Forodhani Zanzibar

Mohammed Salum

New Member
Joined
Jul 23, 2022
Posts
1
Reaction score
4

Moja ya maeneo yanayokusanya watu wengi, hasa nyakati za jioni visiwani Zanzibar, ni Forodhani Garden, ukubwa wake si zaidi ya kilomita moja za mraba, lakini hubeba melfu ya wageni wa ndani na wa nje ya Tanzania.

Upekee wa bustani hii ni uwepo wa vyakula vya aina mbalimbali, vikiwemo vya asili. Hapa ni kama kioo cha uso wa Zanzibar na taswira ya visiwa hivi eneo lililo kando ya bahari na linalotazama majumba ya asili ya mji mkongwe…

Kutokana na umuhimu wake, haikushangaza kutumika kwa karibu dola milioni 3 mwaka 2009 kuboresha eneo hili kukidhi matakwa ya kitalii bila kuathiri, asili yake.

Asubuhi na mapema ukifika eneo hili liko kimya kiasi, kwenye viti vya kupumzikia, utakuta watu wachache wamejipumzisha na wengine kusoma vitabu, kusikiliza muziki kwenye simu.

Ni eneo la maarufu pia kwa watu wanaotaka kutafakari wakihitaji utulivu nyakati za asubuhi, lakini nyakati za alasiri eneo hili linakuwa na shughuli nyingi zaidi za biashara ya chakula cha mtaani, pengine kuliko maeneo yote ya Zanzibar na mengi ya Tanzania.

Kwa Wazanzibari eneo hili ni mali na linawakilisha utamaduni wao, kwa wageni eneo hili ni burudani na starehe.
 
Umesahau kuitaja Beit Al Ajaib, kuwa kwa sasa, inachafua madhari ya Forodhani baada ya kubomoka kutokana na uzembe...
 
Nafikiri Halmashauri ya Kigamboni ingetenga eneo na kulifanya kuwa Kama bustani ya Forodhani pia kuwe na maeneo ya kupumzika.Wanasubiri Kigamboni ijae pomoni Kuna maeneo huko pembamnazi,Kimbiji,Puna hadi Buyuni.Wikiend mtu atoke Vingunguti akavute hewa Safi na kupunguza stress huko.
 
Ila wale vijana wanaojiita Beach Boys huwa wanatia aibu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…