FT|| Horoya AC 1-0 Simba SC | CAF Champions League | Stade General Lansana Conte | 11.02.2023

FT|| Horoya AC 1-0 Simba SC | CAF Champions League | Stade General Lansana Conte | 11.02.2023

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Ni msimu mwingine wa Ligi ya Mabingwa Africa. Leo hapa nyumbani Tanzania ni sikukuu kwa wapenda kandanda hasa soka la kuvutia, Samba Loketo.

Wawakilishi wa Tanzania, katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba SC leo majira ya saa 1:00 usiku atashuka dimbani huko nchini Guinea, kuchuana na Horoya AC katika dimba la Stade General Lansana Conte.

Simba ambao wamejizolea umaarufu linapokuja suala la mechi za kimataifa, wamekuwa wakifanya vizuri sana watashuka dimbani wakiwa na lengo la kupata matokeo mazuri hasa baada ya vinara wa kundi lao Raja kuibomoa Vipers 5-0 katika mchezo uliopigwa jana usiku.

Simba itawakosa baadhi ya wachezaji kama Jonas Mkude, Augustine Okrah, Saido Ntibazonkiza ambao wamebaki nyumbani Tanzania kutokana na sababu mbalimbali.

Mchezo utakuwa mubashara kupitia ZBC2 katika Kisimbuzi cha AzamTv na Chaneli 229 katika kisimbuzi cha DStv.

Karibuni sana kwa live updates...kila la heri kwa mnyama mkubwa mwituni
D8586104-5AF0-481E-8239-50449261CC11.jpeg
 
Tucheze mpira tusikabie kwa macho, attack is the best defence, any sloppy start kesho tunapigwa 3+ Simba ikacheze mpira sio kutafuta draw, with or without the ball, st pieces, reckless fouls, laziness, unnecessary mistakes,
3-4-2-1 ndio formation nzuri Kwa kesho

Watara aliwakosea nini Benchi la ufundi? Nani alimleta Simba SC.
 
Outarra ni mzito kiasi hana kasi, mechi za kimataifa unahitaji wachezaji sharp vinginevyo tutaoigwa kama ngoma. Angalia akina juko walivypigwa 5-0 kama wamesimama jana
Tucheze mpira tusikabie kwa macho, attack is the best defence, any sloppy start kesho tunapigwa 3+ Simba ikacheze mpira sio kutafuta draw, with or without the ball, st pieces, reckless fouls, laziness, unnecessary mistakes,
3-4-2-1 ndio formation nzuri Kwa kesho

Watara aliwakosea nini Benchi la ufundi? Nani alimleta Simba SC.
 
Mechi muhimu sana kwetu...Ukiangalia ubora wa timu zote kwenye hili kundi utagundua hawa ndio wenye nafasi yetu ya kufuzu. Raja yeye ana asilimia kubwa ya kusonga hatua nyingine kwa kuzingatia ubora wake lakini pia matokea aliyopata leo yanadhihirisha wao ni wakubwa. Mwingine ni kati ya sisi(Simba) na Horoya, Vipers hatumdharau lakini ugeni wake na hiki kipigo alichopokea cha tano bila, huenda asiwe tishio sana. Tufe nao hawa, kama tusipowafunga basi tutoe droo, ikibidi kbs tuwape ushindi mwembamba. Tusiwachukulie poa hawa sio wanyonge kiivyo!
 
Mechi muhimu sana kwetu...Ukiangalia ubora wa timu zote kwenye hili kundi utagundua hawa ndio wenye nafasi yetu ya kufuzu. Raja yeye ana asilimia kubwa ya kusonga hatua nyingine kwa kuzingatia ubora wake lakini pia matokea aliyopata leo yanadhihirisha wao ni wakubwa. Mwingine ni kati ya sisi(Simba) na Horoya, Vipers hatumdharau lakini ugeni wake na hiki kipigo alichopokea cha tano bila, huenda asiwe tishio sana. Tufe nao hawa, kama tusipowafunga basi tutoe droo, ikibidi kbs tuwape ushindi mwembamba. Tusiwachukulie poa hawa sio wanyonge kiivyo!
Vipers kawaiga kula gwara uarabuni
 
Back
Top Bottom