Full blood picture ni kipimo gani? Je, nikipima kipimo cha Full blood picture kila ugonjwa mwilini mwangu utaonekana?

Full blood picture ni kipimo gani? Je, nikipima kipimo cha Full blood picture kila ugonjwa mwilini mwangu utaonekana?

Joined
Apr 28, 2017
Posts
30
Reaction score
73
Full blood picture ni kipimo gani? Je, nikipima kipimo cha Full blood picture kila ugonjwa mwilini mwangu utaonekana?

Full blood picture au Full blood count kimekuwa ni kipimo kinachosikika sana kikitajwa mara nyingi kila tuendapo kupata huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Ukitumia tafsiri ya moja kwa moja kutoka kingereza kwenda Kiswahili ni rahisi kufikiri Full blood picture inaonyesha kila kitu mwilini, la hasha sio kweli, Full blood picture haioneshi kila kitu au kila ugonjwa mwilini tofauti na jina lake linavyosema.

Uhalisia ni kuwa Full blood picture inaangalia aina tu za seli katika mfumo wa mwili wa mwanadamu na wala sio magonjwa yote mwilini unavyoweza kudhani.

Full blood picture inaangalia aina kuu tatu za seli mwilini. Seli hizi ni chembe seli nyeupe “white blood cell”, chembe sahani” platelets” na seli za damu “ red cell line”.

Tukianza na seli nyeupe au kitaalam “white blood cells” hizi ni seli kinga zinazohusika na kuulinda mwili usipate au upambane pale upatapo magonjwa. Hizi ni seli ambazo huongezeka kwa wingi kipindi mtu kapata maradhi au infection kama ambavyo mara nyingi utaambiwa ukienda hospitali, hii nimeiongelea kwenye makala nyingine .

unaweza kugusa kiunganishi hiki kuisoma makala ya infection kwa kina hapa Kila nikienda hospitali naambiwa nina Infection, Infection ni nini? na kwanini kila mara naambiwa nina infection?

Chembe sahani au platelets hizi ni seli zinazohusika na ugandaji wa damu mwilini.

Seli za damu au kitaalam red cell line hizi zinaonesha wingi wa damu, na kama damu imepungua mwilini kipimo hiki kinaweza kikakupa viashiria ni kwanini damu inapungua, mfano kama ni upungufu wa madini chuma n.k

Kwa kifupi kabisa bila kwenda ndani kabisa hivi ndo vitu ambavyo Full blood picture inaonyesha na sio magonjwa yote mwilini kama ambavyo jina la kipimo linasema au unaweza kudhani linamaanisha.

Mwisho kabisa , majibu na usahihi wa kipimo hiki utategemea na ubora wa machine ya kupima kipimo hiki, ubora wa kemikali “ reagent “ inayotumika kupima, uhodari wa mtu anayekutafsiria majibu ya kipimo hiki maana sio kila mtu anaweza kusoma na kutafsri kwa usahihi kabisa kipimo hiki.

Shukrani za kipekee sana kwako ambaye umesoma mpaka hapa chini, nakutakia afya njema kabisa katika mapambano yako ya kila siku.
 
Mbona jina lake linavyosema ndio uhalisia ulivyo,naona wewe unasema kwamba kipimo hakina maana kama jina lake lilivyo,kana kwamba jina hili linaelezea kitu tofauti,no jina lake na maana yake ni ile ile.

full blood licture = inachukua picha ya damu nzimaaa ya mwili.

Na aina za damu ni tatu.
Damu nyeupe = ulinzi
Damu Nyekundu = kontawa,msambazaji wa huduma muhimu za mwili
Na damu sahani.= husaidia kupunguza damu kumwagika.
 
Mbona jina lake linavyosema ndio uhalisia ulivyo,naona wewe unasema kwamba kipimo hakina maana kama jina lake lilivyo,kana kwamba jina hili linaelezea kitu tofauti,no jina lake na maana yake ni ile ile.

full blood licture = inachukua picha ya damu nzimaaa ya mwili.

Na aina za damu ni tatu.
Damu nyeupe = ulinzi
Damu Nyekundu = kontawa,msambazaji wa huduma muhimu za mwili
Na damu sahani.= husaidia kupunguza damu kumwagika.
Noted, issue ni baadhi ya watu akipima full blood picture ikawa normal anakwambia amepima kipimo cha kuangalia mwili nzima na hana ugonjwa ilihali anaumwa
 
Full blood picture ni kipimo gani? Je, nikipima kipimo cha Full blood picture kila ugonjwa mwilini mwangu utaonekana?

