Freeman Mbowe mishale mingi lakini hachoki, hapoi. Je ana mrithi?

Freeman Mbowe mishale mingi lakini hachoki, hapoi. Je ana mrithi?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Mbowe ni mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambapo amedumu madarakani kwa muda mrefu akijaribu kumfukuzia Baba wa Taifa kwa muda ambao aliiongoza TANU hatimaye CCM tangu uhuru hadi alipoamua kung'atuka kwa hiyari yake.

Ingawa tuampiga mishale mingi bwana Mbowe lakini ameendelea kuwa nguzo ya CHADEMA hasa kuelekea kwenye mitaguso ya kisiasa. Pamoja na kufanyiwa hila za kihuni na CCM kuitumia NHC kuporomosha biashara zake ambazo amezirithi kutoka kwa baba yake.

Hivi karibuni alikabiliwa na kesi ya kubumba ya ugaidi ambapo kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani, sisi kama jamii tulifunguka macho kugundua UKATILI mkubwa unaofanywa na CCM kupitia jeshi la polisi ambao wanatumika kudhibiti upinzani wa kisiasa dhidi ya CCM

Swali ambalo kama jamii ya wadadisi wa siasa za Tanzania tunapaswa kupata majibu ni kuhusu succession plan, kwamba baada ya yeye ameandaliwa nani kupokea kijiti kuweza kuipeleka CHADEMA kwenye kufanikisha malengo yake ya kuongoza dola kwa manufaa ya Watanzania?

Kiongozi makini ni yule ambaye anaongoza huku akiandaa watu wanaoweza kuongoza dira na malengo ya taasisi.

Uzi huu siyo sehemu ya shinikizo la kumtaka ang'oke madarakani
 
Ngoja waje

Awali Mbowe alimuandaa Halima James Mdee lakini baada ya Usaliti sasa anamwangalia zaidi John Heche wa Tarime na Salum Mwalimu wa Unguja
Lakini na Mdee wameshaachana njiapanda.

Kuna tetesi zilivuma mitandaoni kuwa Lisu ndiye anaweza kurithi viatu vya Mbowe.
 
Mbowe ni mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambapo amedumu madarakani kwa muda mrefu akijaribu kumfukuzia Baba wa Taifa kwa muda ambao aliiongoza TANU hatimaye CCM tangu uhuru hadi alipoamua kung'atuka kwa hiyari yake.

Ingawa tuampiga mishale mingi bwana Mbowe lakini ameendelea kuwa nguzo ya CHADEMA hasa kuelekea kwenye mitaguso ya kisiasa. Pamoja na kufanyiwa hila za kihuni na CCM kuitumia NHC kuporomosha biashara zake ambazo amezirithi kutoka kwa baba yake.

Hivi karibuni alikabiliwa na kesi ya kubumba ya ugaidi ambapo kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani, sisi kama jamii tulifunguka macho kugundua UKATILI mkubwa unaofanywa na CCM kupitia jeshi la polisi ambao wanatumika kudhibiti upinzani wa kisiasa dhidi ya CCM

Swali ambalo kama jamii ya wadadisi wa siasa za Tanzania tunapaswa kupata majibu ni kuhusu succession plan, kwamba baada ya yeye ameandaliwa nani kupokea kijiti kuweza kuipeleka CHADEMA kwenye kufanikisha malengo yake ya kuongoza dola kwa manufaa ya Watanzania?

Kiongozi makini ni yule ambaye anaongoza huku akiandaa watu wanaoweza kuongoza dira na malengo ya taasisi.

Uzi huu siyo sehemu ya shinikizo la kumtaka ang'oke madarakani
CHADEMA - Chama cha Demokrasia na Maendeleo,Watu na Maendeleo,Uhuru wa Watu na Maendeleo,kwa tafsiri hiyo UMMA ndiyo wenye mamlaka kuona kuwa nani anafaa kuwa Mwenyekiti wa Chadema siku Mbowe akitoka madarakani na siyo Mbowe kumwandaa mrithi wake.
 
CDM ikipata Dola ndo utakuwa Wakt fasaha wa Mbowe kung'atuka nafasi ya mkt.

Mf Zittow kabwe angepewa uenyekiti enzi zile analeta chikochoko, CDM ingeshakuwa kama NLD.

Narudia kusema Ili Mbowe ang'atuke, ahakikishe CDM inashuka DOLA.
Ametangaza kustaafu 2023
 
Back
Top Bottom