!.. FUMANIZI mara zote HUIMARISHA ndoa..!! by Mtambuzi.
Jamani haya si maneno yangu ila ni nikuu kutoka kwa mwana jamvi mahiri, aliyebobea kwenye jukwaa lililotukuka, MMU.
Yeye ni mtaalamu aliyebobea kwenye fani ya kuumizwa na kuvunjwa moyo, kufurahi na kujihisi mko peponi, na mambo mengine yanayofanana na hayo, ambayo kwa ujumla serikali tukufu ya Tanzania iliamua kuyaita ni UZEMBE baada ya Ngoswe kuharibu Nyaraka za sensa.
Jamani naomba kwa kina kabisa tuichambue sentensi hii.
Nakubaliana na hilo kwa kuzingatia conditions zifuatazo!
Wakati mwingine mtu akipendwa anakuwa mpofu na kujiona yeye ndie yeye na wengine wote si lolote si chochote! Wanafikia hadi kuamini huwezi kupata mwingine zaidi yake! Sasa huyu apendwae akiwa mpuuzi, kitakachofuata hapo ni visa na mikasa....anaamini, huwezi kwenda kokote!! Hata hivyo, anafanya hayo wakati nae bado anakupenda!
Sasa mtu huyo siku akaja kukufumania, loh! Ndipo atakapokuja gundua kwamba kumbe u're able kumpata mwingine zaidi yake! Hapo sasa, ndipo atakapojiuliza na kurudi nyuma ili ailinde ndoa yake kwani keshafahamu kwamba, u're able to go anywhere!
Hata hivyo, msumari huo unakuwa mkali zaidi kwake na kumfanya afanye jitihada zaidi za kuilinda ndoa yake ambayo alishaanza kuipuuza; endapo atakufania kwa mtu ambae kwa namna moja au nyingine yupo juu dhidi yake! Say ni mkeo! Ukaja kufumaniwa kwa mwanamke ambae ni mkali zaidi kuliko yeye....aisee, hata kama ulikuwa huwekei maji ya kuoga, utawekewa!
Alternatively, huyo mwenzi wako keshakinahi kabisaa na wewe! Labda anaendelea kuishi na wewe kwa sababu tu anabanwa na mambo fulani fulani! Kwa ndoa kama hiyo, fumanizi lina mchango mdogo sana.....sana sana kitakachotokea ni kwamba, ikiwa nae alikuwa na mwenzi wake wa siri, sasa hatafanya siri tena!! Afanye siri kumuogopa nani wakati na wewe mwenyewe unafanya!