Four cylinder Vs six cylinder

Four cylinder Vs six cylinder

Hiyo ni kweli kabisa ndio maana injini ya 3s ya rav 4 au Noah sr40 ukiangalia ulaji wake wa mafuta hautofautiani sana na injini ya 1G ya GX 100 au GX 110 ya mark 2 lakini watu wengi hawalijui hilo ila wanachoangalia ni six tuu
ebu fafanua vizuri mkuu.
 
Six cylinder ina nguvu sana na inakimbia kukiko 4 cylinder! Na six cylinder inakunywa mafuta madogo kiasi ukilinganisha na 4 cylinder.
Tengeneza scenario vzuri mkuu, sijakupata unachomaanisha
 
Siyo nadra, hilo halipo!!! Huwezi kukuta gari mbili zenye idadi tofauti ya cylinder lakini CC ni sawa!! Hivi vipimo viko standard!!
kwann usikute ...suzuki 2nd generation kuna 2000cc v6 na third generation kuna 2000cc i4 ....
 
Nahisi unataka kuelewa jambo fulani muhimu sana ila ambalo ni pana na linachanganya kwa kiasi fulani kwa sababu ufafanuzi wake unahusisha vitu vingi vya mfumo wa injini. mbaya zaidi nahisi swali lako hujaliweka vizuri kutosha kueleweka unachotaka kutofautishiwa.

hata hivyo mm ntajifanya ulikuwa unaulizia hivyo vitu kwenye gari.
4 cylinder ni tofauti na 6 cylinder kwa upande wa nguvu ya gari pia matumizi ya mafuta.

kwanza fahamu kuwa cylinder ni mtungi unaopokea mafuta na kuyachoma ili yaweze kutengeneza nguvu ya kusukuma gari. mtungi huu una kitu kiitwacho pistoni kilichozama ndani yake na kina uwezo wa kuingia ndani na kutoka mithili ya pampu ya baiskeli unapojaza upepo tairi. pistoni hupanda na kushuka ndani ya cylinder, wakati pistoni inapanda huruhusu mafuta kuingia ndani ya cyinder na wakati inashuka hukandamiza na kuunguza mafuta yaliyoingia ambayo hutengeneza nguvu ya kusukuma gari. zoezi hili hurudia rudia kwa haraka sana na ndipo gari hutembea.

kujibu swaki lako
Ukisikia 4cylinder maana yake kuna mitungi minne ya kuchoma mafuta kwa wakati mmoja.. na 6 cylinder maana yake mitungi sita ya kuchoma kwa wakati mmoja...

1. ikiwa kila cylinder ina ujazo sawa wa lita 0.5 kwenye injini ya cylinder 4 basi kwa mpigo mmoja kila cyinder ya injini itachoma mafuta hivyo cylinder 4 zitachoma o.5 * 4= 2litre (2000cc)
japo kuna vitu vingine lkn kiwango cha mafuta yanayochomwa kwa mpigo mmoja huchangia kuamua nguvu ya gari.

ikiwa hiyo gari ya 6cylinder pia kila cylinder ina ujazo wa lita 0.5 inamaana kwa mpigo mmoja mafuta yanayochomwa ni 0.5*6= 3Litre (3000cc).

kwa hesabu hizo maana yake gar ya 4cylinder itakula mafuta kidogo kuliko ya ile ya 6cylinder, pia ya 4cylinder itakuwa na nguvu kidogo kuliko ya 6cylinder

2. sasa ili gari zenye idadi tofauti ya cylinder zile kiwango sawa cha mafuta itakuwa namna hii
Ikiwa injini ya 4cylinder inkula cc 2000 maana yake kila cylinder inabugia 500cc yaani cylinder moja ina ujazo wa 500cc tu, na kwa kadri vyilinder inavyoweza kuchoma mafuta mengi kwa pamoja ndivyo gari inavyokuwa sio na nguvu tu bali pia kasi japo kuna vigezo vingine vya kuamua.

ikiwa injini ya 6cyilinder inakula cc 2000 pia maana yake kila cylinder inabugia 333.3cc yaani cylinder moja ina ujazo wa 333.3cc tu. hivyo kwenye mpigo mmoja kila cylinder inachoma mafuta kidogo kuliko inavyofanyika kwenye injini ya cylinder 4. hivyo gari hii itakuwa na nguvu ndogo kuliko hiyo ya cylinder 4 japo itakuwa na uwezo wa kukimbia zaidi kuliko hiyo ya cylinder 4.

