Freedom speech sio freedom ya kutukana

Developer IOS

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2017
Posts
1,456
Reaction score
1,410
Habari wanabodi,Kumekuwa na mkanganyiko katika tafsiri sahihi ya uhuru wa maoni ulioruhusiwa kikatiba
Uhuru wa Maoni Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.

Ukisoma vipengele vya katiba vinaelezea wazi kuwa uhuru huo wa kutoa maoni unatakiwa usiathiri sheria za nchi

Nia ya kufanya uchochezi Sheria Na 18 ya 1950 kif. 2; Sura 455
55.-(1) Nia ya kufanya uchochezi ni nia ya:-
(a) ya kuleta chuki au kudharau au kuchocheza, kutopenda dhidi ya mamlaka halali ya Jamhuri ya Muungano au Serikali yake;
au (c) kuleta chuki au kudharau au hamasa ovu ya kuwafanya dhidi ya utawala wa sheria katika Jamhuri ya Muungano; au (d) kupandisha hali ya kutoridhika au kudharau baina ya wakazi wa Jamhuri ya Muungano; au (e) kukuza hisia za nia mbaya na chuki baina ya aina mbali mbali za watu wa Jamhuri ya Muungano.

Lugha chafu, mzozo, na kutishia kutumia wa nguvu. Sheria Na. 48 ya 1948 kif. 2; 14 ya 1950 kif. 9; 49 ya 1955 kif. 7; na Sheria Na. 12 ya 1962
(1) Mtu yeyote ambaye- (a) anatumia lugha chafu, ya matusi au ya usafihi kwa mtu mwingine yoyote kwa namna ambayo huenda ikaleta uvunjifu wa amani; au

Ukiangalia sheria za nchi hapo juu na ukiangalia uhuru wa kutoa maoni wanaoutaka upinzani uchwara utagundua upinzani wetu uchwara wanashindwa kutofautisha kati ya uhuru wa kutoa maoni na uhuru wa kutukana.Tanzania tuna utamaduni wetu ambao unabainisha wazi kuwa sio vizuri kutukana kuwabeza na kuwadhihaki watu waliotuzidi umri au viongozi wetu.

Sio tu ni kinyume cha dini bali hata dini na sheria za Mungu muumba mbingu na ardhi anakataaa

Qur’an chapter 4:59, “O ye who have believed, obey Allah and obey His Messenger and the people of authority amongst you. And if you disagree over anything, return the matter to Allah and His Messenger (Muhammad, pbuh) if you truly believe in Allah and the Last Day. That is the best [way] and best in result.”
Qur’an chapter 4:59, “O ye who have believed, obey Allah and obey His Messenger and the people of authority amongst you. And if you disagree over anything, return the matter to Allah and His Messenger (Muhammad, pbuh) if you truly believe in Allah and the Last Day. That is the best [way] and best in result.”
Imam Al-Fudhayl Ibn ‘Iyadh (RA) said: “If I have a good prayer (that will be accepted by Allah), I will make it for the leader. We have been commanded to pray for them with goodness and we have not been commanded to curse them even if they are transgressors and oppressors. This is because their injustice would only be on their necks (as sins) and their being upright (because of good supplications for them) will be for them and for us.” (Alwajeez fee ‘Aqeedah as-Salaf)
Waroma 13:1
Kila mtu na ajitiishe* kwa mamlaka zilizo kubwa,+ kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kupitia Mungu;+ mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.+ 2 Kwa hiyo, yeyote anayepinga mamlaka amechukua msimamo dhidi ya mpango wa Mungu; wale ambao wamechukua msimamo dhidi ya mpango huo, watajiletea hukumu wao wenyewe.

Hivyo wakuu naomba kuwataka ndugu zangu kueheshimu katiba na kutofautisha uhuru wa kujieleza na uhuru wa kutukana hivyo kuacha mara moja kuwadhihaki na kutukana viongozi wetu kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na katiba yetu , utamaduni wetu pamoja na kwenda kinyume na Mungu muumba mbingu na ardhi
 
Masenu ulichukua muda gani kukaa chini, kufikiria na kuandika haya uliyoandika?
 
Ndugu,Watu hawakuumbwa kwa ajili ya sheria,bali sheria imewekwa na watu.Kwa mujibu wako inaonekana kabisa hujui tofauti kati ya tusi na kuambiwa ukweli na hujui tofauti ya uchochezi na kuwafumbua watu fikra.Dunia ya sasa imebadilika,katika hali ya kawaida ni vibaya kuonyesha umajinuni katika maswala ambayo kimsingi lazima yasemwe wazi.Ninachoona katika Jamhuri yetu ni tabia ya viongozi kutopenda kusikiavile wasivopenda basi.Hili taifa lina sheria ila kama hizo sheria zinakinzana na matakwa ya hali halisi ni wajibu wetu kusemA KWA SAUTI MPAKA KILA MTU ASIKIE NA KUELEWA.

Nakutakia kila la heri katika jitihada zako za kumuunga mkono ili usijisahau na kuacha kuangalia utendaji wake kwa jicho la tatu,Tusiweke nchi yetu rehani kwa watu wenye uchu wa madaraka
 
Acha kuwadanganya watu, wewe jamaa ni mpuuzi sanaa, sheria ulizozitumia hapo karibu zote zilishafutwa au kufanyiwa marekebisho makubwa. Pumbavu sana
 
Speech nimaneno/mawazo yaliyopangiliwa yanayotoka kwenye kinywa cha mtu au yaliyo wasilishwa kwenye mfumo wa maandishi na hata audio , nia ni yawafikie watu wengne ili waweze kujifunza , kupongeza , kushauri na hata kukosoa.
Tukianza hapo , Freedoom of speech" ni hali ya kuwasilisha hayo mawazo yaliyopangiliwa kwa uhuru pasi kuvunja sheria ( kutumia matusi) .
Shida yangu inaanzia hapa kwetu ili uonekane umeutumia vizuri huo uhuru basi ni lazima umsifie huyo aliekupa huo uhuru hatakama anapaswa kukosolewa.
Nadha ni wakati muafaka sasa wakuubadilisha huo uhuru kutoka kuwa "FREEDOM OF SPEECH nakuwa FREEDOM OF SUPPORTIG" nadhan kwa tafsiri hyo hatutaweza kugombana teena...

Nimawazo yangu tu.. cdhan kma kunaubaya nikiishia hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…