Full Time: Azam FC 1- 4 Yanga SC | Community Shield | Final | Benjamin Mkapa Stadium | 11/08/2024

Full Time: Azam FC 1- 4 Yanga SC | Community Shield | Final | Benjamin Mkapa Stadium | 11/08/2024

kiwatengu

Platinum Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
18,585
Reaction score
16,780
downloadfile.jpg
Match Day
⚽ Azam FC vs Yanga SC
🏟️ Benjamin Mkapa Stadium
🛡️ Community Shield.
📅 11.08.2024
⏰ 7:00pm



#Daimambelenyumamwiko#

Tukutane saa Moja kwa Updates...
Mwanzo mwisho!!

Kikosi Cha Yanga Kinachoanza.
20240811_180924.jpg

KIKOSI CHA AZAM
Screenshot_20240811-181442~2.png
Updates....

Timu zote sasa zinaingia uwanjani ili mchezo uanze kutoka kwa Miamba miwili Yanga SC dhidi Azam FC

Mchezo umeanza sasa.

Dakika 2, Yanga wameaza kwa kasi.

Dakika 4, Max Mpia anakosa nafasi ya kufunga goli.

Dakika 8, Yanga wanajenga shambulizi ila Azam wanaokoa.

Dakika 13, Goooooool Feisal anawapa goli la kuongoza Azam FC.

Dakika 18, goooooooool Dube anawazawashia Yanga.

Dakika 25, Mpira umekuwa wa kasi sana na Diarra anapata kadi ya njano

Dakika 27, Gooooooool Azam wanajifunga na Yanga wanapata goli ya pili.

Dakika 29, Diabi anapata kadi ya njano.

Dakika 30 Goooooool Aziz Ki anapiga msumari wa tatu.

Dakika 35, Azam wanafanya mabadiliko Diabi anatoka.

Dakika 40, Azam wametengeneza nafasi nzuri ya kufunga goli lakini wamekosa kuitumia.

Dakika 2, zimeongezwa kumaliza dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Dakika 45, za kipindi cha kwanza zimetamatika Yanga SC 3- 1 Azam FC.

Kipindi cha pili kimeanza kwa kasi sana.

Dakika 50, Bado timu zote zinacheza kwa tahadhari sana hadi sasa.

Dakika 52, Blanco anapiga shuti kali sana Diarra anaisaidia Yanga kwa kuudaka mpira kwa uzuri kabisa.

Dakika 56 , Mudathir anapata kadi ya njano.

Dakika 59, Adam Adam anaingia

Dakika 71, Mzize anachukua nafasi ya Dube na Bakari Nondo anachukua nafasi Mudathir

Dakika 75, Chilambo na Eva Meza wanachukua nafasi Lusajo na Chama anachukua nafasi ya Aziz Ki kwa upande wa Yanga.

Dakika 85, Yanga wanafanya mabadiliko anatoka Pacome anaingia Musonda na Aucho nafasi yake anachukua ya Andambwile.

Dakika 5 zimeongezwa kumaliza mchezo wa leo .

Dakika 92, Goooooool Mzize anapiga msumari wa nne

Naam Dakika 90 zinatamatika katika Dimba la Benjamini Mkapa Yanga SC ni Bingwa wa Ngao ya Jamii.

Full Time: Yanga SC 4 -1 Azam FC.

Nyie Hamuogopi!
20240811_212043.jpg

 
Back
Top Bottom