FT: Ligi Kuu Bara | Azam FC 1-1 Simba SC | Uwanja wa Chamazi Complex | Mei 18, 2022

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Vuguvugu na patashika na mshike mshike ya Ligi Kuu Tanzania Bara NBC Premier League kuendelea kupigwa leo Mei 18, 2022 ambapo Wana lamba lamba Azam FC wanamkaribisha Mnyama Mkali Mwituni Simba SC kwenye Uwanja wa Chamazi Complex.

Mchezo utakuwa mgumu na pia ushindani wa aina yake, Azam FC wanafatuta alama tatu muhimu ili kuwapelela kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu, huku Simba SC akizitaka alama tatu ili kupunguza gepu na kuweka presha kwa kinara wa Ligi Kuu.

Azam FC kwa sasa wamekuwa na changamoto kwenye eneo la ulinzi, kwani wamekuwa wakiruhusu magoli siku za karibuni, kwenye eneo la Uzuiaji 'Defensive' wamekuwa wakifanya makosa mengi kiasi cha kugharimu timu.

Simba SC anakwenda kwenye mchezo huu akiwa na from nzuri ya ushindi kwa siku za karibuni huku safu yake ya ushambuliaji ikionekana kurudisha 'Confidence' hali ya kujiamini, hivyo ni ngumu kuona Azam FC wakijizuia dakika zote kutofanya makosa.

Kocha msaidizi wa Azam FC, amesema kuwa, ligi safari hii ni nzuri sana, kwasababu kila timu inataka matokeo kwa mechi yake, wanakwenda kucheza na Simba SC, na mechi itakuwa ngumu lakini wanaahidi kuondoka na alama zote tatu.

Naye Kocha Pablo Franco wa Simba SC amesema kuwa, itakuwa mechi bora sana, kwa vile timu zote zinapenda kucheza mpira nzuri hivyo inakuwa mechi bora sana ambayo mashabiki watafurahia kuiangalia kwasababu kila timu ina wachezaji wazuri, hivyo watacheza kadri ya uwezo wao kuona kama watapata chochote Chamazi.

Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1:00 Usiku. Usikose Ukaambiwa

Kulipewa Mwana..Kulitaka Mwana


================

Kikosi cha Azam FC:

Kikosi cha Simba:

Mchezo umeanza Uwanja wa Chamazi Complex

2' Azam FC wanapata kona, inapigwa Bocco anaokoa.
3' Mchezo una kasi, timu zote zinaonekana kuuchezea mpira
4' Simba wanafanya shambulizi, Kibu Denis anapiga kichwa langoni lakini mpia unaokolewa.
8' Mchezo ni wa kushambuliana baina ya timu zote
10' Azam FC wanafika langoni mwa Simba lakini Aishi Manula anakuwa makini
14' Simba wanafanya shambulizi lakini mpira unatoka nje.
16' Roders Kola wa Azam FC anapata kadi ya njano kwa kucheza faulo
22' Sakho anapiga shuti linagonga nguzo na kurejea uwanjani
28' Faulo kadhaa zinatokea kwa pande zote mbili
29' Simba wanaongeza kasi ya mashambulizi
33' Azam FC wanafika langoni kwa Simba, wanapata faulo lakini Manula anadaka mpira
37' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Rodgers Kola anafunga bao kwa Azam FC

44' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Bocco anaifungia Simba kwa kichwa akimalizia mpira uliopigwa na Shomari Kapombe
45' Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola anazozana na mwamuzi wa kati.
45' MAPUMZIKO

Kumbuka kuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Nabi yupo uwanjani akishuhudia mchezo huu

Kipindi cha pili kinaanza
48' Simba wameanza na mashambulizi kwa kasi
51' Azam FC wanapiga faulo inaokolewa na walinzi wa Simba.
58' Muzamiru Yassin anachezewa faulo kwa kugongwa kichwani, mchezo umesimama akipatiwa matibabu
62' Prince Dube anawapita walinzi wa Simba na kupiga shuti kali linaokolewa na Manula inakuwa kona
65' Simba wanajibu shambulizi kali, shuti la Kibu Denis linapaa juu ya lango la Azam FC
68' Mchezo umefunguka, kasi na kushambuliana kwa zamu
74' Mashambulizi ni makali kwa zamu zamu
76' Banda anabaki na kipa wa Azam lakini anashindwa kuweka mpira wavuni
78' Azam wanapiga pasi kadhaa na kumiliki mpira
83' Mchezo ni mzuri na mashabiki wanashangilia
83' Daniel wa Azam FC yupo chini ameumia
90' Zinaongezwa dakika tatu za nyongeza.

FULL TIME: AZAM FC 1-1 SIMBA
 
Kwenye michezo mitano ya mwisho Azam FC, wameshinda mmoja na sare mmoja na wamepoteza mitatu

Leo tena Azam anadonosha alama tatu dhidi ya Simba SC Mnyama.
 
Lini aliwahi kupata hizo pointi? Zaidi ya kuachia?
Azam ni simba b ipo kushindana na yanga
Nyie si mnakubaliana na kiemba kuwa Yanga na Azam ni mechi inayo chukuliwa kwa ukubwa wa fainali na kwamba mechi ya Azam na Simba ni mechi ndogo tu kwao, sasa malalamiko haya yanatokea wapi?
 
Azam aka simba b tayari wamepewa maagizo na Bakhressa kuwa waachie simba mbovu ifunge..

Mechi mbovu kuwahi kutokea
Hii mechi kama wachezaji wote wa Azam na bench la ufundi na uongozi wao wataiona hii mechi ina umuhimu kwao kupata nafasi ya top four, basi Azam watashinda au watatoa sare. Lakini kama wataingia kucheza mechi ili kumfurahisha boss wao ambaye ni Simba kindaki kindaki kuwa mechi ya leo isiwe tiketi ya Yanga kujipa uhakika wa ubingwa kwa zaidi yaasilimia 90, basi watazioga leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…