Fumanizi mara zote huimarisha ndoa..!!

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
!.. FUMANIZI mara zote HUIMARISHA ndoa..!! by Mtambuzi.
Jamani haya si maneno yangu ila ni nikuu kutoka kwa mwana jamvi mahiri, aliyebobea kwenye jukwaa lililotukuka, MMU.
Yeye ni mtaalamu aliyebobea kwenye fani ya kuumizwa na kuvunjwa moyo, kufurahi na kujihisi mko peponi, na mambo mengine yanayofanana na hayo, ambayo kwa ujumla serikali tukufu ya Tanzania iliamua kuyaita ni UZEMBE baada ya Ngoswe kuharibu Nyaraka za sensa.
Jamani naomba kwa kina kabisa tuichambue sentensi hii.
 
Last edited by a moderator:
Huimarisha kama hujalimwa Talaka.....lakini na uaminifu pia unapungua kwa kiasi kikubwa..
 
having conflicts in not a problem. The issue is how confilcts build or break relationships!Your perception and attitude matters a lot!
 
Labda baada ya kushindwa kusababisha talaka au kilema au fedheha za kufededwa (@gfsonwin sijakosea spelling??)
Lakini pia husababisha KUTOAMINIANA!
 
Hasa kama unaweza kunasisha na kudai fidia ya mamilioni kwa mgoni wako na kuweza kuyatumia mamilioni kukuletea heshima!
 
Kwetu Sumbawanga, hatuna haja ya kukunasisha kiunoni, ukiwa unapizi na radi inakutulia hapo hapo, wewe na mwenzako mnaaga dunia na raha zake
asigwa ulipiga tukio nini?
Infidelity ina raha yake, lakini kasheshe lake usilipimie, ni big soo
 
Hasa kama unaweza kunasisha na kudai fidia ya mamilioni kwa mgoni wako na kuweza kuyatumia mamilioni kukuletea heshima!

Hapo limeimarisha ndoa au limemnufaisha mfumanizi????
 
lakini kusema ni rahisi au tukio likitokea kwa mwenzio unaweza sema jamaa wakae waelewane... Wacha lije kwako....
 
Kuna jamaa alimfumania mkewe akiwa anatoa penzi enje ya ndoa, chakushangaza jamaa hakumsemesha mkewe wala nini,
Ila alivyowakuta aliingiza mkono mfukoni na kutoa sarafu ya shilingi 200 na kuirusha juu na kuidaka na kuiingiza mfukoni,
haikuishia hapo alikua anarusha ile hela kila akimuaga mkewe wakati akienda kazini na wakati akirudi nyumbani.

Mke alishindwa kumwelewa mumewe maana alikuwa maana ilikua ni mara mbili anairusha juu ile sarafu
kila wakati anatoa 200 yake na kuirusha juu na baada ya hapo huiingiza mfukoni.

Ilifika kipindi mpaka mke akawa anamwogopa mkewe yaani ikafikia hatua ambapo mke aliamua kuondoka na kumwacha mume mwenyew, huku akijiuliza kwanini mumewe anafanya kitendo kile.

Jamaa aliamua kumfuata mkewe nyumbani kwao na kumuomba warudi nyumbani ila alipofika hapo nyumbani hakusahau kuirudia ile style yake ya kurusha hela ndipo mke alipoendelea kukataa kuondoka na mumewe huku akiropoka aliyomfanyia mumewe. Ndipo wazazi walipoyajua yote.

Muda mchache baadae walirudiana na kuishi pamoja, huku mwanamke akiwa mtiifu na mwaminifu katika ndoa yake.
Hapo tunaona jinsi gani fumanizi lilivyoimarisha ndoa.

CC: Mtambuzi, Speaker, SnowBall, snowhite, Kaunga, Mamndenyi, gfsonwin, Bujibuji, asigwa.
 
Kwani wafumaniwao ni makahaba????????
Wewe unandoa yako umeolewa au unampenzi wako unaanza kutanga tanga hovyo we si kahaba tu, au kunajina lingine zuri ?
 
Hapa ndipo naamini ule usemi wa akili zako changanya na za....
Bujibuji labda uanze wewe application ya huo msemo kwa kujilengeshea fumanizi then ukuje na mrejesho nyuma.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hata mimi huwa natamani kujua kaka Mtambuzi alikuwa na maana gani hapa!
 
Last edited by a moderator:
Kwi kwiiiiii saudari.. Tuambie tu ukweli story yako ya coin ya 200 umetunga lol.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…