokeo yake.
5)Huwa hamna tamaduni na desturi ya kujadili na wenzenu juu ya mustakabali wenu mnapo kuwa shule, kujadili kuhusu masomo, past papers n.k
6)Huwa hamna ukaribu na wanafunzi wa shule zingine, hapa naongelea mahusiano yako na wanafunzi wa shule nyingine, lakini haswa katika masomo, mnapokuwa na mahusiano mazuri kimasomo na shule zingine, inakupa fursa ya kujua yanayoendelea huko, ambayo kimsingi yanakusaidia katika ufaulu wako.
7)Huwa hampendi kusikiliza maono, ushauri, mwongozo na maelekezo kutoka kwa waliowazidi, wenda kielimu au kiumri, huwa mnamisimamo na mawazo yenu hata kama mawazo hayo sio sahihi.
8)Huwa hamna vipaumbele mnapokuwa shule, hii inawafanya mnafanya mambo mengi kwa wakati mfupi na mwisho wa siku yanatokea haya, wanafunzi wengi mnatamani kujua kila kitu mnapokuwa O-level, sasa usipotenga muda wa kutosha katika kujisomea na kufanya mazoezi mbalimbali, basi lazima hile kwako, huwezi kuendesha elimu huku kulia kwako kuna club, mademu na tungi. Kushoto kwako kuna facebook, twiter,skype, whats up na bbm. Nyuma kuna kazi za nyumbani na changamoto zingine za kifamilia. Mbele kuna NECTA, kazi yake kubwa ni kufanya assessment ya yale yote mliojifunza mnapokuwa shule, kama mmeelewa au lah.
Kati ya hizo sababu nilizo ziorodhesha hapo juu, wewe jiangalie na ujifananishe na kila sababu moja moja hapo, halafu ufikie hitimisho ni kipi haswa kimekufanya uangukie pua.