Fuata njia hizi kulinda wazo lako la biashara

Fuata njia hizi kulinda wazo lako la biashara

chuma jr

Member
Joined
Oct 17, 2015
Posts
88
Reaction score
135
Kutokana na kutembea sana humu JF nimekutana na baadhi ya member wakiuliza njia za kutumia ili waweze kulinda mawazo yao ya biashara mimi kama member mwenzenu nilikuwa katika sintofahamu hiyo nilikuwa sijui wapi niende nikalihifadhi wazo langu kisheria hivyo nilipita humu lakini sikupata muelekeo rasmi sababu wengine walitaja BRELA ndipo unaenda kusajiri wazo wengine walisema cosota lakini kidogo nilipata idea kisha nikajiongeza hivyo ningependa kuleta mrejesho na muongozo utakaowasaidia members wengine wenye mawazo ya biashara lakini hawajui wapi wakasajiri ili endapo kama wanaenda kuomba ufadhili wa mtaji au kuomba partner wa biashara unakuwa na hofu ya kuibiwa wazo lako na usiwe pa kumpeleka huyo mtu sasa fuata njia hizi.

1}Andika au record hilo wazo lako ukirecord hakikisha linahifadhiwa kwenye CD na sio sehemu tofauti na CD
hakikisha wazo lako linakuwa kwenye mtiririko ufuatao
a}mwanzo-hapa mwanzo unaanza kutoa kama muhtasari wa wazo lako.
b}katikati-hapa ndipo unaliweka wazo lako lote bila kubakisha.
c}Mwisho- hapa unahitimisha kwa kutoa matarajio yako kama wazo lako likianza kufanya kazi ni faida zipi unazitarajia kama ni faida binafsi au na taifa kiujumla.

Ukishaliandaa hilo wazo kwa mtiririko huo nenda COPYRIGHT SOCIETY TANZANIA (COSOTA) ukiwa na karatasi iliyobeba hilo wazo lako au CD iliyokuwa na sauti yako au ya mtu mwingine aliyerekodi ukienda huko andaa 10,000 ya fomu then 20,000 ya kujisajiri yani ada ya mwaka hiyo kuwa mwanachama then 1,000 ya kujaza fomu ya usajiri wa kazi yako jumla unatakiwa kuwa na 31,000 tu ila viambatanisho muhimu lazma uwe na kitambulisho na pasport size mbili hapo kwenye kitambulisho unatoa copy ndipo unawapatia ila sijajua kama cha shule kinatumika.

Baada ya kujaza fomu zote utakazopewa na ukilipia hiyo 31,000Tsh utasubiri wazo lako lipitiwe na wana baraza la cosota hao ndo wataamua kama kweli linahitajika kuhifadhiwa kama wazo unique au ni wazo ambalo lishawahi kusajiriwa hivyo tayari lina mwenyewe kama ni wazo jipya halijawahi kuonekana na halina utata wowote basi utapewa hati ya umiliki wa hilo wazo lako lakini hiyo hati utailipia elfu 10,000 tu hivyo utakuwa na uwezo wa kwenda kwa mtu ukaliwasilisha hilo wazo na asikuzidi akili na kwa usalama wake unaweza kumuonesha ile hati ya cosota ili ajue kuwa unalilinda kisheria lakini pia ukishakuwa mwanachama pale cosota unaweza kusajiri wazo lingine na lingine na mengi zaidi au kazi yoyote ya ubunifu wako utasajiri kwa elfu moja 1000 utasubiri baraza lipitie hiyo kazi yako kisha utalipia elfu kumi 10,000 ya kuchukua hati ya umiliki hivyo kila kazi utakayo isajiri itapewa hati yake.

Lakini kama wazo lako tayari lishakuwa developed yani linafanya kazi tayari lakini unaweza kulilinda pia ukaenda kusajiri kama kampuni au biashara ili mtu asiweze kufuata nyayo zako akaleta ushindani hiyo kama ukipenda mwenyewe lakini sio lazma.

