FT: Simba SC 3-1 Singida Big Stars | Estadio Benjamin Mkapa | 03/02/2023

FT: Simba SC 3-1 Singida Big Stars | Estadio Benjamin Mkapa | 03/02/2023

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Majira ya Saa 1:00 Usiku kwa Masaa ya Afrika ya Mashariki,Mnyama mkubwa mwituni, Simba SC watashuka dimbani katika dimba la Benjamin Mkapa kuwakaribisha wana alizeti Singida Big Stars.

Mechi inategemewa kuwa ngumu, maana katika mchezo wa kwanza pale Liti, Singida, timu hizo zilitoshana nguvu kwa sare ya 1-1.

Simba itashuka dimbani ikiwategemea wachezaji wake mahiri kama Chama, Saido, na wengineo huku Singida Big Stars ikiwategemea zaidi akina Bruno, Kazadi na mastaa wengneo.

Je, Simba ataweza kuzoa alama zote tatu? Au Singida ndio atakayeibuka kidedea? Tukutane saa 1:00 usiku kwa live updates...

Ubashiri wangu: Simba 2-1 Singida
 
Nikatika muendelezo wa mbilinge mbilinge za ligi kuu NBC, leo hii mnyama mkali SIMBA SC Dhidi ya walima alizeti SINGIDA BS, Kunako uwanja wa Benjamin Mkapa, leo hii nyasi zitawaka moto pale wanaume 22 watakapokua wanatunisha misuli kutetea timu zao katika kusaka alama 3 muhimu zitakazo wafanya wakae vizuri katika msimamo wa ligi, Simba akitaka kumkaribia mtani wake Yanga na mpinzani pekee ktika kuuwania ubingwa, na Singida akipigania nafasi ya 3 dhidi ya wana lambalamba azam fc, je ni mnyama atalipa kisasi cha kulazimisha sare ya 1-1 nakupunguzwa kasi ya kuuwania ubingwa, ama singida ataendelea kutonesha kidonda na kudidimiza matumaini ya mnyama katika kuufukuzia ubingwa? Tuwe wote hapa kuanzia saa 1:00 kwa updates.
Ghazwat mwana kulitaka mwana kulipata.
 
Majira ya Saa 1:00 Usiku kwa Masaa ya Afrika ya Mashariki,Mnyama mkubwa mwituni, Simba SC watashuka dimbani katika dimba la Benjamin Mkapa kuwakaribisha wana alizeti Singida Big Stars.

Mechi inategemewa kuwa ngumu, maana katika mchezo wa kwanza pale Liti, Singida, timu hizo zilitoshana nguvu kwa sare ya 1-1.

Simba itashuka dimbani ikiwategemea wachezaji wake mahiri kama Chama, Saido, na wengineo huku Singida Big Stars ikiwategemea zaidi akina Bruno, Kazadi na mastaa wengneo.

Je, Simba ataweza kuzoa alama zote tatu? Au Singida ndio atakayeibuka kidedea? Tukutane saa 1:00 usiku kwa live updates...

Ubashiri wangu: Simba 2-1 Singida
Hivi katika lile Shindano lenu la Mwanachama Bora wa Jukwaa la Michezo ( Sports ) hapa JamiiForums liliisha kwa nani kuwa Mshindi? Nilitamani sana niwepo ili nami nipige Kura yangu.
 
Majira ya Saa 1:00 Usiku kwa Masaa ya Afrika ya Mashariki,Mnyama mkubwa mwituni, Simba SC watashuka dimbani katika dimba la Benjamin Mkapa kuwakaribisha wana alizeti Singida Big Stars.

Mechi inategemewa kuwa ngumu, maana katika mchezo wa kwanza pale Liti, Singida, timu hizo zilitoshana nguvu kwa sare ya 1-1.

Simba itashuka dimbani ikiwategemea wachezaji wake mahiri kama Chama, Saido, na wengineo huku Singida Big Stars ikiwategemea zaidi akina Bruno, Kazadi na mastaa wengneo.

Je, Simba ataweza kuzoa alama zote tatu? Au Singida ndio atakayeibuka kidedea? Tukutane saa 1:00 usiku kwa live updates...

Ubashiri wangu: Simba 2-1 Singida
SIMBA 3-0
 
Hivi katika lile Shindano lenu la Mwanachama Bora wa Jukwaa la Michezo ( Sports ) hapa JamiiForums liliisha kwa nani kuwa Mshindi? Nilitamani sana niwepo ili nami nipige Kura yangu.
Unajisikiaje pale unapojitekenya na kucheka mwenyewe? Kabla ya kuja kuandika hapa, nilijaribu kuangalia ile ID yako pendwa ya game changer! Nikakuta tayari umeme umepita!!

Shida ni nini hasa? Mbona unakula sana umeme?
 
Unajisikiaje pale unapojitekenya na kucheka mwenyewe? Kabla ya kuja kuandika hapa, nilijaribu kuangalia ile ID yako pendwa ya game changer! Nikakuta tayari umeme umepita!!

Shida ni nini hasa? Mbona unakula sana umeme?
Wewe ndiyo uliyeulizwa Swali? Acha Kiherehere kama Mfuko wa Shati sawa?
 
Back
Top Bottom