Kumbuka: nahisi ni nadra sana kukuta gari yenye cylinder nyingi kuwa na cc sawa na gari yenye cylinder chache. Mara nyingi kama sio zote gari ya cylinder nyingi huwa ina cc kubwa pia.
Na engine ya 3s au 5L sjui, ni nn hivi vitu au ndo cylinder zenyewe??

VVTI nayo inatajwa sana na wanunuzi, tuwekane sawa ni kitu gan?
 
good pia six mara zote huwa haitoi muungurumo mkubwa km four na hii inachangiwa na kuwa na cyrinder nyingi zaidi ya gari zenye four. chukulia mfano pikipiki yenye piston moja au mashine ya disel yenye piston zilivyo na kelele
Kwa maana hiyo treni labda haina cylinder kabisa....mbona inakelele nyingii [emoji23][emoji23][emoji23]
 
V6 Haitoi mlio kivipi mkuu, wakati hizo engine ndio huwa zina mshindo mkali mno kuliko v4. Mfano mlio wa gx100/110 ukilinganisha na mlio wa corrolla limited?
v4 v6 ....hizo "v' zinamaanisha ni idadi ya piston au?
 
Na hapa ndipo penye hoja ya fuel consumption na sio idadi tu ya cylinders bali pamoja na ukubwa wa hizo cylinders na technology inayotumika katika generation ya nishati kuzungusha crank shaft.
Ukubwa wa cylinder nao tunaujuaje sasa wakat wa kuchagua gari? Au tuseme cylinder ndogo kabisa na kubwa kabisa vipimo vyake vinasomekaje kama unajua mkuu
 
v4 v6 ....hizo "v' zinamaanisha ni idadi ya piston au?
V ni mpangilio wa piston katika cylinder block.

Actually hamna mpangilio wa V kwa piston 4. Isipokuwa kuna kwa piston 6 zilizo na mpangilio wa v
 
Kaka nakubaliana na wewe, ILA tofauti ipo, ujazo ni sawa ila kama huyo wa Cylinder Sita atatumia masaa 2 kumaliza, huyo wa pili atatumia masaa mawili na nusu kumaliza mafuta yote. Kadri ya masaa yatakavyo kuwa mengi ndivyo umbali unaweza kuongezeka kabla ya kuongeza mafuta na hapo ndipo linapokuja swala la kuwa gari halili mafuta mengi maana unaagalia urefu wa route dhidi ya mafuta yaliyitumika. So kimsingi kila kitu kiko sawa kiujazo ila kuyamaliza kwa haraka huo ndiyo ulaji wenyewe.
Mkuu nimekuelewa sana, otherwise mleta mada atuambie piston zinatofautiana ukubwa
 
Injini ya gari langu ni 5.7L V8, kwa hiyo ninasoma 2000 cc cylinder 6 ninakuwa kama siamini ninachosoma, kwani nafikiri 2000 cc ni kama lita mbili tu. Kwa injini kama hiyo kuwa na cylinder sita ina maana itakuwa na vipistoni vidogo sana katika karne hii, hivyo sehemu ya energy inapotea bure kukabiliana na friction baina ya moving parts.
5.7L hii inamaanisha nn kitaalam
 
Hizi nondo safi sana kwa kupata japo basics knowledge ya magari..hongera mtoa post..ngoja tuchimbe kdg na sisi!
 
