Wakuu yamebaki masaa takribani 16 kipenga kipulizwe kuashiria mtanange mkubwa kuanza kati ya Simba na Yanga zote za Dar. Mbali na kuwa ni watani wa jadi timu hizi zina historia kubwa katika mpira wa Tanzania. Mashabiki wana hamasa kubwa wakitegemea mpira na ufundi wa hali ya juu. Kamanda wako ninaahidi kukuletea live updates hapahapa JF kila dakika itakayocheza. Tulia
========
00' Mpira umeanza hapa uwanja wa Taifa
06' Kipa wa Yanga, Mustapha anapiga mpira nje kuashiria kuumia baada ya kudaka mpira wa kona
28' Kiiza anakosa goli baada ya kupewa pasi nzuri na Mustapha kufanikiwa kuutoa
30' Bado milango yote migumu, faulo ya haraka baada ya Awadh wa Simba kuwekwa chini
35' Yanga wanafanya mabadiliko ya wachezaji na Msuva anatoka
39' Hamis Tabwe anaangushwa chini na kugaagaa lakini anaweza kuinuka na kuendelea na mtanange
41' Yanga wanakosa goli baada ya kipa kufanikiwa kuutoa na kuzaa kona ambayo hata hivyo haikuleta mafanikio.
44' :A S soccer:Hamis Tambwe anafanikiwa kuiandikia Yanga bao la kwanza
45+2' Mpira unaenda mapumziko
45' Mpira umerejea baada ya mapumziko
64' Mbuyu Twitte anapewa kadi ya manjano baada ya kucheza ndivyo sivyo
79' :A S soccer:Bao la pili kwa Yanga kupitia kwa Malimi Busungu, Simba 0-2 Yanga
90' Kipa wa Yanga, Mustapha yuko chini na anapewa kadi ya njano kwa kupoteza muda, dakika saba zinaongezwa.
90+8' Mbuyu anapewa kadi ya pili ya manjano na kuwa kadi nyekundu
90+9' Kipenga kinapuliza kuashiria mwisho wa mechi ya leo, Simba 0-2 Yanga.