Full blood picture au Full blood count kimekuwa ni kipimo kinachosikika sana kikitajwa mara nyingi kila tuendapo kupata huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Ukitumia tafsiri ya moja kwa moja kutoka kingereza kwenda Kiswahili ni rahisi kufikiri Full blood picture inaonyesha kila kitu mwilini, la hasha sio kweli, Full blood picture haioneshi kila kitu au kila ugonjwa mwilini tofauti na jina lake linavyosema.

Uhalisia ni kuwa Full blood picture inaangalia aina tu za seli katika mfumo wa mwili wa mwanadamu na wala sio magonjwa yote mwilini unavyoweza kudhani.

Full blood picture inaangalia aina kuu tatu za seli mwilini. Seli hizi ni chembe seli nyeupe “white blood cell”, chembe sahani” platelets” na seli za damu “ red cell line”.

Tukianza na seli nyeupe au kitaalam “white blood cells” hizi ni seli kinga zinazohusika na kuulinda mwili usipate au upambane pale upatapo magonjwa. Hizi ni seli ambazo huongezeka kwa wingi kipindi mtu kapata maradhi au infection kama ambavyo mara nyingi utaambiwa ukienda hospitali, hii nimeiongelea kwenye makala nyingine .

unaweza kugusa kiunganishi hiki kuisoma makala ya infection kwa kina hapa Kila nikienda hospitali naambiwa nina Infection, Infection ni nini? na kwanini kila mara naambiwa nina infection?

Chembe sahani au platelets hizi ni seli zinazohusika na ugandaji wa damu mwilini.

Seli za damu au kitaalam red cell line hizi zinaonesha wingi wa damu, na kama damu imepungua mwilini kipimo hiki kinaweza kikakupa viashiria ni kwanini damu inapungua, mfano kama ni upungufu wa madini chuma n.k

Kwa kifupi kabisa bila kwenda ndani kabisa hivi ndo vitu ambavyo Full blood picture inaonyesha na sio magonjwa yote mwilini kama ambavyo jina la kipimo linasema au unaweza kudhani linamaanisha.

Mwisho kabisa , majibu na usahihi wa kipimo hiki utategemea na ubora wa machine ya kupima kipimo hiki, ubora wa kemikali “ reagent “ inayotumika kupima, uhodari wa mtu anayekutafsiria majibu ya kipimo hiki maana sio kila mtu anaweza kusoma na kutafsri kwa usahihi kabisa kipimo hiki.

Shukrani za kipekee sana kwako ambaye umesoma mpaka hapa chini, nakutakia afya njema kabisa katika mapambano yako ya kila siku.
Cc Full Blood Picture njoo kujibu hapa
 
Full blood picture inahusika na matatizo yote ya damu sehemu mbali mbali za mwili na mifumo yake,hakipimi magonjwa mengine
Hadi ngoma?maana juzi kati nimeenda hospital daktari kaniandikia hicho kipimo,wakt wa kunisomea majibu akaniambia tu mbona nina damu nyingi afu sidonate?nikataka kumuuliza umejuaje na wakati hujanipima ngoma?
 
Ahsantee kwa Somo hili zuri. [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Hadi ngoma?maana juzi kati nimeenda hospital daktari kaniandikia hicho kipimo,wakt wa kunisomea majibu akaniambia tu mbona nina damu nyingi afu sidonate?nikataka kumuuliza umejuaje na wakati hujanipima ngoma?
kipimo hiki hakipimi ngoma, kuwa na damu nyingi kinaonesha (Hb)level, lakini pia na kuwa na damu nyingi sio kigezo cha kudonate,
wachangiaji damu wote wanatoaga damu zao hivyo hivyo una ngoma, homa ya ini au hauna, wakifika maabara wanapima hizo damu zilizokuwa donated, kama haina shida yeyote inakuwa inafaa kwa matumizi, kama ina ngoma au magonjwa mengine yanayoambukiza kwa njia ya damu inatupwa,
lakini pia benki ya damu hutoa majibu ya damu yako kwa baadhi ya magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya damu baadae kama ukitaka majibu yako
 
Hadi ngoma?maana juzi kati nimeenda hospital daktari kaniandikia hicho kipimo,wakt wa kunisomea majibu akaniambia tu mbona nina damu nyingi afu sidonate?nikataka kumuuliza umejuaje na wakati hujanipima ngoma?
Afection yoyote kwenye blood itaonekana...wingi ama kupungua kwa damu haina uhusiano na maambukizi ya damu(kama yapo)
 
Back
Top Bottom