Pre GE2025 Freeman Mbowe: CHADEMA ina Mashujaa wasiokata tamaa, ni bora tufe tumesimama kuliko tuishi tumepiga magoti!

Pre GE2025 Freeman Mbowe: CHADEMA ina Mashujaa wasiokata tamaa, ni bora tufe tumesimama kuliko tuishi tumepiga magoti!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, ameibukia Kanda ya Kaskazini kwenye kikao cha kazi, siku chache baada ya uzushi wa tukio la kupewa sumu. Katika hotuba yake, Mbowe alikumbusha dhamira ya kuanzishwa kwa chama hiki miaka 33 iliyopita, akisisitiza kuwa malengo yao ni makubwa kuliko changamoto zinazowakabili.

“Wakati wote tukikumbuka dhamira ya kuanzishwa kwa chama hiki, lazima iwe kubwa kuliko kutekwa kwetu, kupoteza mali zetu na kupoteza fursa yoyote. Licha ya yote tuliyoyapitia, sote tulisimama na leo tumekuwa mashujaa,” alisema Mbowe, akionesha imani katika nguvu ya chama chake.

Akiweka wazi hali ya kisiasa nchini, Mbowe alisisitiza kwamba ukuaji wa CHADEMA unachangia mivutano ya kisiasa. “Utomvu wa nidhamu ni madhara ya kukua; ukiona chama cha siasa hakina mivutano, hicho ni chama mfu,” alisema. Aliwakumbusha wanachama wa CHADEMA kuwa, tofauti na vyama vingine vilivyoshindwa, wao wamechagua kusimama imara, badala ya kukata tamaa.
Pia, Soma:
-> CHADEMA Kufanya Mikutano 105 kwa siku 21 tu Kanda ya Kaskazini, Lissu na Mbowe kuongoza Mashambulizi
-> Mbowe: Kuna Watu wanasema Nina mgogoro na Tundu Lissu nawaambia Watasubiri sana, Chopa inaanza operation Karatu na Nitakuwa na Tundu Lissu!
-> Mbowe: Siwezi gombana na Lema, mama yake atanipigia Simu
-> Freeman Mbowe mwanasiasa, mfanyabiashara na mkulima asiye ogopa hasara
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ametoa wito kwa viongozi wa chama hicho kuwa na uthabiti na kutoingia kwenye hofu au kukata tamaa. Akizungumza kwenye kikao cha kazi katika Kanda ya Kaskazini, Mbowe alisema ameona roho ya kukata tamaa na hofu miongoni mwa baadhi ya viongozi waandamizi, hali ambayo haipaswi kuruhusiwa katika uongozi.

"Baada ya kuwasikiliza viongozi waandamizi, nimeona maumivu, nimeiona roho isiyokubalika ya kukata tamaa, roho ya hofu na kurejea nyuma, jambo ambalo nakemea na halipaswi kufanywa na viongozi wakati wowote," alisema Mbowe kwa msisitizo.

Mbowe aliendelea kwa kusisitiza kuwa uongozi si kazi rahisi, bali ni mzigo mzito kama msalaba. Alisema, "Uongozi ni gunia la misumari, na kwa kiongozi asiyekubali kushushwa, kukanyagwa, kutukanwa, au kudharauliwa, hawezi kuwa kielelezo sahihi cha kipimo cha uongozi."

Mbowe alihitimisha kwa kuwahimiza viongozi kuwa imara na kutokata tamaa katika juhudi za kuimarisha chama, akiwataka wawe mfano wa uvumilivu na uthabiti kwa wanachama na taifa kwa ujumla.
Soma, Pia:
=> Freeman Mbowe: CHADEMA ina Mashujaa wasiokata tamaa, Wengine walisalimu Amri, ni bora tufe tumesimama kuliko tuishi tumepiga magoti
=> Lissu ambana Mbowe: Aelezea Historia yake, adai hajawahi omba kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, "Nimekijenga chama kwa jasho na nguvu zangu"
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, ameibukia Kanda ya Kaskazini kwenye kikao cha kazi, siku chache baada ya uzushi wa tukio la kupewa sumu. Katika hotuba yake, Mbowe alikumbusha dhamira ya kuanzishwa kwa chama hiki miaka 33 iliyopita, akisisitiza kuwa malengo yao ni makubwa kuliko changamoto zinazowakabili.

“Wakati wote tukikumbuka dhamira ya kuanzishwa kwa chama hiki, lazima iwe kubwa kuliko kutekwa kwetu, kupoteza mali zetu na kupoteza fursa yoyote. Licha ya yote tuliyoyapitia, sote tulisimama na leo tumekuwa mashujaa,” alisema Mbowe, akionesha imani katika nguvu ya chama chake.

