FT: Yanga S.C 3-1 Geita Gold | NBC Premier League | Chamazi Complex | 12.03.2023

mzee wa bwaksi

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2021
Posts
2,255
Reaction score
3,972
Machampioni watetezi wa ligi kuu nchini Tanzania Young Africans S.C almaarufu Yanga leo wanashuka dimbani kuzisaka alama 3 dhidi ya Geita Gold kutoka mkoani Geita katika mwendelezo wa ligi kuu ya Nbc...

Mchezo huo utakuwa mgumu kwa timu zote kwani Yanga wanataka kushinda ili kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi huku na Geita nao wakiitaji alama zote tatu ili kujiweka sawa kwenye msimamo wa ligi.
Ikumbukwe kuwa toka wamepanda ligi kuu, Geita Gold wamepoteza Michezo yote waliyokutana na Yanga hivyo mchezo wa leo utakuwa mgumu zaidi maana wamepania kufuta uteja kwa Yanga.

Mchezo utapigwa majira ya saa 12:15 jioni pale katika dimba la Azam Chamazi Complex

 
Na,Iona goli za kutosha, Mayele [emoji460][emoji460], Musonda[emoji460][emoji460], Mzize[emoji460][emoji460], Aziz[emoji360][emoji460][emoji460]
Morison [emoji460]

Yanga 9-1 Geita gold. Goli la Geita atajifunga zawadi mauya
 
Kama Geita haijawahi kuishinda yanga, sasa itakuwaje kwa mechi hii ya leo ambayo yanga inazihitaji zaidi alama tatu kuliko Geita wanavyozihitaji, tusubiri samaki kuliwa na mtu, badala ya mtu mwenye njaa kula samaki.
 
Kama Geita haijawahi kuishinda yanga, sasa itakuwaje kwa mechi hii ya leo ambayo yanga inazihitaji zaidi alama tatu kuliko Geita wanavyozihitaji, tusubiri samaki kuliwa na mtu, badala ya mtu mwenye njaa kula samaki.
Mechi itakuwa ngumu mkuu maana Geita watacheza wame relax maana hawako kwny hatihati yakushuka Wala kuingia top 4, Wakati Yanga watakuwa wana tension kubwa kuhakikisha gape la point 8 linarudi
 
Yanga bana wanajitajiaga mijigoli miiingii wanaishi 1 wakjitahidi 2
Tumekubaliana humu ligi ya ndani kuwa anaetembeza bahasha zaidi ndio anayefunga magoli mengi, kwaio Simba mnaongoza kutembeza bahasha.
Na mkasema kipimo kizuri kipo kule kimataifa, Aya Yanga ameshafunga magoli 6 kimataifa Simba imefunga magoli 2 tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…