Fred Ngajiro aka Fred Vunjabei ni nani huyu jamaa?!

Hakuna chakula cha maskini au tajiri. Wote tunakula hivyo, ila sema maskini anaeza akala kidogo, asikiunge, n.k. Kwa mfano mimi bila kula ugali sina raha. Hicho ndicho chakula nilichozoea. Kwa hiyo kula ugali si umaskini. Mpare kula kande si umaskini wala ubahili. Mchagga/Mhaya kula ndizi ni jadi wala siyo umaskini au utajiri. Mimi kwa mfano sipendi maraharage. Hii sio kwa sababu ya umaskini au utajiri bali kwetu hicho chakula hakikuwepo wakati nakuwa (ila leo kipo ingawaje si kwa saana).
 
TZ kuna makabila yaliyokuwa nyuma kimasomo na kibiashara, lakini yalkuwa na sifa za kuchapa kazi. Ila uchapa kazi wao ulikuwa ni wa kuwatumikia watu wengine. Kula na makabila yaliyopata elimu mapema kupitia wamisionari na hiyo elimu iliwapa nguvu ya kiuchumi.

Wakinga ni kabila lilokuwa nyuma kielimu lakini walikuwa wachapa kazi wazuri saana. Ila uchapakazi wa Wakinga ulikuwa ni kutumikishwa kwenye majumba na mashamba ya Wanyakyusa. Baada ya uhuru na mbiu ya mwalimu Nyerere ya kujitegemea, Wakinga waliaangalia mbali na kubaini kuwa mafanikio yao yako katika kujitegemea na sio kuajiriwa. Waliacha kazi za kutumikishwa na kutumia nguvu zao kujiinua, ndioy maana baada ya muda mfupi matajiri wakubwa maeneo ya huko wakawa Wakinga. Hadithi hiyo hapo juu ilikuwa kweli kwa wenyeji wa Mbeya Wasafwa. Sasa hivi Wasafwa nao wako juu kiutajiri kuliko Wanyakyusa. Utajiri wa Wanyayusa ulishuka baada ya kukosa cheap labor ya Wasafwa na Wakinga. So goes the story!
 
Nilipoona ubini huo ngajiro nikajua ni mkinga, wakinga utajiri wao???!unakuta tajiri but analala chooni au anavaa ndala mdongeo(tofauti mguu huu na ule) na kingine kumbe ana undugu na fadhili ngajiro aliyekuwa anatia nia jimbo la iringa kumbe??
Una maana alijenga choo na anaitumia kama chumba cha kulala. Sasa naamini akutukanae hakuchagulii.
 
We utajiri wa mnyakyusa hujashuka mpaka leo nenda huko Tukuyu utawaona,, wasafwa mpaka wengi wao bado wanaishi pembezoni mwa miji,, wanapenda kuchunga ngo'mbe na kuleta maziwa mjini!
 
Katika machawa wa Fredi kuna lile bonge mie aisee huwa simuelewagi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Sema jamaa linajituma kama ndakuwa sijafananisha au kukosea ana kampuni ya kutengeneza vifungashio.
 
yaani utajiri kwa kujibana mpaka kula, na chakula bora ni kande,maharage na mboga za majani?[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] daaah.

Hakuna tajiri anayejua makande.
Tajiri anayekula makande ni maskini aliyechangamka tu.
 
fred vunja bei mshamba, ushamba ndio unaomsumbua hana utajiri wowote wa maana hela yote inaishia kwenye kujitangaza ili awe star. hana hela hizo mnazofikiria
Fred ana hela wewe.
Tajiri kijana.
Alisikika chawa mmoja akisema
 
Wasafwa akili zao kama wagogo. Akili ndogo sana
 
Utajiri ni kula nini ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…