WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 963
Filamu ni moja ya kazi za sanaa zenye kuelimisha, kuburudisha na pia kuingiza kipato.Binafsi napenda sana Filamu na nafuatilia sana maendele ya fani ya filamu hapa Tanzania.Nakumbuka miaka ya nyuma, nyingi ya filamu zilizotamba zaidi katika kumbi za sinema enzi hizo – Drive-in, Avalon,New Chox,Empire, Empress,Odeon ( Dar Es salaam), Majestic kule Tanga, Shaan kule Morogoro, Tivoli - Mwanza, Plaza – Moshi, ni sinema zilizokuwa zinatengenezwa Hollywood na Bollywood kwa maana ya Marekani na India.Polepole majumba hayo yakapoteza umaarufu hasa baada ya watu kuanza kujipa raha wenyewe katika sebule zao kwa maana ya video n.k.
Polepole Filamu za kinaigeria nazo zikapanda chati na kupendwa sana thanks to Nollywood productions.Kenya nayo ( sijui Kenya inajiita nini katika hizi xxxxwood LOL)haikubaki nyuma katika kutoa burudani na hasa Kiswahili cha Kenya kiliongeza ladha katika filamu hizo.Kama watanzania, nadhani tulipokea changamoto na kuanza kukomaa katika utengezaji wa filamu – tamthiliya, maigizo n.k.Tukaanza kuona nyota zetu zikijitokeza kuanzia akina Onyango, Mama Haambili( RIP) Mzee Jongo (RIP) wakipanda chati kutoka kuigiza michezo ya redio hadi kwenye Filamu za kwenye TV.Vijana machachari kama akina Ray – Vincent Kigosi, Nora, Dr Cheni, Kanumba,Irene Uwoya, na wengine wengi wakaanza kung'ara na kuiweka Tanzania katika ramani – thanks to Tollywood productions.
Tumeona wasanii wetu kadhaa kama Kanumba, Ray C,Mwisho na sasa Richard Bezuidhouit ( Big Brother winner 2007) wakipata fursa kubadilishana ujuzi kwa kwenda kuigiza na wasanii waliokomaa wa Nigeria kama akina Nkiru Sylvanus, Damijo, Vivien Nnamji,Ngozi Ezeoni nakadhalika.Hii inatia moyo sana.Na kuonyesha kuwa sanaa hii inakuwa kwa kasi, Filamu za Tanzania zinaonyeshwa siyo ndani ya Tanzania tu, bali hadi nje ya mipaka.Thanks to Multi-choice/M-net na TBC arrangements.LAKINI kuna tatizo linalohitaji kushughulikiwa haraka nalo ni la lugha.Nyingi ya filamu zetu ziko kwa Kiswahili which is good.Lakini ili kupanua soko na kuingizia kipato wahusika inabidi kuangalia ni vipi hili litafanyika.Nimeona filamu nyingi zikiwekewa sub-titles za Kiswahili – hii ni mbinu nzuri na rahisi zaidi kuliko kulazimisha wasanii kuigiza kwa kiingereza au ku superimpose kiingereza kwenye filamu za Kiswahili.TATIZO kubwa liko kwenye utafsiri wa maneno kwenye hizo sub-tiles , kuandika maneno ya kiingereza na pia grammar.Binafsi nimekuwa nikijiuliza, kwani wahusika hawatafuti wahariri kupitia na kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuzirusha hewani tena nje ya mipaka?
Hebu tujadili tuone wenzetu hawa tunawasaidia vipi.
Polepole Filamu za kinaigeria nazo zikapanda chati na kupendwa sana thanks to Nollywood productions.Kenya nayo ( sijui Kenya inajiita nini katika hizi xxxxwood LOL)haikubaki nyuma katika kutoa burudani na hasa Kiswahili cha Kenya kiliongeza ladha katika filamu hizo.Kama watanzania, nadhani tulipokea changamoto na kuanza kukomaa katika utengezaji wa filamu – tamthiliya, maigizo n.k.Tukaanza kuona nyota zetu zikijitokeza kuanzia akina Onyango, Mama Haambili( RIP) Mzee Jongo (RIP) wakipanda chati kutoka kuigiza michezo ya redio hadi kwenye Filamu za kwenye TV.Vijana machachari kama akina Ray – Vincent Kigosi, Nora, Dr Cheni, Kanumba,Irene Uwoya, na wengine wengi wakaanza kung'ara na kuiweka Tanzania katika ramani – thanks to Tollywood productions.
Tumeona wasanii wetu kadhaa kama Kanumba, Ray C,Mwisho na sasa Richard Bezuidhouit ( Big Brother winner 2007) wakipata fursa kubadilishana ujuzi kwa kwenda kuigiza na wasanii waliokomaa wa Nigeria kama akina Nkiru Sylvanus, Damijo, Vivien Nnamji,Ngozi Ezeoni nakadhalika.Hii inatia moyo sana.Na kuonyesha kuwa sanaa hii inakuwa kwa kasi, Filamu za Tanzania zinaonyeshwa siyo ndani ya Tanzania tu, bali hadi nje ya mipaka.Thanks to Multi-choice/M-net na TBC arrangements.LAKINI kuna tatizo linalohitaji kushughulikiwa haraka nalo ni la lugha.Nyingi ya filamu zetu ziko kwa Kiswahili which is good.Lakini ili kupanua soko na kuingizia kipato wahusika inabidi kuangalia ni vipi hili litafanyika.Nimeona filamu nyingi zikiwekewa sub-titles za Kiswahili – hii ni mbinu nzuri na rahisi zaidi kuliko kulazimisha wasanii kuigiza kwa kiingereza au ku superimpose kiingereza kwenye filamu za Kiswahili.TATIZO kubwa liko kwenye utafsiri wa maneno kwenye hizo sub-tiles , kuandika maneno ya kiingereza na pia grammar.Binafsi nimekuwa nikijiuliza, kwani wahusika hawatafuti wahariri kupitia na kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuzirusha hewani tena nje ya mipaka?
Hebu tujadili tuone wenzetu hawa tunawasaidia vipi.