damian marijani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2010
- 695
- 466
Leo nataka nitoe mada hii kuhusu fructose. Hii ni aina ya sukari inayopatikana kwenye matunda mbalimbali. Kwa kawaida kuna aina tatu kuu za sukari (simple sugar au monosaccharides) nazo ni: glucose, fructose na galactose (inayopatikana kwenye maziwa).
Fructose inapoliwa haisababishi kupanda kwa sukari katika damu kwa sababu inabidi iwe processed kwenye ini iweze kugeuzwa kuwa glucose. Glucose ndiyo sukari pekee ambayo mwili unaitumia katika viungo mbalimbali kama source of energy. Hivyo basi fructose imekuwa ikitajwa kuwa ni moja ya vyakula vyenye Low glcemic index.
Kwa maelezo hayo hapo juu itaonekana kuwa fructose ni nzuri kuliwa. Hapa nataka kutoa angalizo kuwa sukari hiii inapoliwa kwa kiasi kidogo haina tabu. Lakini inapoliwa kwa kiasi kikubwa ina madhara makubwa.
Baadhi ya madhara hayo ni kama:
Kuwa na mafuta (triglycerides) kwenye mzunguko wa damu. Hii inatokana na kushindwa kwa ini kuprocess fructose wakati inapoliwa kwa wingi. hivyo ini linatengeneza mafuta aina ya Triglycerides ambayo yanaweza kusababisha ugonjwa wa moyo.
Fructose inaweza kusababisha kuongeza hamu ya kula (appetite) kwa ajili ya kutoweza kuongeza glucose kwenye damu katika kipindi kifupi kama ilivyoelezwa hapo juu.
Matumizi ya fructose kwa wingi inaweza kusababisha kuwa na ugonjwa wa kisukari.
Fructose inapoliwa haisababishi kupanda kwa sukari katika damu kwa sababu inabidi iwe processed kwenye ini iweze kugeuzwa kuwa glucose. Glucose ndiyo sukari pekee ambayo mwili unaitumia katika viungo mbalimbali kama source of energy. Hivyo basi fructose imekuwa ikitajwa kuwa ni moja ya vyakula vyenye Low glcemic index.
Kwa maelezo hayo hapo juu itaonekana kuwa fructose ni nzuri kuliwa. Hapa nataka kutoa angalizo kuwa sukari hiii inapoliwa kwa kiasi kidogo haina tabu. Lakini inapoliwa kwa kiasi kikubwa ina madhara makubwa.
Baadhi ya madhara hayo ni kama:
Kuwa na mafuta (triglycerides) kwenye mzunguko wa damu. Hii inatokana na kushindwa kwa ini kuprocess fructose wakati inapoliwa kwa wingi. hivyo ini linatengeneza mafuta aina ya Triglycerides ambayo yanaweza kusababisha ugonjwa wa moyo.
Fructose inaweza kusababisha kuongeza hamu ya kula (appetite) kwa ajili ya kutoweza kuongeza glucose kwenye damu katika kipindi kifupi kama ilivyoelezwa hapo juu.
Matumizi ya fructose kwa wingi inaweza kusababisha kuwa na ugonjwa wa kisukari.