Ukubwa wa cylinder nao tunaujuaje sasa wakat wa kuchagua gari? Au tuseme cylinder ndogo kabisa na kubwa kabisa vipimo vyake vinasomekaje kama unajua mkuu
Ukubwa wa cylinder unapimwa kwa cubic centimeter (cc) ikiwa ni diameter ya bore ama kipenyo cha kinu husika kinachokabili mshindo wa cylinder katika mchakato wa kuchoma mafuta.

Kila cylinder ina mzunguko wa kupanda na kushuka katika kinu chake mithili ya mtu anavyotwanga kisamvu kwenye kinu isipokuwa tu cylinder inakuwa iko direct proportional na kinu chake kwa vipimo so its almost inagusa kingo za kinu haichi nafasi pembeni.

Sasa ishu ya cc ndio hasa inadetermine ukubwa wa cylinders. Kivipi?
Mfano gari inayoandikwa V6 with 3.5L ina maana hii gari ina cylinders 6 zenye jumla ya cc 3500 zilizo katika mpangilio wa V kwa maana tatu zimelala kulia na tatu zilizobaki zimelala kushoto katika angle ambayo zikipishana zinatengeneza umbile la herufi V.

Katika hizo cc 3500 kila cylinder bore inabeba kiasi flani cha mafuta. Ili kupata namba kamili utachukua 3500 gawanya 6 kisha utapata kiwango cha mafuta ambacho kila cylinder bore inabeba. Hesabu itakupa ni kama cc 583.3 kwa cylinder moja.
 
Mkuu comment yako, na profile picture vinaendana.
Huyo kuzungumzia gari wewe umeruka kwenye ndege, wakati wowote utarukia kwenye meli.
Jaribu kuangalia kwa kina hiki kitu. Resonance in relation to number of piston with a consideration of fuel consumption .
Kabla ya kukua kwa technology tulikuwa na kitu kinaitwa governor ambayo ilikuwa mechanical. Ilikuwa inatumia proposional principal, ie unapofungua mafuta na ndivyo yatakavyolika.
Baada ya kukua kwa technology tukapata, proposional +derivatives governor, ie hata ufungulie mafuta hadi mwisho, mafuta yatatumika kulingana na mzigo, na hata ukibania mafuta unajisubmbua kwani engine itakosa nguvu
Baadae technology ikazidi kupanuka, tukapata proposional +derivatives +intergral governor. Hii imefuata kanuni ifuatayo, ukubwa wa pua si wingi wa makamasi. Ie unaweza kuta engine ina v12, lkn ulaji wake ukawa sawa na 6cylinder. How? Ni rahisi.
Sio kwa kuwa umetengeneza choo basi kila wakati ukajisaidie, no. Utaenda chooni pale utakapobanwa.
V12 on normal loads sio piston zote 12 will be supplied with fuel, may be 6 of them.
How do they achieve comfotability? Minimization of resonance, na ndio maana zipo kimya.
Kanuni ya hapo juu in applying only ktk magari.

Mkumbuke consumption inavyo hesabiwa.
Consumption kwenye barabara = power of engine xload x conditions of load x time ÷ distance covered.
Ile consumption ilioandikwa kwenye gari ni bench tested results. Ni engine imewekwa juu ya bench ikawashwa.
Wakora
Very professional,nice.
 
Ukubwa wa cylinder unapimwa kwa cubic centimeter (cc) ikiwa ni diameter ya bore ama kipenyo cha kinu husika kinachokabili mshindo wa cylinder katika mchakato wa kuchoma mafuta.

Kila cylinder ina mzunguko wa kupanda na kushuka katika kinu chake mithili ya mtu anavyotwanga kisamvu kwenye kinu isipokuwa tu cylinder inakuwa iko direct proportional na kinu chake kwa vipimo so its almost inagusa kingo za kinu haichi nafasi pembeni.

Sasa ishu ya cc ndio hasa inadetermine ukubwa wa cylinders. Kivipi?
Mfano gari inayoandikwa V6 with 3.5L ina maana hii gari ina cylinders 6 zenye jumla ya cc 3500 zilizo katika mpangilio wa V kwa maana tatu zimelala kulia na tatu zilizobaki zimelala kushoto katika angle ambayo zikipishana zinatengeneza umbile la herufi V.