Yangu ni hayo tu ndugu zangu kutokana na msaada ninaoupata kupitia members wa JF hivyo na mimi nimeona nisiwe mchoyo kushare nanyi huu utaratibu najua kuna wengi wanapitia hali ya kutokujua ni wapi watayalinda mawazo yao ya biashara kisheria ili yasichukuliwe hivyo nadhani hii itasaidia watu wengi sana,ADMINS mnaweza kupin hii thread ikae juu ili ionekane kirahisi na kama sijaiweka kwenye jukwaa linalohitajika mnaweza kunisaidia kuipeleka kwenye jukwaa husika.

ASANTENI SANA
 
Very informative thread, asante sana kwa kutujuza utaratibu huu kwa sie ambao tulikua hatufahamu!
 
Ina maana wazo la biashara ni siri?.... ukishaliweka public lazima watu walicopy tu
Hapa nazungumzia situation ambazo tunapitia vijana wengi tunakuwa na IDEAS lakini ukiangalia mtaji wa kutekeleza hiyo project yako hauna so unahitaji mtu akusapoti sasa niambie mtu umempelekea idea yako halafu anaikataa baada ya muda akiitafakari kwa umakini anaona ni idea ambayo itatengeneza pesa nzuri tu hapo ataamua kukusariti na kuifanya yeye hata kama akikusaidia atakuita ukawe kibarua wa kawaida ambae hautonufaika.

Zaidi ya kupokea mshahara wa mwisho wa mwezi na ukiangalia ile ni idea yako na hauna pa kumpeleka kisheria hivyo ni muhimu kulinda idea yako kisheria na sijamaanisha kuwa wazo la biashara ni siri haliwezi kuwa siri hata siku moja kama ni wazo hai na unahitaji litokee kuwa biashara kamili sababu hata kama usipoenda kuomba msaada wa kifedha kwa mtu lakini si ipo siku litakuwa biashara kamili sasa watu si watacopy hiyo biashara pia hivyo haliwezi kuwa siri ila lengo ni kulinda hakimiliki yako mkuu wangu.
 
Kama utafuata utaratibu uliotolewa na mtoa mada ..utakuwa umelilinda wazo lako. Hiyo nakubali, na je mwingine akifanya editing akafuata utaratibu huo huo na kusajili itakuwaje?
 
Hakuna wazo jipya...Kumbuka kuwa ukijarifiria nakuenda kuliwekea Copyright kuna aliliwaza na hana pesa ya copyright.. so ukilitumia ni ka unamuonea. Hata likiwa na Copyright mtu ypypte anaweza litumia kwa kubadili maneno machache tu......

Njia pekee nayo amini kuhusi kulinda wazo lako..Nikuliweka katika vitendo..Ndipo kuliombea Copyright. Hapo hata mtu akiliiba na kulitumia, atakamatwa oale itakapo onekana wewe umeanza kulifanyia kazi mapema sana.
 
hapa nazungumzia situation ambazo tunapitia vijana wengi tunakuwa na IDEAS lakini ukiangalia mtaji wa kutekeleza hiyo project yako hauna so unahitaji mtu akusapoti sasa niambie mtu umempelekea idea yako halafu anaikataa baada ya muda akiitafakari kwa umakini anaona ni idea ambayo itatengeneza pesa nzuri tu hapo ataamua kukusariti na kuifanya yeye hata kama akikusaidia atakuita ukawe kibarua wa kawaida ambae hautonufaika na zaidi ya kupokea mshahara wa mwisho wa mwezi na ukiangalia ile ni idea yako na hauna pa kumpeleka kisheria hivyo ni muhimu kulinda idea yako kisheria na sijamaanisha kuwa wazo la biashara ni siri haliwezi kuwa siri hata siku moja kama ni wazo hai na unahitaji litokee kuwa biashara kamili sababu hata kama usipoenda kuomba msaada wa kifedha kwa mtu lakini si ipo siku litakuwa biashara kamili sasa watu si watacopy hiyo biashara pia hivyo haliwezi kuwa siri ila lengo ni kulinda hakimiliki yako mkuu wangu.
mi naona njia nzuri ya kulinda wazo la biashara ni kuliweka public ..halafu unaweka onyo yoyote atakaefanya biashara kama hiyo unamshtaki.....
 
