Binafsi niliutazama mpira.
Azam walifungwa goli kutokana na uzembe wa mabeki, kwani walicheza offside triki, na mchezaji mwingine wa Prison ambaye hakuwa offside akaponyoka akaenda kufunga kirahisi.
Pamoja na kufungwa, Azam inabaki timu yenye wachezaji wenye vipaji na timu imeunganika.
Kilichowaletea shida Azam ni uwanja hauko level, yaani mpira unadunda dunda kwenye pichi, hivyo pasi hazipigwi vizuri wala hazituliziki, wala mchezaji ha-dribo vizuri.
Hili wanatakiwa Azam walifanyie kazi kwa kujizoesha kucheza kwenye viwanja vibovu, ambapo wanatakiwa wawe wanapiga mipira mirefu, badala ya kutaka kulifikia lango la mpinzani kwa pasi fupi fupi wakati uwanja ni mbaya!
Azam wakicheza uwanja mzuri ni tishio.
Sent from my TECNO F1 using
JamiiForums mobile app