FT: Pre-season International Friendly Match | Simba SC 6-0 Al Akhood Club

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Klabu ya Simba imejitupa uwanjani hii leo kwenye mchezo wa Kimataifa wa kirafiki (International Friendly match) dhidi ya Al Akhaood Club, ambapo matokeo ni kuwa Simba SC imeibuka na ushindi mnono wa mabao sita kwa bila.

Huu ni mchezo wa pili kwa Simba baada ya kutanguliwa na ule wa Ismailia SC ambao matokeo yalikuwa ni kutoshana nguvu kwa sare ya bao moja kwa moja, ambapo bao la Simba likifungwa na Nyota Augustine Okrah.

Kwenye mchezo wa leo Julai 23, 2022 matokeo ni haya | FT: Simba SC 6-0 Al Akhaood Club.

Wafungaji Simba SC.

Moses Phiri
Jonas Mkude
Maddie kagere
Pape Sakho
Pape Sakho
Erasto Nyoni

 
Kwenye list ya wafungaj umedanganya
 
Ila hapa naona kama simba wanatakiwa watuweke sawa. Kwa mtazamo wangu na nilichokiona ni kwamba ahmed ally yey amepost tumecheza na abo hamad ya misr na huku page ya simba imepost al akhood.

Hiv hii ni tmu moja ina majina tofaut au ni vip na ukiangalia hyo al akhood ni ya saud arabia au misr pia ipo?
NB. Mkaangalie kwanza kweny post zao mjiridhishe
 
Mkuu usihangaike bila sababu chukua hii na baki na hii hapa Simba SC Vs Akhaood Club
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…