Nafikiri hatuelewani hapa ..
Kwani wazo la biashara linalindwa ili iweje? Mfano una wazo la biashara ya kufuga nguruwe kwa kutumia teknolojia inayotumika nchi jirani ... utamkataza vipi mwingine asifanye hivyo?

Ina maana wewe kama wazo lako linafanya kazi ngazi ya mkoa, na mikoa iko zaidi ya ishirini, ni kwa nini wengine wasifanye kwa mikoa inayobaki.

Ubinafsi ndo unaturudisha nyuma.
 
Nafikiri hatuelewani hapa ..
Kwani wazo la biashara linalindwa ili iweje? Mfano una wazo la biashara ya kufuga nguruwe kwa kutumia teknolojia inayotumika nchi jirani ... utamkataza vipi mwingine asifanye hivyo?

Ina maana wewe kama wazo lako linafanya kazi ngazi ya mkoa, na mikoa iko zaidi ya ishirini, ni kwa nini wengine wasifanye kwa mikoa inayobaki.

Ubinafsi ndo unaturudisha nyuma.
Mkuu nadhani hii siyo maana ya mtoa mada, kwa jinsi nilivyomuelewa kwa mfano wewe Tutor B una idea yako lakini huwezi kupata capital kwa sasa hivyo unakuja kunishirikisha ili mimi bunyebunye nitoe pesa na wewe utoe wazo hilo, kisha tugawane kutokana na makubaliano yetu.

Lakini kwa uswahili na kugeuka kwa sababu mimi nina pesa na wazo pia nimeshalipata kutoka kwako naamua kufanya peke yangu.

Hivyo kama umefuata utaratibu aliotoa hapo juu mtoa mada unaweza kupata msaada COSOTA.
Ahsante.
 
Mkuu nadhani hii siyo maana ya mtoa mada, kwa jinsi nilivyomuelewa kwa mfano wewe Tutor B una idea yako lakini huwezi kupata capital kwa sasa hivyo unakuja kunishirikisha ili mimi bunyebunye nitoe pesa na wewe utoe wazo hilo, kisha tugawane kutokana na makubaliano yetu.

Lakini kwa uswahili na kugeuka kwa sababu mimi nina pesa na wazo pia nimeshalipata kutoka kwako naamua kufanya peke yangu.

Hivyo kama umefuata utaratibu aliotoa hapo juu mtoa mada unaweza kupata msaada COSOTA.
Ahsante.
Ni lini ulisikia COSOTA wamemsaidia mtu? Hivyo vyombo vipo kimaslahi zaidi wala havifanyi chochote. Hata hawa sijui TFDA, TBS hakuna wanachokifanya zaidi ya kukusanya hela .

Nilisajili kinywaji (spirit) nikafuata utaratibu wote .. na nikapewa documents zote. Haikupita muda serikali ikatangaza kuondoa viroba kwenye soko la vinywaji .. hadi naandika hapa sikupata msaada wowote.

Kama una wazo lako la biashara mshirikishe mwenye mtaji mfanye kazi lakini hakikisha kuna kitu unakifanya wewe kama wewe ili kulinda wazo lako.

Narudia COSOTA hawatakusaidia kwa lolote; mwenye pesa ni wa kuogopa.

Hapa mimi nasambaza mbolea ya maji .. sijapata pesa kwa ajili ya kusajiri, wapo wanaonifuata na kunishauli tushirikiane tukasajili .. nawakatalia. Ninachokifanya ni kwamba nimekuwa na shamba darasa ambapo wale wanaobisha kwamba mbolea yangu haijasajiriwa nawaeleza kuwa kusajiri ni kutafutia ulaji wengine.

Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno.
 
Back
Top Bottom