Akiweka wazi hali ya kisiasa nchini, Mbowe alisisitiza kwamba ukuaji wa CHADEMA unachangia mivutano ya kisiasa. “Utomvu wa nidhamu ni madhara ya kukua; ukiona chama cha siasa hakina mivutano, hicho ni chama mfu,” alisema. Aliwakumbusha wanachama wa CHADEMA kuwa, tofauti na vyama vingine vilivyoshindwa, wao wamechagua kusimama imara, badala ya kukata tamaa.
Pia, Soma:
-> CHADEMA Kufanya Mikutano 105 kwa siku 21 tu Kanda ya Kaskazini, Lissu na Mbowe kuongoza Mashambulizi
-> Mbowe: Kuna Watu wanasema Nina mgogoro na Tundu Lissu nawaambia Watasubiri sana, Chopa inaanza operation Karatu na Nitakuwa na Tundu Lissu!
-> Mbowe: Siwezi gombana na Lema, mama yake atanipigia Simu
-> Freeman Mbowe mwanasiasa, mfanyabiashara na mkulima asiye ogopa hasara
mashujaa gani na walikusaliti wote kwenye maandamano yako haramu ya kukurupuka? acha upotodhaji wa wazi chairman alaaa.. :pulpTRAVOLTA:
 
Mungu ambariki mwenyekiti wetu. Historia itampa tuzo nyingi sana
Ni kweli bila Chadema hata Barabara zinazojengwa zisingekuwapo. Wanajenga eti kwa kuwakomesha wapinzani kumbe sisi ndo tunafaidika. CHADEMA oyeeeeeeeeee!!!! Kwa hiari yao ccm wanadharau sana.
 
Mwamba kama Mwamba

1000012480.jpg
 
Kwi Kwi Kwi.

CHADEMA ni laana kubwa sana kuwahi kutokea, sio Tanzania tu, bali bara zima la Afrika.

Wanachama wake ndio Usiseme.

======
Masaliti hawa.
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, ameibukia Kanda ya Kaskazini kwenye kikao cha kazi, siku chache baada ya uzushi wa tukio la kupewa sumu. Katika hotuba yake, Mbowe alikumbusha dhamira ya kuanzishwa kwa chama hiki miaka 33 iliyopita, akisisitiza kuwa malengo yao ni makubwa kuliko changamoto zinazowakabili.

“Wakati wote tukikumbuka dhamira ya kuanzishwa kwa chama hiki, lazima iwe kubwa kuliko kutekwa kwetu, kupoteza mali zetu na kupoteza fursa yoyote. Licha ya yote tuliyoyapitia, sote tulisimama na leo tumekuwa mashujaa,” alisema Mbowe, akionesha imani katika nguvu ya chama chake.

Akiweka wazi hali ya kisiasa nchini, Mbowe alisisitiza kwamba ukuaji wa CHADEMA unachangia mivutano ya kisiasa. “Utomvu wa nidhamu ni madhara ya kukua; ukiona chama cha siasa hakina mivutano, hicho ni chama mfu,” alisema. Aliwakumbusha wanachama wa CHADEMA kuwa, tofauti na vyama vingine vilivyoshindwa, wao wamechagua kusimama imara, badala ya kukata tamaa.
Pia, Soma:
-> CHADEMA Kufanya Mikutano 105 kwa siku 21 tu Kanda ya Kaskazini, Lissu na Mbowe kuongoza Mashambulizi
-> Mbowe: Kuna Watu wanasema Nina mgogoro na Tundu Lissu nawaambia Watasubiri sana, Chopa inaanza operation Karatu na Nitakuwa na Tundu Lissu!
-> Mbowe: Siwezi gombana na Lema, mama yake atanipigia Simu
-> Freeman Mbowe mwanasiasa, mfanyabiashara na mkulima asiye ogopa hasara
hata katika familia mitaani huko kuna watoto huwa wanacheza michezo ya kuigiza kama wakubwa ndiyo chadema wanachokifanya ni michezo ya kitoto lakini kamwe hawawezi kushika dola wataishia kucheza michezo yao ya kitoto tu
 
Kwi Kwi Kwi.

CHADEMA ni laana kubwa sana kuwahi kutokea, sio Tanzania tu, bali bara zima la Afrika.

Wanachama wake ndio Usiseme.

======
Masaliti hawa.
CCM ni genge la kigaidi linalotumia mabavu ya vyombo vya dola kuendeleza utawala wake wa kidhalimu.
 
Back
Top Bottom