Katika hizo cc 3500 kila cylinder bore inabeba kiasi flani cha mafuta. Ili kupata namba kamili utachukua 3500 gawanya 6 kisha utapata kiwango cha mafuta ambacho kila cylinder bore inabeba. Hesabu itakupa ni kama cc 583.3 kwa cylinder moja.
Hii nimeielewa kabisa. Inamana gari zenye cc sawa ila idadi ya cylinder tofauti inamana yenye cylinder chache itakua ina nguvu kubwa, speed ndogo na tutegemee kwamba kwenye safar ndefu itakunywa sana mafuta coz itatumia muda mrefu kufika but inafaa kwa safar fupi za mjin
 
Hivyo kama zote zina cc zinazolingana basi ile ya 4 cylinder itakuwa na inachoma mafuta mengi kwa kila piston moja ukilinganisha na piston ya 6 cylinder.

Cylinder 4 mafuta mengi kwa kila piston lakini ina piston chache. Kwa hiyo bado hakuna conclusion engine ipi itatumia mafuta mengi zaidi.
 
Hii nimeielewa kabisa. Inamana gari zenye cc sawa ila idadi ya cylinder tofauti inamana yenye cylinder chache itakua ina nguvu kubwa, speed ndogo na tutegemee kwamba kwenye safar ndefu itakunywa sana mafuta coz itatumia muda mrefu kufika but inafaa kwa safar fupi za mjin
Hewala, gari ikiwa na cylinder chache inatumia nguvu sana kwenye kupata speed kubwa hivyo mafuta mengi yatalika ili kuipata speed kubwa tofauti na gari yenye cylinder nyingi hivyo haifai sana kwa matumizi ya mwendokasi.

Pia gari yenye cylinder kubwa haitatumia nguvu sana kupata speed kubwa/kuchanganya na hivyo haitakula mafuta mengi ikiwa kwenye speed tofauti na yenye piston chache. Hivyo ina ufanisi zaidi kwenye speed kubwa zaidi kuliko kwa uendeshaji wa speed ndogo.
 
Mkuu comment yako, na profile picture vinaendana.
Huyo kuzungumzia gari wewe umeruka kwenye ndege, wakati wowote utarukia kwenye meli.
Jaribu kuangalia kwa kina hiki kitu. Resonance in relation to number of piston with a consideration of fuel consumption .
Kabla ya kukua kwa technology tulikuwa na kitu kinaitwa governor ambayo ilikuwa mechanical. Ilikuwa inatumia proposional principal, ie unapofungua mafuta na ndivyo yatakavyolika.
Baada ya kukua kwa technology tukapata, proposional +derivatives governor, ie hata ufungulie mafuta hadi mwisho, mafuta yatatumika kulingana na mzigo, na hata ukibania mafuta unajisubmbua kwani engine itakosa nguvu
Baadae technology ikazidi kupanuka, tukapata proposional +derivatives +intergral governor. Hii imefuata kanuni ifuatayo, ukubwa wa pua si wingi wa makamasi. Ie unaweza kuta engine ina v12, lkn ulaji wake ukawa sawa na 6cylinder. How? Ni rahisi.
Sio kwa kuwa umetengeneza choo basi kila wakati ukajisaidie, no. Utaenda chooni pale utakapobanwa.
V12 on normal loads sio piston zote 12 will be supplied with fuel, may be 6 of them.
How do they achieve comfotability? Minimization of resonance, na ndio maana zipo kimya.
Kanuni ya hapo juu in applying only ktk magari.

Mkumbuke consumption inavyo hesabiwa.
Consumption kwenye barabara = power of engine xload x conditions of load x time ÷ distance covered.
Ile consumption ilioandikwa kwenye gari ni bench tested results. Ni engine imewekwa juu ya bench ikawashwa.
Wakora
cumins!!!
 
Back
Top Bottom