Hatimae ile siku tuliyokuwa tukiisubiria imefika, ni bonge la mechi kati ya Azam na Yanga katika fainali ya kombe la shirikisho la CRDB
Mechi hii itachezwa majira ya saa 2:15 usiku pale kwenye dimba la New Amaan Complex, Zanzibar
Je, nini kitatokea katika mtanange huo wa kukata na shoka?
Kuwa nami hapa kuanzia Mwanzo, Katikati na Mwisho wa mechi hii
#CRDBBankFederationCup #KombeLaShirikisho #KombeLaShirikishoLaCRDBBank #TFF #AzamFC #YangaSC #AzamvsYanga
----------------------------------------------------------
Updates 1920 Hours
Kikosi cha Yanga: Diara, Yao, Lomalisa, Bacca, Job (C), Aucho, Maxi, Mudathir, Mzize, Aziz Ki na Pacome
Subs: Mshery, Mwamnyeto, Kibabage, Mkude, Sureboy, Shekhan, Farid, Guede, Musonda...
Kocha : Gamondi Miguel / Musa Ndao
----------------------------------------------------------
Kikosi cha Azam: Mohamed, Lusajo (C), Msindo, Fuentes, Bangala, Bin Zayd, Adolf, Sopu, Kipre Jr, Feitoto, Syllah
Subs: Foba, Chilambo, Amoah, Manyama, Akaminko, Sidibe, Nado, Chiwalanga, Kichindo
Kocha : Bruno Ferry/Yusuf Dabo
----------------------------------------------------------
2015 Hours Kick off
01" Yanga wameanzisha mpira hapa
06" Timu bado zinashambuliana kwa zamu, na zinajaribu kusomana
Azam 0 Yanga 0
10" Azam wanashambulia hapa kuelekea Yanga lakini Abdul Sopu anakuwa offside hapa
15" Presha ya shambulizi ni kubwa kwa Azam lakini wanajaribu kuzima Shambulio la Pacome Zouzoua (0-0)
18" Azam wanapata faulo ila inazuiwa na ukuta wa mabeki wa Yanga
23" Sopu Anapiga kona kuelekea Yanga, chupuchupu Mzize ajifunge inakuwa kona tena... azam wanaipiga inaokolewa Yanga wanashambulia Mzize anakosa goli hapa..
27" Aziz Ki anapiga shuti pale lakini Kipa wa Azam anautoa nje kwa ustadi..
30" Aziz Ki anadondoshwa na Adolf, Yanga wanapata faulo inapigwa pale Mustafa Mohamed anaitoa nje..Kona inapigwa wanaokoa Azam
AZM 0 YNG 0
35" Bado ngoma ngumu 0-0, Yanga wanamiliki mpira zaidi, Pacome anakosa umakini ananyang'anywa mpira
41" Azam wanashambulia kwenda Yanga, Beki wa Yanga wanakuwa imara wanazuia shambulizi (0-0)
45" Azam wanashambulia kwenda Yanga..Kipre anaangushwa faulo...Job anapewa kadi njano
3 dakika kuelekea halftime
45+2 Feitoto anamchezea faulo Lomalisa...Njano kadi kwa Feitoto
HALFTIME AZAM 0 YANGA 0
----------------------------------------------------------
Updates 2120 Hours
KIPINDI CHA PILI KIMEANZA
45" Azam wanaanzisha mpira hapa kuelekea Yanga
51 " Lomalisa anamjaribu kipa wa Azam, mpira unaenda nje..Kona fupi inapigwa anaukata Aucho lakini unadakwa
54" Kadi ya njano kwa Mudathir akimuangusha Kipre kwa kushirikiana na Aucho
61" Yanga wanapata faulo baada ya pacome kuangushwa na Msindo..Faulo inapigwa inaokolewa
67" Yao anarusha mpira kuelekea Azam, naona Aziz ki hajaelewana na Yao mpira unaenda nje..Goal kick